Mastaa wetu waachane na biashara?

JAYJAY

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2008
Posts
8,191
Reaction score
8,490
Wadau nauliza hii kutokana na kuendelea kufa au kuzorota kwa miradi ya kibiashara ya wasanii wetu mastaa nje ya fani zao zilizowapa majina.

Biashara ya Lady Jaydee mgawaha wa Nyumbani Lounge , bar ya marehemu Ngwea ilikufa kabla ya yeye mwenyewe kufariki, duka la pamba la AY, Diamond na Ray C yote yalikufa kifo cha kawaida . Mo Faya ya King Kiba hii ilikufa kabla ya kuanza na mhanga mwingine ni Chibu Pefrume na Diamond Karanga nayo chali pia. Huku lotion ya Mwana Fa ikiwa inahemea pua moja.

Je, hawa jamaa wanakosea wapi?
 
Hao wasanii wanajua fika kuwa mashabiki zao wengi ni watu wa kipato cha chini au cha kati,wao wakija na product huwa wanaleta kwa bei ambazo watu wa chini hawawezi afford,mfano chibu perfume,na ile ya de la boss perfume,kingine wasanii hao wenye biashara wanaamini kupitia majina yao basi biashara itatoka,wanasahau biashara inataka nidhamu na usimamizi mkubwa kuipa promo bidhaa yako kupitia social media pekee haitoshi,sababu nyingine hizi biashara asilimia kubwa ni za watu wengine ila wasanii huwa wanakula shavu kupitia majina yao utakuta anaingia mkataba na mwenye mzigo baadaye anapoiona faida ni kubwa inapatikana na yeye anachukua asimilia chache ya kinachopatikana huwa wanahisi wanaibiwa wakati mkataba walisaini kwa akili zao kamili kinachofuata ni kuvunja mikataba(hi ndio kesi ya manara na perfume zake na boss wake).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wasafi.com hii nayo ni failure product. Aina ya msimamizi aliyepewa romi joni(sijui nimepatia) sidhani kama alikuwa na uwelewa jinsi digital business zinavyofanyika.

Unauza nyimbo wakati huo nyimbo hiyohiyo utaipata kwa djmwanga, bekaboy, na viblog vingine bure.

Ila diamond anafanya vizuri wasafi media na wcb label.

Mi naona wasanii wangekuwa wanafanya biashara wanafahamu nazo au wawe na timu ya watu sahihi ambao watagawana majukumu mfano wcb label ina mameneja watatu.

Au unakuwa na idara ya marketing ila kutegemea tu umaarufu pekeee ni ngumu bidhaa kufanya vizuri.
 
Tatizo kubwa la watu wengi tunaongea vitu ambavyo hatuvijui na tunajifanya tunajua tuje kwenye chibu perfume hii biashara japo ilikuwa ni Bei kubwa lakin iliuzika alipata suppliers wengi wa kununua hiyo perfume lakini Kuna wakati akatumia umaarufu wake kuuza mwenyewe pale GSM cos baadhi ya perfume alibaki nazo na alipata maelfu ya watu nenda YouTube utaona.Na yeye amethibitisha perfume zimeisha kwa alizouza lakini kuendelea au kutoendelea ni matakwa yake ni Kama vile nguo za WCB japo idadi ya wanunuzi ilikuwa kubwa lakini yenyewe hakuifanya iwe endelevu.Na sasa hiv mondi ana wasafi media na inakuja vizuri Sana

Tukija kwenye diamond karanga ilikuwa ni partnership between mondi na kampuni inatotengeneza hizo karanga na uliona namna gani jamaa alivyopromote na zikiwa zinauzika Sana na wakawa wamepata faida tatizo likatokea katika makubaliano yao ikapelekea kuvunjika ndo maana mondi akawa azipromote Tena na zikawa hazitengenezwi ndo maana sasa hiv huwezi kuzikuta mtaani Kama Mara ya kwanza.

Biashara pekee naona iliyofeli kwa mondi ni wasafidot.com ila hizo zingine zilifanikiwa lakini hakufanya ziwe na mwendelezo.wasafidot.com ilifeli cos watanzania wengi sio wazuri kwenye kununua ngoma Kama nchi zingine wao wanapenda kutumia bando kuwaajili ya kuview wimbo YouTube na kupiga kura kwenye matuzo pia nakufuatilia udaku.

Jux na shilole pia ni watu waliofanikiwa kwenye biashara sio Kama unavyosema eti wasanii wanafeli wapi.jux amefanikiwa kwenye kuuza nguo zake na shilole amefanikiwa kupitia mama ntilie amekuwa akipata wateja wengi kwenye mgahawa wake.

NB: sio wasanii wote waliofeli kwenye biashara Kuna baadhi wamefanikia na kuna wengine unakuta Kati ya biashara tatu alizofanya moja ndio umefeli.
 
FynByFalsafa nayo inahemea pua moja??? πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€.
 
Ni wasanii wachache sana duniani walioweza kufanikiwa kisanii na kibiashara. Asilimia kubwa ya wasanii hua wanafeli wakiingia kwenye biashara na mara nyingi ndio hua chanzo cha kufilisika kwao.
 
Mimi naona shida kubwa ina kuja kwenye swala la management..biashara ikiwa na usimamizi mbovu haiwezi kuendelea...

Wasanii wengi wamesha jiaminisha kuwa wao ndiyo kila kitu..kuna muda walitakiwa wa waajiri watu waendeleze biashara zao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
FynByFalsafa nayo inahemea pua moja??? πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€.

Mi niliijaribu. Sio mbaya sana wala sio kali sana. Ila kwa bei ya 6,000/= (Blue) me niliipenda.

Ila izo za kina Chibu Perfume bei kali sana me siwezi nunua.
 
Mi niliijaribu. Sio mbaya sana wala sio kali sana. Ila kwa bei ya 6,000/= (Blue) me niliipenda.

Ila izo za kina Chibu Perfume bei kali sana me siwezi nunua.
Chibu Bei yake Sokoni Tsh ngapi? FynByFalsafa kwa Buku 6 sio mbaya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…