Maswali na ushauri kwa Malinzi

Ni kweli ligi inabidi iboreshwe ushindani uongezeke,tatizo timu nyingi hazina vyanzo vya mapato kuweza kupambana,tatizo hili sio la kwetu ni la nchi nyingi duniani na matokeo yake mabingwa wanakuwa ni wale wale miaka nenda rudi.
 

Mpaka leo hoja yangu katika post #76 ya thread hii hujaijibu hata kwa PM. Wewe ni kiongozi wa umma na sitaki kutafsiri kuwa hii nidharau!
 

Mpaka leo hoja yangu katika post #76 ya thread hii hujaijibu hata kwa PM. Wewe ni kiongozi wa umma na sitaki kutafsiri kuwa hii nidharau!
Jibu la hiyo hoja ,ambayo you keep on repeating,litausaidia nini mpira wa nchi yetu.......au una lako jambo mkuu? Liseme tu,maana hapa mimi ninajulikana kwa jina na sura,mwenzangu upo chini ya mwavuli wa avatar na pseudoname.
 
Habari Mr PRESIDENT MALINZI

Ok mr president kuna suala hili la mchezaji MWASAPILI wa MBEYA city kushindwa kusafiri na timu ya taifa kwenda Namibia kwa mechi ya kirafiki sababu ikiwa zinahusu HATI YA KUSAFIRIA {PASIPOTI}.

Mkuu kabla hujajibu swali langu niseme kitu kimoja tuweke sawa..Yes ndio tunajua kuwa suala la mtu kuwa HATI ya kusafiri PASIPOTI ni la wajibu binafsi ndio, Lakini turudi kwenye hili ndio mchezaji kaitwa timu ya taifa na nazani au nina uhakika baada ya kuitwa maandalizi ya safari yalianza kufanywa ikiwemo kuu kabisa la kushughulikia masuala ya viza na mengine ya safari, moja ikiweo kila mchezaji kutoa pasipoti yake au kukabidhi taarifa za pasipoti yake kwa ajili ya kushughulikia safari, Hivi ina maana baada ya kugundua kuwa kuna mchezaji mmoja hana hati ya kusafiria na anahitajika kusafiri na timu hakuna hatua zozote za haraka na dharura zilizochukuliwa na tff kuhakikisha mchezaji huyo anapata HATI kwa haraka ili aweze kusafiri na timu? nini kazi ya kamati au watu wanahusika na timu ya taifa ikiwemo kuandaa safari na kuhakikisha kila mchezaji anakuwa na vitu muhimu vinavyohitajika kwa safari? Sizungumzii TFF kumlipia gharama za kupata hati La ,ila kwakuwa mchezaji wa timu ya taifa ni sawa mtumishi yoyote wa serikali kwani anawakilisha nchi na umma TFF imeshindwaje kushughulikia kwa haraka suala ili kupata pasi? Kupata hati kwa haraka inawezekana kabisa ndani ya siku 2 endapo muombaji atatoa sababu za msingi na vielelezo vya kutosha na sahihi vya kutaka apatiwe kwa uharaka zaidi, mchezaji asingeweza yeye kama yeye kwenda uhamiaji na kusema anataka kwa dharura kwa ajili ya kusafiti na timu ya taifa bila uthibitisho wa tff na TFF walitakiwa kusimama kwenye hili.. Kwa hii kweli sidhani kama TFF wanaweza kwa namna yoyote kukwepa lawama? Je wahusika au kamati inayohusika na timu ya taifa kwa mambo ya safari na mengineyo kama hili tu wameshinndwa je kazi yao ni nini hasa?

K wa mujibu wa kocha msaidizi inasemekana walimpigia simu mmoja wa watu wa tff wahusika kuhusu kwamba wameshatuma risit aliyolipia hati akiwa mbeye ili afanye haraka kwa dar es salaam apate hati nasikia huyo mu wa tff akawajibu kuwa hana muda na yupo bize na kuangalia mechi ya TWIGA STARZ...

MKUU TUNAOMBA MAJIBU KWA HILI TAFADHARI ....





 
Jibu la hiyo hoja ,ambayo you keep on repeating,litausaidia nini mpira wa nchi yetu.......au una lako jambo mkuu? Liseme tu,maana hapa mimi ninajulikana kwa jina na sura,mwenzangu upo chini ya mwavuli wa avatar na pseudoname.

Sasa mbona wakasirika yakhe? Nijibu tu hoja yangu.......kama jibu langu halisaidii kitu kwenye mpira wetu basi ile safari uliifanya ya nini? Mimi sina jambo lolote na wewe bali huyu uliyemfuata! Na kwa majibu yako haya utakuwa mtu wa madharau sana!




