Mwanaume Alivyotumia Sura Mbaya Kupata Umaarufu, Marafiki
Imeandikwa na Kaanaeli Kaale; Tarehe: 14th September 2009
Masoud Sura Mbaya kama anavyojulikana sasa ni msanii ambaye alivuma miaka ya 90 baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika mashindano ya mwanamume mwenye sura mbaya.
Kwa mara ya kwanza alishiriki katika mashindano ya wanaume wenye sura mbaya yaliyofanyika Buguruni Dar es Salaam na kuibuka mshindi wa kwanza ambapo alipata zawadi ya redio.
Mashindano hayo ya kusisimua yalifanyika kwa mara ya pili katika Wilaya ya Kinondoni ambapo, Masoud aliwashinda wasanii wengine maarufu wakiwamo mwanamuziki wa siku nyingi Remmy Ongala na msanii maarufu wa vichekesho Khalid John, maarufu kama Mzee Jangala.
Masoud anasema anaamini kuwa hakuna mwanamume mwenye uwezo wa kumnyanganya nafasi hiyo nchini Tanzania kwa kuwa ana uwezo wa kubadilisha sura yake kwa kutumia hisia mbalimbali. Mimi ni sura mbaya nambari wani Tanzaniawa kunishinda hajapatikana.
Wapo waliojaribu kukata rufaa kupinga ushindi wangu lakini niliwashinda hata kwenye rufaanajivunia ushindi wangu na kila ninapojiangalia kwenye kioo naona wazi kuwa nina haki ya kushinda, anasema Masoud.
Ingawa hivi sasa anajivunia sura yake, maisha yake ya utotoni hayakuwa ya furaha kwa kuwa alichukizwa na tabia ya vijana wenzake waliopenda kumtania kwa kumuita sura mbaya. Kitendo hicho kilimsababishia hasira za mara kwa mara na kujiona mpweke.
Masoud alishiriki pia katika mashindano ya pili ya kumtafuta mwanamume mwenye sura mbaya ambayo yalifanyika Kinondoni na kupata zawadi ya TV baada ya kuibuka mshindi wa kwanza.
Baada ya ushindi huo, Ongala alikata rufaa na kudai kuwa Masoud alipendelewa. Hata hivyo Masoud alishinda katika rufaa hiyo jambo lililomuongezea umaarufu.
Kuanzia kipindi hicho amekuwa akishiriki katika matamasha ya wasanii mbalimbali na sherehe ambapo watu humkodisha ili atoe burudani.
SOURCE: HabariLeo
Imeandikwa na Kaanaeli Kaale; Tarehe: 14th September 2009
Masoud Sura Mbaya kama anavyojulikana sasa ni msanii ambaye alivuma miaka ya 90 baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika mashindano ya mwanamume mwenye sura mbaya.
Kwa mara ya kwanza alishiriki katika mashindano ya wanaume wenye sura mbaya yaliyofanyika Buguruni Dar es Salaam na kuibuka mshindi wa kwanza ambapo alipata zawadi ya redio.
Mashindano hayo ya kusisimua yalifanyika kwa mara ya pili katika Wilaya ya Kinondoni ambapo, Masoud aliwashinda wasanii wengine maarufu wakiwamo mwanamuziki wa siku nyingi Remmy Ongala na msanii maarufu wa vichekesho Khalid John, maarufu kama Mzee Jangala.
Masoud anasema anaamini kuwa hakuna mwanamume mwenye uwezo wa kumnyanganya nafasi hiyo nchini Tanzania kwa kuwa ana uwezo wa kubadilisha sura yake kwa kutumia hisia mbalimbali. Mimi ni sura mbaya nambari wani Tanzaniawa kunishinda hajapatikana.
Wapo waliojaribu kukata rufaa kupinga ushindi wangu lakini niliwashinda hata kwenye rufaanajivunia ushindi wangu na kila ninapojiangalia kwenye kioo naona wazi kuwa nina haki ya kushinda, anasema Masoud.
Ingawa hivi sasa anajivunia sura yake, maisha yake ya utotoni hayakuwa ya furaha kwa kuwa alichukizwa na tabia ya vijana wenzake waliopenda kumtania kwa kumuita sura mbaya. Kitendo hicho kilimsababishia hasira za mara kwa mara na kujiona mpweke.
Masoud alishiriki pia katika mashindano ya pili ya kumtafuta mwanamume mwenye sura mbaya ambayo yalifanyika Kinondoni na kupata zawadi ya TV baada ya kuibuka mshindi wa kwanza.
Baada ya ushindi huo, Ongala alikata rufaa na kudai kuwa Masoud alipendelewa. Hata hivyo Masoud alishinda katika rufaa hiyo jambo lililomuongezea umaarufu.
Kuanzia kipindi hicho amekuwa akishiriki katika matamasha ya wasanii mbalimbali na sherehe ambapo watu humkodisha ili atoe burudani.
SOURCE: HabariLeo
Last edited: