Elections 2010 Maswali haya yanahitaji majibu ya Dr. Slaa na Chadema mapema iwezekanavyo

Elections 2010 Maswali haya yanahitaji majibu ya Dr. Slaa na Chadema mapema iwezekanavyo

Ntemi Kazwile

JF-Expert Member
Joined
May 14, 2010
Posts
2,182
Reaction score
308
Nimekuwa nikisikia minong'ono ya chini chini ambayo sasa imeanza kupazwa sauti na wagombea wa CCM kuwa ahadi za mgombea urais wa Chadema, Dr W Slaa, ni za uongo na hazitekelezeki. Kuna watu ambao ninawafahamu kuwa hawaipendi CCM lakini sasa wanaanza kuwa na mashaka na ahadi za Chadema kuwa kikingia madarakani kitatoa huduma za elimu na afya bure na pia kuwa kila kitu kitafanyiwa kazi ndani ya siku 100.

Ninashauri Chadema waanze kujibu haya maswali kwa kutoa vielelezo vya namna ambavyo wataweza kutoa elimu na afya bure, nawashauri watoe takwimu za idadi ya wanafunzi katika kila ngazi na gharama za kumsomesh mwanafunzi mmoja au kundi la wanafunzi 100 na waonyeshe ni namna gani watapata mapato ya kugharimia huduma hizi, kwa kusema tu jumla jumla kuwa kuna fedha inapotea kwenye misamaha ya kodi bila kutoa vielelezo watapoteza kura nyingi za watu ambao wangewapigia kama watapewa maelezo na vielelezo vinavyojitosheleza. Ikiwezekana waanze sasa kutupa hata mfano budget ya serikali yao kwa muhtasari.

Hii itawaziba midomo akina Kinana, Makamba, Kikwete na wengine kusema kuwa haya wanayoahidi Chadema na Slaa ni uongo. Pia itatoa fursa kwa watu makini kupima na kuona kuwa inawezekana watoto wao wakapata huduma bure na bora wakiwachagua Chadema. Nadhani kila mtu anataka kupata huduma bora na kwa gharama nafuu.

Kingine cha msingi ambacho nawashauri waanze kufanya ni kutoa maelezo ya namna ambavyo watatekeleza hayo wanayoyaahidi, nadhani hakuna Mtanzania leo hii ambaye hajui kuwa CCM ni genge la wahuni wasipoteze muda wao uliobaki kuelezea haya wajikite kwenye namna watakavyoshugulikia ikiwa ni pamoja na kutoa takwimu na vipeperushi. Naamini hii itawasaidia zaidi kuliko kupoteza muda wao kulipua makombora ya namna ambavyo Kikwete anaendesha nchi hii kama shirika la ukoo wao, tunajua na tunaelewa yote haya. Tunaomba tupatiwe majibu ya namna tutakavyotoka hapa
 
Mnhhhhh...mzee uloyasema yana-ka-ukweli fulani ndani yake hasa pale suala la kutekeleza ahadi ndani ya siku 100 mie pia siliafiki hilo....kuhusu elimu na afya bure ni kitu kilicho wazi kabsaaaa....tunatatizo moja kubwa serikali ya ccm "mambo ya msingi hayapewi kipaumbele"...wananunua ma prado-v8 ambayo running cost zake ni sawa na ada ya shule za wanafunzi nchi nzima.... Achilia mbali hizo posho na allowance za ajabuajabu za waheshimiwa...hata wabunge wenyewe wapo 310 kila mwezi wanatumia about 5mil ambazo ni sawa na 1.55b kwa mwaka ni sawa na tshs 18.6b...hii kiasi inatosha kusomesha wanachuo wetu 18,600 kwa mwaka kwa ada ya tshs 1m .... Mikataba ya madini na utozaji kodi wa ki-ndugu na kujuana inatosha kutoa tiba mahospitalini kwetu....yapo mengi naweza kumaliza siku nikiyajadili hapa....ni maoni tuu
 
