Mataifa jirani yanatuthibitishia kuwa sisi tunaopiga kelele kwenye mitandao kuhusu Corona tuna uelewa mpana kuliko CCM na Serikali yake

Mataifa jirani yanatuthibitishia kuwa sisi tunaopiga kelele kwenye mitandao kuhusu Corona tuna uelewa mpana kuliko CCM na Serikali yake

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Hili suala la COVID 19 kabla halijaanza kusambaa huko kwa majirani sisi huku tulipiga kelele sana. Tulipiga kelele tukabezwa, tukadharauliwa, tukatukanwa. Kumbe waliokuwa wakitutukana walikuwa hawajui chochote kuhusu huu ugonjwa. Aibu!

Kikundi cha sisi wa kwenye mtandao tumeonyesha mapenzi mema na hii nchi na zaidi tunaonekana kujua mambo kwa usahihi sana kuliko CCM na serikali yake. Tupo imara.

Hatimaye mataifa jirani yanathibitisha leo kuwa Tanzania ni epicenter kwa maambukizi ya Corona. Hilo kwa sasa halina mjadala tena.

Tutamuhukumu Rais Magufuli kwa wakati sahihi. Vifo hivi lazima vije kutolewa maelezo tena kwa usahihi. Hii ni nchi na kinachofanya nchi iwepo cha kwanza kabisa ni binadamu walio hai. Uongozi unaopuuzia uhai wa binadamu kamwe usipewe nafasi, huo ni uongozi wa maafa.

Tunaridhishwa na hatua wanazotuchukulia wenzetu. Nilionya kuwa wakati utafika nchi yetu itatengwa kwa kupuuzia hatua zinazotakiwa kuchukuliwa dhidi ya COVID 19. Tunaelewa kuwa zipo hatua kali zaidi zitafuata. Tuwe tayari kutumikia ukaidi wetu!
 
Ninakumbuka baa la kipindupindu liliibuka nikiwa mdogo. Ninakumbuka manesi waliweka kambi sokoni kutoa sindano ingawa wakati ule sikujua mantiki yake. Sasa hivi ndiyo ninaelewa kuwa ile ilikuwa Public Health Action.

Wakati ule tulikuwa na sera za elimu kwa wote. Kulikuwa na elimu ya watu wazima. Vijijini jioni wanaume walikaa pamoja kusikiliza taarifa ya habari ya saa mbili. Elimu ya kipindupindu ilitolewa.

Kulikuwa na vitabu vya elimu ya watu wazimavilivyokwenda na picha za kuchora. Vilieleza umuhimu wa kutumia choo na choo ni lazima kiwe na mfuniko.

Umuhimu wa kunawa mikono baada ya kutoka chooni na kabla ya kula.

Umuhimu wa kuosha matunda na mboga mboga

Umuhimu wa kuchemsha maji ya kunywa.

Ninadhani wakati ule walimudu kulidhibiti gonjwa mlipuko kuliko tulivyo limudu janga la corona sasa hivi.
 
Sky Eclat

Kulikuwa na vitabu vya elimu ya watu wazimavilivyokwenda na picha za kuchora. Vilieleza umuhimu wa kutumia choo na choo ni lazima kiwe na mfuniko.

NAKAZI HAPA,hakika sitosahau vile vitabu vyenye zile picha!

Old is good
 
Sky Eclat

Kulikuwa na vitabu vya elimu ya watu wazimavilivyokwenda na picha za kuchora. Vilieleza umuhimu wa kutumia choo na choo ni lazima kiwe na mfuniko.

NAKAZI HAPA,hakika sitosahau vile vitabu vyenye zile picha!

Old is good
Mantiki yangu ni kuwa umma haujapata elimu ya kutosha kuhusu corona. Sasa hivi tuna idadi kubwa ya wasiojua kusoma na kuandika. Hakuna njia inayolenga kutoa elimu ya kuwafikia.
 
Waambie wafunge kabisa mipaka yao,!

Lakini usisahau kwamba hili la corona haliwezi kuwaepusha chadema kupata kipigo oktoba mwaka huu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Haya ndiyo mawazo na akili za wanachama wa chama cha mapinduzi
Hawajui kwa kushoto wala kulia ni wapi.
Wapo wapo tu na mawazo ya uchaguzi,wala hawajui covid 2019 ni kitu gani na ina madhara gani kwa watu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nashangaa mpaka sasa yona wetu kapiga usingizi mzito kule burigi huku merikebu yetu ikiwa inazama na abiria hatushituki
 
Mkuu mbona tupo wana CCM tunaopenda kuwasikiliza madaktari zaidi kuliko wanasiasa katika suala hili la COVID19.
Leo nikamsikilize Makonda kuliko kumsikiliza daktari bingwa, itakuwa kichekesho.
 
Mitandao inafanya kazi mujarabu ya kuwaelimisha Watanzania
 
CCM ikiendelea kuongoza nchi baada ya janga la corona basi watanzania wote hapo nyumbani mnatakiwa kupimwa akili zenu.

Haiwezekani mnaachwe mfe ovyo ovyo kama kuku mwenye mdondo halafu mnaridhika tu

kush na Wisdom
 
Waambie wafunge kabisa mipaka yao,!

Lakini usisahau kwamba hili la corona haliwezi kuwaepusha chadema kupata kipigo oktoba mwaka huu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hii mada sio ya uchaguzi, na hata kama ni ya uchaguzi bado ccm hawana cha kujivunia kwenye uchaguzi, maana hawashindi kwa kura bali kwa matumizi mabaysla ya madaraka aliyonayo rais. Wananchi walishaamka zamani sana boss.
 
Back
Top Bottom