Tetesi: Mataifa yenye nguvu, matifa yenye kura ya veto UN na mataifa yanayomiliki silaha za nyuklia

Tetesi: Mataifa yenye nguvu, matifa yenye kura ya veto UN na mataifa yanayomiliki silaha za nyuklia

Proved

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2018
Posts
32,639
Reaction score
42,908
Salamu wote wanajukwaa kama kichwa cha habari hapo juu je kunatofauti Kati ya mataifa yaliyotajwa hapo juu? Je wakisema mataifa yenye nguvu ina maana ni Yale yenye uwezo wa kupiga kura ya veto huko UN? Vp kuhusu Japan na Ujerumani maana ni nchi tajiri utasema yana nguvu japo hayawezi kupiga Kura ya veto UN? Au nguvu ni kumiliki nyuklia tu basi Pakistan na India wana nguvu pia japo hapo UN hawana veto power na kiuchumi si sana? au nguvu ni kijeshi na kiuchumi pekee? Japo Japan haijawekeza sana kijeshi(japo wameanza kujihami dhidi ya China siku za karibuni) japo kiuchumi wako vizuri? Karibuni wadau mnipe ufafanuzi.
 
Mods naomba rekebisha tittle badala ya matifa isomekee mataifa.
 
Mataifa yenye kura ya VETO UNO ni waliokuwa washindi wa vita vya pili vya Dunia. siyo kwamba mataifa yenye kura ya VETO ndo pekee yenye Uchumi Mkubwa Duniani japo na wenyewe wapo vizuri. Mataaifa hayo ni USA, UK, France, RUSSIA na CHINA.
 
Back
Top Bottom