Masomo ya Sayansi jaman

matc

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2012
Posts
260
Reaction score
45
Kiukwel hali ni mbaya sana kwa walimu wa sayansi kwanza idadi yao ni ndogo sana ukilinganisha na hawa wa art na makazin pia hawapo kias kwamba hal ni mbaya sana.Mwl mwenye vipindi vichache anavyo 35 kwa wiki wakat wa art ni 4 mpk 2.
Serikali imeliacha hili kimya na ndo maana linaendelea.Taifa haliwezi kuzalisha wataalamu wa sayans kwa sasa..
Serikaki iweke mishahara tofauti ili pia isaidie kuwapa moyo walimu na kuwavuta wengine kusoma sayansi.
 
Hili ni janga la kitaifa! Na kwa tathmini ya haraka walimu wengi wanaograduate sahz hawana kipaji cha hesabu yaani kifupi ni kwamba wapo shallow they were not born talented to be mathematicians! Hakuna mwl mwenye ufaulu wa darajaB ktk academic certificates zao. Ukiwakuta darasani wanademadema tu na wanafundisha wakiwa wamekunja ndita.
 
na huo ni ukwel hayo ni majanga kwa kwel
 
Serikar inapaswa ipromote walim wa sayans ili watu wawe na mhamko wa kosoma Sayans
 
tatizo sio lipo kwa walimu tu hata wanafunzi wenyewe hawana ari ya kusoma masomo ya sayansi ndio maana walimu nao huwa wanakuwa kama hawaeleweki darasani.
 
Serikali haijaonesha jitihada zozote kuhuisha masomo ya sayansi sielewi kwa nini wanaacha hali hii iendelee kuwa mbaya. kuna wakati Rais Kikwete alinukuliwa kuwa ana mpango wa kuleta walimu wa masomo ya sayansi toka nje ya nchi, Hadi leo kimyaa, kama kawaida yake kuwa na ahadi zisizotekelezeka. Nawashauri walimu wa sayansi wadai usawa wa idadi ya vipindi mashuleni la sivyo mtaendelea kuteseka
 

Ndiyo BRN hiyo...
 
tatizo sio lipo kwa walimu tu hata wanafunzi wenyewe hawana ari ya kusoma masomo ya sayansi ndio maana walimu nao huwa wanakuwa kama hawaeleweki darasani.

Mkuu ari ya mwanafunzi kupenda somo flani haiji from nowhere,lazima awepo mtu,be it ni mwalimu au vinginevyo akupe ile hamu na ukishajenga mapenzi na somo from the very begining,huko mbele unaweza kujisotea mwenyewe.Mwl Maximillian Tungaraza(Mungu akusaidie mwalimu wangu) alinifanya nikapenda sana Biology na Chemistry lakini nimefanya hustles mwenyewe hadi sasa am going to be a medical practitioner.
 

Mkuu sababu ni obvious,they have nothing to loose.Watoto wao wanasomeshwa shule nzuri,sasa wao wahangaikie nini.Na ndio maana hata utaratibu wa kuwapata waalimu wetu tayari ni janga.
 
Sasa mbona unachanganya habari.
Unazungumzia science au mathematics???
 
tatizo sio lipo kwa walimu tu hata wanafunzi wenyewe hawana ari ya kusoma masomo ya sayansi ndio maana walimu nao huwa wanakuwa kama hawaeleweki darasani.

Ni kweli lkn wanafunzi wanafundishwa kwa nadharia mno kwan shule hazina hata maabara..Idadi ndogo ya walimu pia inachangia kwn inafanya walimu washindwe kufuatilia kile watoacho kwa wanafunz..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…