Matakwa ya Spika Ndugai kuhusu Kamati za Bunge kufuatilia mchakato wa ajira za walimu. Je, Serikali inafanya udanganyifu?

Huyu naye ni janga tu badala ya kuishauri serikali iongeze ajira ye anasema kuifuatilia vitu vidovidogo hivi
 
Nimemuona akiongelea hill bungeni lakin sijamuelewa kabisa!??
Nahisi kama amelalamikia kuna dalili za watu kutoka kanda Fulani wanapendelewa kwenye baadhi ya ajira nahisi alilenga kusema baadhi ya maeneo kwa kweli nimeshangaa saana
 
Mhe. Ndugai amenena jambo la muhimu sana kwa Taifa letu, jambo ambalo wengi walilifumbia macho lkn lina hatarisha umoja wa taifa letu nalo ni mgawanyo wa ajira na nafasi za uteuzi serikalini ulio sawia na wa haki, kimaeneo na hata kiimani, sio sahihi kujaza ktk utumishi wa umma watu wa aina mmoja halafu wengine wengi wakatupwa nje, hilo sio sahihi kabisa kwa ustawi na uzalendo wa taifa letu, lazima jambo hilo.litazamwe kwa kuzingatia sifa, usawa wa maeneo na hata usawa wa imani zote kushiriki ktk ujenzi wa taifa lao utaleta na kuimarisha uzalendo.
 
Kwa sasa hali ya wiano wa ajira ni issue kwa tanzania, wizara ya nishati na wizara madini 90% ya watumishi wake wanaongea lugha moja au niseme wametokana na kabila moja. Kuna wakati fulani TISS karibia wote walitokea mkoa wa Tanga,ilileta shida kubwa sana. Mzee Yusuph makamba akiwa Katibu Mkuu wa CCM, makatibu wa CCM mikoa na wilaya nchi nzima walitokea Tanga. Ndugai ulichokisema uko sawa, na ni mara ya kwanza Mh. Ndugai kusifiwa.
 
yupo sahihi na sidhani lengo lake lilikuwa kwa walimu ni zaidi ya hapo, kuna namna hizi nafasi haziwezi kuwapata watu fulani hata kama wana uwezo kuliko hao waliopo kwenye mifumo kwq sababu ya kujuana tu
 
Nimemuona akiongelea hill bungeni lakin sijamuelewa kabisa!??
Nahisi kama amelalamikia kuna dalili za watu kutoka kanda Fulani wanapendelewa kwenye baadhi ya ajira nahisi alilenga kusema baadhi ya maeneo kwa kweli nimeshangaa saana
ndo wakati sahihi kwa viongozi kubadilisha mfumo kwa kupendelea watu wa sehemu viongozi wanapotoka badala yake wapewe watu kutokana na sifa stahiki, utumishi uwe wa wote sio wa kikundi fulani
 
Watu wanazungumza ili wasikike si waeleweke.
hapana kaweka msingi na kwa level ya ndugai lazima atapeleka kwa waziri mkuu na raisi ili kubadilisha mfumo wa kuajiri ndani ya serikali, keki ya taifa iwe ni ta wote, kuanzia utumishi kitengo cha ajira, teuzi mbaliii mbali, na maeneo yote.... kuwe na sifa maalumu na watu wenye uwezo ndo wapate hizo nafasi.
 
ni kweli kabisa kuna kipindi cha mzee watu wa kanda ya ziwa walijazwa sana kwenye taasisi nyeti mpka kwenye mawizara na kila eneo wakaneemeka sasa hivyo mpka lini?? mabadiliko ni muhimu
 
Ikiwa ufuatiliaji huo ni kwania njema ya dhati ya moyo wake na ikiwa lengo ni kuiunga mkono awamu ya sita,itakuwa ni jambo jema sana.
Iko shaka, mbona spika amekuwa hivyo awamu hii. Ana bifu na mtu au anataka kujisafisha kutokana na kutotenda ipasavyo kipindi cha mwendazake?
Kwanini anayasema leo kwa mfano urari wa ajira ambao haukuzingatiwa kabisa na mwendazake. Yawezekana alinufaika na serikali ile na sasa anaona masilahi yake hayazingatiwi, au naye alimwogopa mwenda zake kama ilivyo kwa wengine wote. Ni bora tu aseme anayasema haya akiwa na rejea ya serikali ipi, iliyopita au hii ya sasa kwani vinginevyo tutadhani anabifu na serikali ya mama Samia.
 
Baada ya mama kusema bunge lijadili mambo yenye yenye tija kwa taifa, Ndugai kachukia, saa hii anajifanya anaibana serikali! Kwa taarifa yake bunge hili kibogoyo halina nguvu hiyo.
 
Angekuwa Spika akili kubwa angeliketisha bunge lifiriki,lishauri na kusimamia serikali namna ya kuondoa tatizo la ajira nchini.

Binafsi Sijaona "uspika " ktk kauli yake, fikiria walioomba ajira ni 120000 wanaotakiwa ni 6000,hao 114000 wataenda Wapi? Hiyo ndio ilipaswa kuwa hoja inayofaa mbunge /Spika.

Watanzania tuache umbumbumbu wa kufikiri, tatizo la nchi ni ajira hakuna, likitatuliwa hilo hatutakuja kujiuliza huyu ni kabila gani gani na yule ni kabila gani ameajiriwa.
 
Ninashauri ,katiba mpya ipatikane, spika,naibu spika, jaji mkuu, IGP na wengine, waanze nao kinyang'anyiro cha kufanya interview. Hizi teuzi hizi, tumeanza kuona matatizo yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…