Jamal Malinzi
JF-Expert Member
- Feb 9, 2013
- 710
- 650
- Thread starter
-
- #401
CHUAKACHARA kikao cha kamati ya rufaa ya uchaguzi kinaendelea,maamuzi hayajatolewa mpaka sasa.Kuna uzi humu kuwa Wambura ameshinda. This is great! Haki imetendeka. Sishabikii Wambura, ila ujinga wa mashabiki wa Simba na Yanga ukomeshwe!
Magehema kwa swali lako sina shaka wewe ni mtaalam wa mpira wa awali (grassroot),grassroot ni mpira unaochezwa katika umri wa miaka 6-12.Katika ngazi hii msisitizo ni kumfanya mtoto ajenge mapenzi ya kucheza mpira,hapa ushindi hautiliwi mkazo. Katika ngazi hii watoto wanatakiwa wachezee mipira midogo (size 3/4,mipira ya wakubwa ni size 5).Mipira hii inatakiwa ipatikane kwa wingi na kwa bei nafuu,tatizo kodi inasababisha bei yake iwe kubwa.Tanzania tuna shule za msingi yapata 19,600,unapozungumzia makocha wa grassroot unazungumzia kila shule ya msingi iwe na Mwalimu kocha aliyesomea na kupata leseni ya kufundisha grassroot football,ni jukumu la wamiliki wa shule hizi ambao ni ofisi ya Waziri Mkuu kupitia TAMISEMI kuhakikisha walimu hawa wanapatikana,TFF iko tayari kutoa ushirikiano wa kiufundi katika hili.Vyuo vya michezo kama Malya na Murutunguru na hata idara ya michezo ya UDSM vinatakiwa viweke umuhimu wa kipekee kwa kushirikiana na TFF kuhakikisha hizi kozi zinatolewa. Sasa hivi TFF inaandaa mpango wa miaka kumi wa maendeleo ya mpira wa vijana,yote haya yatafafanuliwa kwenye program hii na bajeti yake itaelezwa.Wadau wote tukiongozwa na Serikali,TFF,mashirika ya umma/binafsi,NGO,Media,watu binafsi itabidi tushirikiane kutekeleza mpango huu.Bila program makini ya maendeleo ya mpira wa vijana tutabakia kuota kushiriki fainali za kombe la dunia.Wenzetu afrika magharibi na kaskazini walithubutu wameweza (nchini Misri youth development programme yao ilianza mwaka 1957!).Mheshimiwa Rais, swali langu ni soka la watoto wadogo, kumekuwa na upungufu mkubwa wa makocha wenye sifa za kufundisha watoto wadogo U14 pamoja na vifaa hasa mipira ya size ya watoto matokeo yake watoto wanatumia mipira mikubwa jambo ambalo kitaalamu halimjengei msingi mzuri. TFF ina mpango gani kwa kushirikiana na wadau kwanza kuagiza vifaa hivyo, na pili kutoa mafunzo kwa makocha wa kufundisha watoto?
Heshima kwako Mkuu..umenijibu Vizuri sana..yaani nimeelewa...Tuombe mungu tupewe UENYEJI huo..Fainali za afrika za vijana finalists ni timu nane tu,hivyo unahitaji viwanja viwili vizuri tu na viwanja vinane vya mazoezi,vyote hivyo tunavyo.
msaada wa FIFA inategemea member association inaomba nini ila limit ni dola laki tano,ndio maana huko nyuma FIFA walitujengea hostel karume.
Swali langu ndugu Malinzi kwanini TFF iliamua kubadili muonekano wa jezi ya timu ya taifa? Lakini pia Heri rangi ingekuwa nzuri, mmechagua rangi nyeusi isiyo hata na mvuto, mlipata ushauri wa kitaalamu kweli? Na je serikali ilishirikishwa? Maana tunaona rangi ya juu ukiacha nyeusi sio rangi ya bebdera ya taifa letu.
Ushauri: ni bora mngeweka blue yenye michirizi ya njano, hapo tungekubali wadau wa soka. Rangi hii nyeusi si njema kwa mafanikio ya soka na haina mvuto.
Pia, ndugu Malinzi uongozi mpya unapoingia madarakani si lazima ubadili kila kitu, ulifanya hivyo kwenye secretariat, kamati za TFF etc, sasa hata jezi kweli?
Heshima kwako Mkuu..umenijibu Vizuri sana..yaani nimeelewa...Tuombe mungu tupewe UENYEJI huo..
ahsante
Wewe pia umelishwa sumu na waandishi waliohongwa na hao FoS, Malinzi anampenyeza vipi huyo mnayemuhita kipenzi chake acha kubeba maneno ya waandishi walionunuliwa na kuyaleta hapa, hapa tunataka facts.
Majuzi Hollyman alifungua thread ya aina hii.Nia na lengo lake lilikuwa ni zuri,namshukuru.Nimeamua nifungue mwenyewe hii thread ili iwe ni uwanja wa kudumu wa kuniuliza maswali,kutaka ufafanuzi na pia kutoa ushauri kuhusu maendeleo ya mpira wetu.Kwa ruhusa ya moderators ninaomba uwe ni ukurasa wa kudumu hapa jf.
Jamal Malinzi
Rais wa TFF
Dar es salaam 04/Feb/2014
Ndugu Jamal, usiyumbe simamia lile unaloliamini. Ulisema utasimamisha uchaguzi Simba mpaka waunde kamati ya maadili. That was a credit to you maana ulikuwa unasimamia sheria. Umeyumba/umeyu,mbishwa na kubadili lililo la kweli. Nadhani waliokwenda mahakamani watashinda maana kamati ya maadili haipo Simba, katiba imevunjwa. Let us wait and see what the Judge will decide!
Jamal Malinzi ni member JF.Njoo utueleze kwa nini hukusimamia maamuzi yako ya awali.Pia kwa nini ulihamisha ofisi za TFF Karume hadi katikati ya jiji? Umefanya maamuzi mengi yasiyo na maana,lakini kwa gharama kubwa.
sikuona mantiki ya Raisi wa TFF kubadilisha maamuzi yale muhimu, sasa hili swala watu wameenda mahakamani kudai haki zao maana chombo kilichoundwa kuhakikisha haki zinapatikana eti wanatumia busara, busara ambayo inavunja katiba! busara inapotumika basi katiba izingatiwe na kuheshimiwa! Busara inapotumika kuvunja katiba na vipengere hiyo inakuwa si busara tenaNdio maana nasema ameyumba. Simamia lile unaloliamini ni sahihi na baada ya kufanya utafiti wa kutosha. He is a public figure with all eyes on him!
Malinzi,
Tunaomba utume hesabu za gharama zilizotumika kuweka watu Lushoto, na Zanzibar kujadili kuboresha timu ya Taifa. Pia naomba gharama zilizotumika katika zoezi la kwenda kutafuta wachezaji mikoani, pamoja na kuwaweka kambini Tukuyu. Nadhani hizo hazitakiwi kuwa ni siri, hamna chochote cha kufanya kuwa ni siri. Na ikiwezekana tupe mchanganuo wa majina ya walioshiriki, na kulipwa pesa.