Matatizo ya matege

NGOSWE2

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2013
Posts
1,323
Reaction score
1,608
Heshima kwenu wakuu! Kuna dawa au aina ya chakula chochote kinachoweza kupoteza matege kwa mtoto mdogo mwenye umri wa miaka 3?

Nina dada yangu wenye mtoto wa tatizo hilo. Maana nimesikia CCBRT wanaweza kuinyosha kwa njia ya upasuaji, lakini dada yangu anaigopa njia hiyo.

Mwenye kujua njia zaidi ya hiyo tafadhari.
 
Miaka mitatu mbona mapema? Yatakuja kuisha yenyewe tu naturally unless kama ana kilema kabisa. Mtoto wa dada alikuwa na matege ya kutisha mpaka tuliogopa. Daktari hata hivyo akituhakikishia kuwa akifikisha miaka mi5 yatakuwa yamekwisha. Na kweli ikawa hivyo.
 

Nashukuru mkuu kwa ushauri wako. Maana sister aliingiwa na hofu sana.
 
Kuna vile viatu wanavalishwaga ya kunyoosha mifupa pia
 
Hapo jamaa yangu ni kumlisha dagaa kwa wingi sana! Calcium imepungua sana.
 

nina uzoefu wa hili, inategemea ni ya magoti kuingia ndani au kutoka nje ? km ni ya ndani kweli yanaweza kunyooka yenyewe hadi miaka 6, tatizo la njia hii km hayatanyooka kikamilifu na tayari amekomaa njia ya viatu haiwezikani inakuwa ngumu sana, kama ni makubwa ni bora kumvalisha viatu vya vyuma angali mdogo kabisa asisumbue kwa usiku tu wakati wa kulala nadhani ndani ya wiki nne hadi sita yatosha baada ya hapo unamuacha anaendelea kunyooka automatically, kuhusu chakula mm sina uhakika..

viatu vinawekwa vyuma/nondo hadi kwenye mapaja na kufungwa kwa mkanda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…