Wameshindwa kujenga hata ofisi zao za chama tangu waanzishwe, wataweza hayao wanayo yadai kwa siku 100
 
Mnhhhhh...mzee uloyasema yana-ka-ukweli fulani ndani yake hasa pale suala la kutekeleza ahadi ndani ya siku 100 mie pia siliafiki hilo....kuhusu elimu na afya bure ni kitu kilicho wazi kabsaaaa....tunatatizo moja kubwa serikali ya ccm "mambo ya msingi hayapewi kipaumbele"...wananunua ma prado-v8 ambayo running cost zake ni sawa na ada ya shule za wanafunzi nchi nzima.... Achilia mbali hizo posho na allowance za ajabuajabu za waheshimiwa...hata wabunge wenyewe wapo 310 kila mwezi wanatumia about 5mil ambazo ni sawa na 1.55b kwa mwaka ni sawa na tshs 18.6b...hii kiasi inatosha kusomesha wanachuo wetu 18,600 kwa mwaka kwa ada ya tshs 1m .... Mikataba ya madini na utozaji kodi wa ki-ndugu na kujuana inatosha kutoa tiba mahospitalini kwetu....yapo mengi naweza kumaliza siku nikiyajadili hapa....ni maoni tuu

Usemavyo ni sawa ninachoshauri kuwa wajikite katika kuonyesha takwimu kama unazotoa kuonyesha kuwa wataweza kutoa huduma hizo kama wanavyoahidi na namna watakavyoyatekeleza hayo wanayoahidi ndani ya siku 100
 
mnhhhhh...mzee uloyasema yana-ka-ukweli fulani ndani yake hasa pale suala la kutekeleza ahadi ndani ya siku 100 mie pia siliafiki hilo....kuhusu elimu na afya bure ni kitu kilicho wazi kabsaaaa....tunatatizo moja kubwa serikali ya ccm "mambo ya msingi hayapewi kipaumbele"...wananunua ma prado-v8 ambayo running cost zake ni sawa na ada ya shule za wanafunzi nchi nzima.... Achilia mbali hizo posho na allowance za ajabuajabu za waheshimiwa...hata wabunge wenyewe wapo 310 kila mwezi wanatumia about 5mil ambazo ni sawa na 1.55b kwa mwaka ni sawa na tshs 18.6b...hii kiasi inatosha kusomesha wanachuo wetu 18,600 kwa mwaka kwa ada ya tshs 1m .... Mikataba ya madini na utozaji kodi wa ki-ndugu na kujuana inatosha kutoa tiba mahospitalini kwetu....yapo mengi naweza kumaliza siku nikiyajadili hapa....ni maoni tuu

kutekelza ahadi ndani ya siku 100 ni upotoshaji wa ccm na ni propaganda tupu. Stay confident, ni lazima nao ccm wajibu ndio maana wanapotosha what chedema is saying.
 
watatekeleza wakipata, ila wanajua hawapati sasa wao wanaahidi tu
 
wameshindwa kujenga hata ofisi zao za chama tangu waanzishwe, wataweza hayao wanayo yadai kwa siku 100

paulss-naomba unitajie ofisi ccm walizojenga wanachama wenyewe, hata huko vijijini ni wenyeviti wa serikali za mitaa na kata walitumika kufuja mapato ya serikali za vijiji na kata kufanikisha upatikanaji wa viwanja na ofisi za ccm. Kumbuka tulikuwa huko huko na tunajuana nje ndani
 
usemavyo ni sawa ninachoshauri kuwa wajikite katika kuonyesha takwimu kama unazotoa kuonyesha kuwa wataweza kutoa huduma hizo kama wanavyoahidi na namna watakavyoyatekeleza hayo wanayoahidi ndani ya siku 100
ntemi kazwile-tatizo la watanzania hatutaki kujielimisha na ccm wanafahamu hilo sana kwa kuwa wao ndio walitunga mitaala ya elimu isiyowafundisha watu kuwa critical thinkers. Je ume[ata muda wa kusoma ilani ya uchaguzi ya chadema au umatumia propaganda za ccm za siku 100. Siku 100 ni kuhakikisha wote wenye tuhuma za ufisadi wako mahakamani. Ndio maana ccm wanaziogopa na kupotosha.

