Maswali ya waandishi wa habari kwa makocha wa kigeni

Maswali ya waandishi wa habari kwa makocha wa kigeni

Seth seth

Senior Member
Joined
Jan 2, 2022
Posts
106
Reaction score
150
Salaam team. Maswali wanayouliza waandishi wa habari baada ya mechi kwa makocha wa kigeni hiyo ndiyo taswira halisi ya Elimu yetu hapa Tanzania. Kwanza utakuta mwandishi wa habari anauliza swali kwa kiingereza ambacho ni "broken " , pili utakuta swali linaloulizwa ni "irrelevant", tatu mwandishi anauliza swali ambalo wenzake wameshauliza na limeshapatiwa majibu. Hii ndiyo taswira halisi ya Elimu yetu ya kibongobongo. Imagine waandishi wamemaliza vidato vyote wakaenda vyuo mbalimbali diploma Hadi degree, wamefanyiwa usaili kabla ya kuajiriwa, wanasililizwa na maelf ya watu mbalimbali kila siku lakini bado wanaliaibisha taifa kwa kuuliza maswali ya siyo na maana mbele ya makocha wa kigeni. Unategemea Hali ipoje kwenye fani nyingine ambazo hatupati wasaa wa kuwaona na kuwasikia? Kiufupi Hali ni mbaya na ndiyo maana ni ngumu kwa wasomi wa kizazi Cha Sasa kushindana na wasomi wa nchi za jirani katika soko la ajira kwa sababu Kama hizo.
 
Salaam team. Maswali wanayouliza waandishi wa habari baada ya mechi kwa makocha wa kigeni hiyo ndiyo taswira halisi ya Elimu yetu hapa Tanzania. Kwanza utakuta mwandishi wa habari anauliza swali kwa kiingereza ambacho ni "broken " , pili utakuta swali linaloulizwa ni "irrelevant", tatu mwandishi anauliza swali ambalo wenzake wameshauliza na limeshapatiwa majibu. Hii ndiyo taswira halisi ya Elimu yetu ya kibongobongo. Imagine waandishi wamemaliza vidato vyote wakaenda vyuo mbalimbali diploma Hadi degree, wamefanyiwa usaili kabla ya kuajiriwa, wanasililizwa na maelf ya watu mbalimbali kila siku lakini bado wanaliaibisha taifa kwa kuuliza maswali ya siyo na maana mbele ya makocha wa kigeni. Unategemea Hali ipoje kwenye fani nyingine ambazo hatupati wasaa wa kuwaona na kuwasikia? Kiufupi Hali ni mbaya na ndiyo maana ni ngumu kwa wasomi wa kizazi Cha Sasa kushindana na wasomi wa nchi za jirani katika soko la ajira kwa sababu Kama hizo.
aibu tupu kila kona. tz incompetents ndio tumejaa ikiwemo mimi
 
Kingereza Cha south Africa ni rahisi sana na hawatumii vocabulary ngumu, nachenyewe tumeshindwa wabongo.
 
Jana nilikuwa nawasikiliza baada ya mchezo wa Yanga dhidi ya Mamelodi kumalizika! Nilishangaa eti kuna binti alijitambulisha kutoka Manara tv!! Ndiyo tv ya wapi hii!!

Mimi nadhani ifikie wakati vyombo rasmi tu na vikubwa vya habari nchini, ndiyo vipewe nafasi ya kuuliza maswali kwa wageni. Hawa waandishi uchwara na vyombo vyao vya habari uchwara wabakie tu kuwa watazamaji.
 
Waandishi wa habari za michezo na uchambuzi wote ni makanjanja! Ifike mahali wasiruhusiwe kutoa uchambuzi wo wote zaidi ya kupiga picha maana ni aibu!

Pongezi kwa Gamondi kwa kuwapa vidonge vyao!
 
Ndugu yang edo kumwembe 😄

Ova
 
Yaani mzungu akiongea kiingereza broken hakuna shida lakini mwafrika watu wanacheka na kushangaa. Bado tuna safari ndefu🙂
 
Yaani mzungu akiongea kiingereza broken hakuna shida lakini mwafrika watu wanacheka na kushangaa. Bado tuna safari ndefu🙂
Shida sana , watu wa Europe akija ambaye English sio mother language anaongea broken ni sawa au kiswahili anaongea broken ni sawa ila sisi tunavyochekana sasa mpaka wangu wanaogopa
 
Back
Top Bottom