Maskini Serengeti Boys

Makupa

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2011
Posts
6,822
Reaction score
4,034
Kama mnavojua timu ya Taifa ya vijana wa chini ya umri wa miaka 17 inashiriki michuano ya kutafuta bingwa wa afrika .Tanzania ni mwenyejeji wa mashindano husika.Hata hivyo pamoja na kuwa mwenyeji ,timu yetu ni kama imeshatolewa kwani imeshafungwa mechi mbili kati ya tatu inazotakiwa kucheza.Pamoja na kutolewa huko si vibaya tukampa pongezi Mwenyekiti wetu wa uhamisishaji ushindi ambae ni mkuu wa mkoa Mheshimiwa Paul Makondo kwa kujitolea kusimamia jukumu hili kubwa .
 
Serengeti boys ilikuwa ni lazima wafungwe tu...Watu wameingiza siasa kwenye mpira unategemea nini?? Yaani watu wanateuliwa ili wapate umaarufu kupitia hii timu...hovyo kabisa...
 
Timu mbovu Ile ya Gabon ilikuwa nzuri.. Ukimtoa Kevin John hakuna ambaye angepata namba kwenye ile timu ya Gabon.. Tulivyofungwa na Uganda mwaka Jana niliwaandikia TFF kwamba nusu ya wachezaji hawafai wakapuuza
 
Hii Serengeti boys hata ikiomba mechi ya kirafiki na Azania secondary inafungwa ata goal 5
 
Ile timu ya Gabon ilikuwa bora lakini pia ilichangiwa na walimu. Huyu kocha hana uwezo wa kuzisoma timu pinzani uwezo wake ndio umefikia hapo
 
Wacha tubaki kuwa wenyeji watazamaji.
Toka lini zero brain akawa tegemeo la kuleta matokeo chanya?
 
Chochote kinachosimamiwa na Bashite hakifanikiwagi
 
Timu mbovu Ile ya Gabon ilikuwa nzuri.. Ukimtoa Kevin John hakuna ambaye angepata namba kwenye ile timu ya Gabon.. Tulivyofungwa na Uganda mwaka Jana niliwaandikia TFF kwamba nusu ya wachezaji hawafai wakapuuza
Nakuunga mkono mkuu, safu ya ulinzi yote mpaka golini hakuna kitu! Mechi mbili imeruhusu goli 8!
 
Timu ile Watoto wenye vipaji hawachezi wale unaona wazazi wao wametoa pesa
 
Makonda! Yaani anapewa timu makonda?

Ukishindwa nihalali kabisa

Bado Taifa stars nayo itapigwa vilivyo....chini ya makonda vyote hupewa laana
 
Serengeti Boys wamenifurahisha sana. Kuna wanasiasa walitaka wapate sifa kupitia hawa vijana ila vijana wamewaaibisha. Big up Serengeti Boys...mpira siyo siasa. Next time wanasiasa wakae mbali na mpira...bado kaka zao kule Misri lazima wachezee kipigo cha mbwa mdokozi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…