Nakushauri tafuta ilani ya chadema utagundua tofauti. Watanzani tusitake kufanyiwa kila ktu, tujiulize sisi tumeifanyia nini tanzania. Sasa kama hatuwezi hata kutafuta ilani za vyama vya siasa na kuzisoma. Tuwaruhusu hao mafisadi waendele kutawala.
 
ntemi kazwile-tatizo la watanzania hatutaki kujielimisha na ccm wanafahamu hilo sana kwa kuwa wao ndio walitunga mitaala ya elimu isiyowafundisha watu kuwa critical thinkers. Je ume[ata muda wa kusoma ilani ya uchaguzi ya chadema au umatumia propaganda za ccm za siku 100. Siku 100 ni kuhakikisha wote wenye tuhuma za ufisadi wako mahakamani. Ndio maana ccm wanaziogopa na kupotosha.

Nakushauri tafuta ilani ya chadema utagundua tofauti. Watanzani tusitake kufanyiwa kila ktu, tujiulize sisi tumeifanyia nini tanzania. Sasa kama hatuwezi hata kutafuta ilani za vyama vya siasa na kuzisoma. Tuwaruhusu hao mafisadi waendele kutawala.

Ahsante mkuu, nimekuwa nikitaka kuisoma lakini sijabahatika kuipata. Nakaa Kibamba kwa yeyo anayejua pa kuzipata mitaa hiyo anisaidie tafadhali, hata kama itanibidi nilipie
 
Wameshindwa kujenga hata ofisi zao za chama tangu waanzishwe, wataweza hayao wanayo yadai kwa siku 100

Mkuu paulss usipoikuwa macho utashitakiwa sasa hivi kwa kunakili isivyohalali maandiko ya watu. Tafadhali andika hapa kuwa sentensi hii sio ya kwako bali ya Nape Mnauye aliyoitoa jana...

Lakini unanifurshisha kuwa unatoa picha ya wana CCM wengine COPY AND PASTE...

Angalia jinsi JK anavyotekeleza maagizo ya Slaa
 
Nimekuwa nikisikia minong'ono ya chini chini ambayo sasa imeanza kupazwa sauti na wagombea wa CCM kuwa ahadi za mgombea urais wa Chadema, Dr W Slaa, ni za uongo na hazitekelezeki. Kuna watu ambao ninawafahamu kuwa hawaipendi CCM lakini sasa wanaanza kuwa na mashaka na ahadi za Chadema kuwa kikingia madarakani kitatoa huduma za elimu na afya bure na pia kuwa kila kitu kitafanyiwa kazi ndani ya siku 100.

Ninashauri Chadema waanze kujibu haya maswali kwa kutoa vielelezo vya namna ambavyo wataweza kutoa elimu na afya bure, nawashauri watoe takwimu za idadi ya wanafunzi katika kila ngazi na gharama za kumsomesh mwanafunzi mmoja au kundi la wanafunzi 100 na waonyeshe ni namna gani watapata mapato ya kugharimia huduma hizi, kwa kusema tu jumla jumla kuwa kuna fedha inapotea kwenye misamaha ya kodi bila kutoa vielelezo watapoteza kura nyingi za watu ambao wangewapigia kama watapewa maelezo na vielelezo vinavyojitosheleza. Ikiwezekana waanze sasa kutupa hata mfano budget ya serikali yao kwa muhtasari.

Hii itawaziba midomo akina Kinana, Makamba, Kikwete na wengine kusema kuwa haya wanayoahidi Chadema na Slaa ni uongo. Pia itatoa fursa kwa watu makini kupima na kuona kuwa inawezekana watoto wao wakapata huduma bure na bora wakiwachagua Chadema. Nadhani kila mtu anataka kupata huduma bora na kwa gharama nafuu.

