Bwana Bima
JF-Expert Member
- Jul 29, 2014
- 429
- 929
Nikiwa nasikiliza idhaa ya kiswahili ya dw Leo mchana moja ya wachambuzi wa maswala ya migogoro huko Congo alitoa ufafanuzi juu ya kikosi kingine Cha SADC Ambacho kinajiandaa kwa awamu nyingine kutumwa huko DRC.
Kilichonishangaza ni pale alipoulkuliwa akisema wanajeshi wakongo wanataka vita na hali ya machafuko iendelee wakihofia kwamba kama vita na machafuko vikiisha basi na wao watapoteza ajira na fursa za kupata Mali.
Jambo hili lilinifanya nijiulize maswali mengi sana. Inaamana hawa wanajeshi moyo wa uzalendo kuhusu nchi Yao hawana? Nini kiini Cha hali kufika hatua hio? Vita inahitaji hari na utayari wa jeshi je wakiwa uwanja wa mapambano wanaweza kuhimili mikiki ya vita? Kama ni hivyo hata kama Rwanda anahusika kuiba Mali huko DRC kutia ndani ya nchi za magharibi je hio haiipi nguvu zaidi hzi nchi kama ni kweli kuendelea kuiba na kuiba zaidi Mali na rasilimali za DRC? Inafikirisha sana. Nadhani ndio sababu kwasasa Tanzania haipeleki Tena jeshi lake huko.Naona kupeleka jeshi huko ni hatari kupita maelezo.
Wajuzi wa mambo naombeni maoni yenu kuhusu hili.
Kilichonishangaza ni pale alipoulkuliwa akisema wanajeshi wakongo wanataka vita na hali ya machafuko iendelee wakihofia kwamba kama vita na machafuko vikiisha basi na wao watapoteza ajira na fursa za kupata Mali.
Jambo hili lilinifanya nijiulize maswali mengi sana. Inaamana hawa wanajeshi moyo wa uzalendo kuhusu nchi Yao hawana? Nini kiini Cha hali kufika hatua hio? Vita inahitaji hari na utayari wa jeshi je wakiwa uwanja wa mapambano wanaweza kuhimili mikiki ya vita? Kama ni hivyo hata kama Rwanda anahusika kuiba Mali huko DRC kutia ndani ya nchi za magharibi je hio haiipi nguvu zaidi hzi nchi kama ni kweli kuendelea kuiba na kuiba zaidi Mali na rasilimali za DRC? Inafikirisha sana. Nadhani ndio sababu kwasasa Tanzania haipeleki Tena jeshi lake huko.Naona kupeleka jeshi huko ni hatari kupita maelezo.
Wajuzi wa mambo naombeni maoni yenu kuhusu hili.