Hivi ni vigezo gani zaidi ya maswali Sekretarieti wanaangalia katika kumpa mtu maksi ndani ya usaili?
kipi ni kiwango cha kufaulu ndani ya sekretariti na ni kwa alama ngapi? ukiachana na alama za ushindani?
kama umeitwa na sekretariti ya ajira sehemu mbili na ukafanya zote na ukafaulu je sekretariti ya ajira hufanyaje?
Na inakuwaje inafika kipindi wanawaita watu kwenye usaili watu watatu nafasi moja halafu hawawachukui wote na baadaye wanatangaza upya? nini sababu zinazosababisha hili kutokea ?
usihofu vyanzo vya taarifa!, hizi ni taarifa sahihi.Nakushukuru sana GP kwa majibu yako, lakini majibu haya yanapatikana wapi GP, au vyanzo vyako vya information ni wapi? Kama ni 50% Basi nitachomoa . Nakushukuru sana kwa majibu yako ya kina .
usihofu vyanzo vya taarifa!, hizi ni taarifa sahihi.
na labda nikueleze kitu kingine muhimu, pass mark ni 50%, lakini inaweza ikatokea watu wamefaulu sana kwa kufungana, hapo pass mark hua inapanda!. na ratio ya kuchuja watu ni 1 kwa tatu. namaanisha kwa mfano nafasi ya kazi ni 4, then wakaaply watu 70, hapo mtaitwa wote 70 kufanya mtihani, lakini watachuja kupata watu 12 tu ili mkafanye oral interview. so wataangalia watu 12 wenye alama nyingi lakini wasivuke 50%.
kuna kuchuja watu kwa aina tofauti, mfano wale wote watakaoenda bila vyeti halisi by default watakua wameondolewa!.
Ukipata sehemu mbili kwenye usahili wa awamu moja tuseme wa mwezi september, wanakupeleka sehemu uliyofaulu ya kwanza! kwa mfano tarehe 5 na 6 ufanye usail pale Hombolo na ufaulu then tarehe 10 na 11 ufanye usahili wa state attorney na ufaulu vile vile na tarehe 23 na 24 ufanye usahili TIA nako ufaulu pia. basi wanakuchagulia hombolo mana ndo ulipata pa kwanza! wanafanya hivyo kupunguza double allocation na kusaidia wale ambao hawana kazi wapate nao mana wewe unakuwa umeshapata! Nina ushahid wa ili nilisemalo!