Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 308
Nimekuwa nikisikia minong'ono ya chini chini ambayo sasa imeanza kupazwa sauti na wagombea wa CCM kuwa ahadi za mgombea urais wa Chadema, Dr W Slaa, ni za uongo na hazitekelezeki. Kuna watu ambao ninawafahamu kuwa hawaipendi CCM lakini sasa wanaanza kuwa na mashaka na ahadi za Chadema kuwa kikingia madarakani kitatoa huduma za elimu na afya bure na pia kuwa kila kitu kitafanyiwa kazi ndani ya siku 100.
Ninashauri Chadema waanze kujibu haya maswali kwa kutoa vielelezo vya namna ambavyo wataweza kutoa elimu na afya bure, nawashauri watoe takwimu za idadi ya wanafunzi katika kila ngazi na gharama za kumsomesh mwanafunzi mmoja au kundi la wanafunzi 100 na waonyeshe ni namna gani watapata mapato ya kugharimia huduma hizi, kwa kusema tu jumla jumla kuwa kuna fedha inapotea kwenye misamaha ya kodi bila kutoa vielelezo watapoteza kura nyingi za watu ambao wangewapigia kama watapewa maelezo na vielelezo vinavyojitosheleza. Ikiwezekana waanze sasa kutupa hata mfano budget ya serikali yao kwa muhtasari.
Hii itawaziba midomo akina Kinana, Makamba, Kikwete na wengine kusema kuwa haya wanayoahidi Chadema na Slaa ni uongo. Pia itatoa fursa kwa watu makini kupima na kuona kuwa inawezekana watoto wao wakapata huduma bure na bora wakiwachagua Chadema. Nadhani kila mtu anataka kupata huduma bora na kwa gharama nafuu.
Kingine cha msingi ambacho nawashauri waanze kufanya ni kutoa maelezo ya namna ambavyo watatekeleza hayo wanayoyaahidi, nadhani hakuna Mtanzania leo hii ambaye hajui kuwa CCM ni genge la wahuni wasipoteze muda wao uliobaki kuelezea haya wajikite kwenye namna watakavyoshugulikia ikiwa ni pamoja na kutoa takwimu na vipeperushi. Naamini hii itawasaidia zaidi kuliko kupoteza muda wao kulipua makombora ya namna ambavyo Kikwete anaendesha nchi hii kama shirika la ukoo wao, tunajua na tunaelewa yote haya. Tunaomba tupatiwe majibu ya namna tutakavyotoka hapa
Ninashauri Chadema waanze kujibu haya maswali kwa kutoa vielelezo vya namna ambavyo wataweza kutoa elimu na afya bure, nawashauri watoe takwimu za idadi ya wanafunzi katika kila ngazi na gharama za kumsomesh mwanafunzi mmoja au kundi la wanafunzi 100 na waonyeshe ni namna gani watapata mapato ya kugharimia huduma hizi, kwa kusema tu jumla jumla kuwa kuna fedha inapotea kwenye misamaha ya kodi bila kutoa vielelezo watapoteza kura nyingi za watu ambao wangewapigia kama watapewa maelezo na vielelezo vinavyojitosheleza. Ikiwezekana waanze sasa kutupa hata mfano budget ya serikali yao kwa muhtasari.
Hii itawaziba midomo akina Kinana, Makamba, Kikwete na wengine kusema kuwa haya wanayoahidi Chadema na Slaa ni uongo. Pia itatoa fursa kwa watu makini kupima na kuona kuwa inawezekana watoto wao wakapata huduma bure na bora wakiwachagua Chadema. Nadhani kila mtu anataka kupata huduma bora na kwa gharama nafuu.
Kingine cha msingi ambacho nawashauri waanze kufanya ni kutoa maelezo ya namna ambavyo watatekeleza hayo wanayoyaahidi, nadhani hakuna Mtanzania leo hii ambaye hajui kuwa CCM ni genge la wahuni wasipoteze muda wao uliobaki kuelezea haya wajikite kwenye namna watakavyoshugulikia ikiwa ni pamoja na kutoa takwimu na vipeperushi. Naamini hii itawasaidia zaidi kuliko kupoteza muda wao kulipua makombora ya namna ambavyo Kikwete anaendesha nchi hii kama shirika la ukoo wao, tunajua na tunaelewa yote haya. Tunaomba tupatiwe majibu ya namna tutakavyotoka hapa