 

Mkuu Malinzi wewe mjibu tu huyo safari kwani mimi sioni tatizo la Mh waziri mkuu mstaafu kukutana na wewe, na pia yeye ni mtanzania anayo kila haki ya kujadili na pia ata kuchangia maendeleo ya mpira wa Tanzania,yeye pia ni mdau.

Swali,Mh Tenga alikuachia/kukabidhi acc yenye T sh mil 720(720,000,000) sasa inakuaje TFF hakuna pesa za kumlipa paulsen?
 
Sawa mh.kwa kunijibu.Naomba kuuliza kwamba kocha wa taifa stars analipwa na serikali au na TFF kama ilivyokuwa kwa Maximo?
 
Sawa mh.kwa kunijibu.Naomba kuuliza kwamba kocha wa taifa stars analipwa na serikali au na TFF kama ilivyokuwa kwa Maximo?
Mwalimu wa timu ya Taifa analipwa na serikali,kwa hili tunamshukuru Rais Kikwete kwa initiative hii,inatusaidia sana.
 
Mmmmmhhhh ........ Kuhusu pesa un a uhakika asilimia

100% na hili ulilolisema au unajaribu kukaanga mbuyu kina malinzi tule?
 
Ndugu yangu kama ulivyosema anayetoa hati ni idara ya uhamiaji na sio malinzi,usitake kunichonganisha na serikali,huyu kijana bado ana nafasi tena nzuri tu ya kulitumikia taifa lake kupitia timu ya Taifa,asikate tamaa.
 
Mkuu mbona umejibu kwa kupanik as if hauko katika mud nzuri.

Kwani kuuliza swali ni kuchonganisha? Kivi tunataka kukuchonganisha na serikali,

Nilitegemea angalau ungetujulisha umma wa wapenda soka wa Tanzania ilikuaje au nini kilikuwa mpaka mchezaji akashindwa kupata HATI kwa haraka kuwahi mechi,

Mr president majibu mepesi sana unatupatia, Nilitegemea angalau ungetumia nafasi hii kuufanya umma uelewe ili kuondoa yanayosemwa ambayo si mazuri kwa upande wa tff na lawama zinazoelekezwa kwa tff


Ndugu yangu kama ulivyosema anayetoa hati ni idara ya uhamiaji na sio malinzi,usitake kunichonganisha na serikali,huyu kijana bado ana nafasi tena nzuri tu ya kulitumikia taifa lake kupitia timu ya Taifa,asikate tamaa.
 
 
 
Last edited by a moderator:
 


Mmmmmhhhh ........ Kuhusu pesa un a uhakika asilimia

100% na hili ulilolisema au unajaribu kukaanga mbuyu kina malinzi tule?

Mkuu ulikabithiwa TFF ikiwa na mkataba wa kuigharamia timu ya Taifa,pia mkataba wa vodacom pesa za kuendesha ofisi.pia na account yenye fedha,Tenga alisema"baada ya wiki mbili TBL watakuwa wameshaingiza fedha kwa ajili ya timu ya taifa kwenye account za TFF"na makataba wa TBL ni wa mabilioni,sasa labda TBL wameacha kuigharamia timu ya taifa mkuu litolee ufafanuzi pls
 
Una uhakika na haya unayoyasema? I wish ungejua gharama halisi za kuendesha Federation na kipato chake.Sipendi kuzungumzia details za wadhamini wetu,hapa sio mahali pake. suffice to say we are trying to do our best under the circumstances.I am not going to say any more.
 
Mh.pole na majukumu.TFF hivi karibuni imehama ofisi toka eneo la karume kwenda kupanga mjini kwenye jengo la kifahari kwa ijili eti ya kupisha uanzishaji wa miradi mbalimbali ya TFF.Mh.huoni kwamba ingekuwa ni vyema kubaki palepale huku hiyo miradi ikiendelea ili kuepuka gharama zisizo za msingi kwa TFF?ikizingatia hivi karibuni ulinukuliwa ukisema TFF ya sasa imeyakuta madeni mengi.Kazi njema mh.
 
Malinzi nimegundua huna jipya lolote...ni siasa tu zile zile za kina Rage..Tenga was the perfect man for our football
 

Nilisoma katika mtandao wa mawakala kuwa wakala asiyetambuliwa anaweza kufanya mazungumzo kwa niaba ya mchezaji, lakini atahitaji usimamizi wa wakala anayetambulika na shirikisho au mwanasheria wakati wa kutia sahihi mikataba. Kuna ukweli hapa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…