Kingine cha msingi ambacho nawashauri waanze kufanya ni kutoa maelezo ya namna ambavyo watatekeleza hayo wanayoyaahidi, nadhani hakuna Mtanzania leo hii ambaye hajui kuwa CCM ni genge la wahuni wasipoteze muda wao uliobaki kuelezea haya wajikite kwenye namna watakavyoshugulikia ikiwa ni pamoja na kutoa takwimu na vipeperushi. Naamini hii itawasaidia zaidi kuliko kupoteza muda wao kulipua makombora ya namna ambavyo Kikwete anaendesha nchi hii kama shirika la ukoo wao, tunajua na tunaelewa yote haya. Tunaomba tupatiwe majibu ya namna tutakavyotoka hapa
Kuna jambo moja muhimu ambalo tunatakiwa tuelewe,CCM wanayosema yote wameyafanya si kwamba wametoa pesa zao mifukoni bali ni kodi za wananchi ambazo wanasiasa hawa hawa tunaowaona wa maana wanapita na kutuambia wamefanya hiki na kile.Cha msingi ni kuangalia pia nini ambacho serikali yetu imekifanya kwa miaka yote hiyo iliyokuwa madarakani kupitia CCM kulinganisha na rasilimali tulizonazo watanzania na baada ya hapo tujiulize je yafaa kuitoa miaka mitano kwa CHADEMA na ahadi inazotoa?Je wataweza kutekeleza yote wanayoyasema?Mana hata ahadi tunazopewa na chama kinachotawala nyingine mpaka leo hazitatekelezwa tena kwa miaka nenda rudi na bado zinakuja nyingine nyingi tu.
Tusiwe waoga wa changamoto za kimaisha hasa katika suala la mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi.
 
Huwezi kutoa ahadi za kisiasa bila kujiwekea muda maalumu uambao utasaidia kukupa dira kama kiongozi kuweza kuyafikia yale ya papo kwa papo,muda wa kati na ya muda mrefu,mwanakijiji alituwekea hapa Ilani ya chadema nawameonyesha kila kitu na sababu zitakazowafanya wao wafanikiwe ,kwenye mikutano ya saa moja hawawezi kunyambulisha kila kitu ilikuwa sisi wananchi tutafute hizo ilani na waandishi wetu wengine wamejitahidi kuweka ilani zote kwenye magazeti yao kama Mwananchi na Raia Mwema
 
Ahsante mkuu, nimekuwa nikitaka kuisoma lakini sijabahatika kuipata. Nakaa Kibamba kwa yeyo anayejua pa kuzipata mitaa hiyo anisaidie tafadhali, hata kama itanibidi nilipie

Kila wiki gazeti la Raia Mwema wanatoa Ilani za CCM, CUF na CHADEMA! Mimi nazisomea humo!
 
paulss-naomba unitajie ofisi ccm walizojenga wanachama wenyewe, hata huko vijijini ni wenyeviti wa serikali za mitaa na kata walitumika kufuja mapato ya serikali za vijiji na kata kufanikisha upatikanaji wa viwanja na ofisi za ccm. Kumbuka tulikuwa huko huko na tunajuana nje ndani


Mkuu ndio matatizo yenu kila mkibanwa mnajilinganisha na CCM,
Ofisi nyingi za CCM zilijengwa wakati wa chama kimoja sawa, hilo halina ubishi lakini ndio kigezo cha wewe kutokujenga zako?
 
