mwagito25
JF-Expert Member
- Aug 11, 2013
- 633
- 352
Habarini wadau.
Leo nimeona nitoe maoni yangu kuhusu watu hawa wanajiita mitume na manabii na masheikh.
Mtu anatumia mafuta, maji, chumvi nk. Wanajiita ni mitume na manabii; je, Biblia inasema hivyo? Ingawa sina rejea ya vifungu moja kwa moja lakin matendo ya Yesu akiwa duniani alifanya miujiza kwa mbinu tofauti ambayo haikuwa kama kanuni. Alimfufua lazaro kwa maneno, aliponya vipofu kwa matope, alimfufua Dorcas kwa maneno nk. Hii inamaanisha nguvu za mungu kumponya mtu hazina kanuni moja.
Hawa watu wanatumia kanuni kuwasaidia watu ni matepeli na nachelea kusema kwamba kuna nguvu ambayo sio ya Mungu wanaitumia ili kujinufaisha.
Nasema hivi kwa sababu, kama wanatumia nguvu za Mungu, biblia inasema "MMEPEWA BURE TOENI BURE", sasa kwanin wao wanazuga kwa kugawa hayo mafuta, chumvi au maji bure kwa wachache kisha wanaanza KUYAUZA. Je, tangu lini NGUVU ZA MUNGU HUWA ZINAUZWA? Sama sio utapeli ni nini?
Lakini naenda mbali kidogo kama kweli wao ni wajumbe wa Mungu Kwanini wasitufundishe sisi wenye shida namna ya kukaa vizuri na Mungu ili hatimaye, watufundishe kuyaombea hayo maji, chumvi na mafuta ili vitufae kwa shida zetu? Kama sio mfumo wa kutuibia na kututapeli ni nini?
Nawaonea huruma watu ambao wanzidi kudanganywa na kuibiwa. Kwa wanaomwamini Mungu wanajua kuna maisha mengine baada ya hapa duniani. Hawa mabwana huwa hawahibir hizi habari zaidi ya kuzungumza kuhusu mafanikio tu. Kwanini wasijadili na kesho yetu pia?
Kwa leo tuishie hapa lakin huu ni uzi huru. Mawazo huru yanakaribishwa.
ITAENDELEA
Leo nimeona nitoe maoni yangu kuhusu watu hawa wanajiita mitume na manabii na masheikh.
Mtu anatumia mafuta, maji, chumvi nk. Wanajiita ni mitume na manabii; je, Biblia inasema hivyo? Ingawa sina rejea ya vifungu moja kwa moja lakin matendo ya Yesu akiwa duniani alifanya miujiza kwa mbinu tofauti ambayo haikuwa kama kanuni. Alimfufua lazaro kwa maneno, aliponya vipofu kwa matope, alimfufua Dorcas kwa maneno nk. Hii inamaanisha nguvu za mungu kumponya mtu hazina kanuni moja.
Hawa watu wanatumia kanuni kuwasaidia watu ni matepeli na nachelea kusema kwamba kuna nguvu ambayo sio ya Mungu wanaitumia ili kujinufaisha.
Nasema hivi kwa sababu, kama wanatumia nguvu za Mungu, biblia inasema "MMEPEWA BURE TOENI BURE", sasa kwanin wao wanazuga kwa kugawa hayo mafuta, chumvi au maji bure kwa wachache kisha wanaanza KUYAUZA. Je, tangu lini NGUVU ZA MUNGU HUWA ZINAUZWA? Sama sio utapeli ni nini?
Lakini naenda mbali kidogo kama kweli wao ni wajumbe wa Mungu Kwanini wasitufundishe sisi wenye shida namna ya kukaa vizuri na Mungu ili hatimaye, watufundishe kuyaombea hayo maji, chumvi na mafuta ili vitufae kwa shida zetu? Kama sio mfumo wa kutuibia na kututapeli ni nini?
Nawaonea huruma watu ambao wanzidi kudanganywa na kuibiwa. Kwa wanaomwamini Mungu wanajua kuna maisha mengine baada ya hapa duniani. Hawa mabwana huwa hawahibir hizi habari zaidi ya kuzungumza kuhusu mafanikio tu. Kwanini wasijadili na kesho yetu pia?
Kwa leo tuishie hapa lakin huu ni uzi huru. Mawazo huru yanakaribishwa.
ITAENDELEA