Hilo la siku 100 naona wengi hawajalielewa au kwa makusudi wanataka kupotosha kwa faida yao. Anachokisema Dr. Slaa (na pia imeelezwa kwenye ilani ya uchaguzi ya kitaifa ya Chadema) ni kwamba ndani ya siku 100 za kwanza za urais (kama akipewa ridhaa) wataanza mchakato wa marekebisho ya katiba (hasa kwenye mfumo wa utawala). Hii itafungua milango mingi sana kwa fursa zilizopo, hili la elimu linawezekana pia, wanachosema chadema ni kwamba ndani ya siku 100 wataanza kutekeleza mkakati utakaowawezesha watoto wote wa kitanzania kupata elimu bure (kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha sita). hii haina maana kwamba mfumo uliopo sasa kwa shule za binafsi utabadilika, shule zinazolengwa hapa ni zile zilizo chini ya uendeshaji wa serikali. structure haitabadilika ila mfumo wa uendeshaji ndio utakaobadilika kwa kuwekeza zaidi katika elimu. Fedha inayolengwa zaidi ni ile ya posho za maofisa wa serikali na mianya mingine ya kifisadi. Kenya wamefanya hili na kwa kiasi kikubwa wamefanikiwa. wanasiasa wa sisiemu kwa makusudi wanalipotosha hili kwa faida yao ya kisiasa
 


Mkuu ndio matatizo yenu kila mkibanwa mnajilinganisha na CCM,
Ofisi nyingi za CCM zilijengwa wakati wa chama kimoja sawa, hilo halina ubishi lakini ndio kigezo cha wewe kutokujenga zako?

Haujajibu swali, je ccm ndio wanaofaa? Wamefilisi SUKITA, wameshindwa kuendeleza vitega uchumi vyote vilivyojengwa na Nyerere na badala yake wanajinufaisha wachache. Kwa mwezi CCM inalipwa mabilioni ya pesa za walipa kodi, je zinatumika je?

Chadema ni chama kichanga na sioni kuwa ni tatizo kwa wao kutokuwa na ofisi.
 
Mkuu paulss usipoikuwa macho utashitakiwa sasa hivi kwa kunakili isivyohalali maandiko ya watu. Tafadhali andika hapa kuwa sentensi hii sio ya kwako bali ya Nape Mnauye aliyoitoa jana...

Lakini unanifurshisha kuwa unatoa picha ya wana CCM wengine COPY AND PASTE...

Angalia jinsi JK anavyotekeleza maagizo ya Slaa



Mkuu hiyo kauli unakuuma sana nini? nikibwagizo tu hicho
je huoni utumbo wenu mnao copy na kupest toka kwa padri wenu slaa mnavyo jaza humu jf
 
Nakushauri tafuta ilani ya chadema utagundua tofauti. Watanzani tusitake kufanyiwa kila ktu, tujiulize sisi tumeifanyia nini tanzania. Sasa kama hatuwezi hata kutafuta ilani za vyama vya siasa na kuzisoma. Tuwaruhusu hao mafisadi waendele kutawala.
haya ndio maneno Jatropha, watu watafute ilani ya Chadema ndio waanze kuongea na kuuliza maswali.
 
Dr Slaa alisema kila kiu ya jibu kwa wananchi mdahalo kwake yeye na JK
JK anaogopa akiadhirishwa live kwani anajua kabisa mdahalo utakua live kwenye TV na maredio ambazo wananchi wengi wangejua wapi mchele na wapi pumba.
 
Haujajibu swali, je ccm ndio wanaofaa? Wamefilisi SUKITA, wameshindwa kuendeleza vitega uchumi vyote vilivyojengwa na Nyerere na badala yake wanajinufaisha wachache. Kwa mwezi CCM inalipwa mabilioni ya pesa za walipa kodi, je zinatumika je?

Chadema ni chama kichanga na sioni kuwa ni tatizo kwa wao kutokuwa na ofisi.


Kama bado wachanga kaeni pempeni subirini siku mkikomaa ndio tutawapa nchi
uongozi sio swala la majaribio ndugu hatuwezi kuwaamini watu wanao shindwa hata kujenga ofisi za kisha tukatumaini kujenga nchi yetu
 
Back
Top Bottom