Matatizo ya Nissan X Trail

Matatizo ya Nissan X Trail

otimbiotimbi

Senior Member
Joined
Dec 12, 2019
Posts
132
Reaction score
230
Hivi karibun kumeibuka wimbi la watu wengi wakiuza gari hii kwa gharama ya chini sana na baadhi ya watu wakiogopa kununua na wamiliki nao wakiwa wanayachukia magari yao.

NISSAN X TRAIL
Ina block ya aluminium inawahi mno kupata moto kama injin ya Noah voxy 1az. Hivyo ukizembea kidogo tu katika mfumo wa upozaji wa injin basi gari hii itakusumbua sana. Hakikisha hawatoi thermostat. Hakikisha rejeta haina uchafu yani kutu, kuwa na kawaida ya kufanyia service rejeta. Ukifika carwash usioshe injini kwa pressure ya maji.

Gari hii usipo zingatia nilichokuelekeza hapo juu itaanza kusumbua na Ikisumbua ukipeleka kwa mafundi wa mtaani wakishindwa kurekebisha tatizo wanaanza kuwaambia wamiliki kuwa gari hizo mbovu na ndio kawaida yake mmiliki atatoka ataenda sehemu nyingine atakutana na mafundi wa mtaani tena maneno yatakuwa ndio hayo utasikia wanasema gari hii ni jini. Haya sasa ukimuuliza ambazo sio majini ni zipi?

Nissan-X-Trail.jpeg

Watakutajia gari ambazo wao wanaweza kubahatisha kutengeneza ndio kwao wanaona bora wakati tatizo sio gari tatizo ni wao wameshindwa kutengeneza na ukiangalia wanaoongoza kwakusema hivyo na kuwakatisha tamaa ni wale wanaoitwa mafundi wakuu.

Sasa akishasema hivyo mpaka wanafunzi wake wote wimbo ni mmoja majini hayo! Kama jana nilienda sehemu nikakuta Nissan Xtrail haibadili gia, fundi kapima na mashine ina mwambia kuna sensor imekufa kanunua nyingine kafunga tatizo liko pale pale nafika namuhoji ananiambia Mimi hiyo gari imenishinda yani nilikaa kimya tu mana huyo ndie fundi ambae anategemewa na vijana anafundisha.

Sasa hapo wamekaa pembeni na vijana wake unasikia wana sema hizi gari ndivyo zilivyo yani hawana muda wakuumiza kichwa fikra na maarifa yamefungwa ndani ya mashine anayo itegemea ikifika kikomo na yeye hana muda wakujifunza zaidi wala kutafuta maarifa kazi yao nikutisha wamiliki wa magari tu.

Nissan Xtrail ina sensor nyingi mno sasa mafundi wa mtaani somo la sensor hawalijui lazima wasumbuke na pia kwenye injin huwa ikianza kuchemsha hawajui wafanye nini.

Ni hayo tu kwa leo🙏🙂
 
Shida hii gari oil yake ni expensive sana,wengi hawapendi kutumia genuine coolant.

Mfumo wake wa umeme hautakibshortcut.yaan ikianza shortcut gari itasumbua sana.
Oil expesnive ni tsh ngapi mkuu? Coolant nayo ni tsh ngapi? Mbona bei ya kawaida sana.

Mi nina huo mninga mwaka wa 8 sasa na haisumbui chochote. Nina ile ya 2005 rangi nyekundu.
 
Shida hii gari oil yake ni expensive sana,wengi hawapendi kutumia genuine coolant.

Mfumo wake wa umeme hautakibshortcut.yaan ikianza shortcut gari itasumbua sana.
Hizo ulizotaja sio shida za gari bali ni shida za waswahili, ukiangalia xtrail japani kule zipo hadi zilizotembea km 300k, ukiiagiza ikija huku 3rd world country inakuwa bado "mpya" ila mswahili akikaa nayo mwaka anapiga yote eti shida ya hizi gari, shida sio gari shida ni wewe unayemiliki hiyo gari
 
Oil expesnive ni tsh ngapi mkuu? Coolant nayo ni tsh ngapi? Mbona bei ya kawaida sana.

Mi nina huo mninga mwaka wa 8 sasa na haisumbui chochote. Nina ile ya 2005 rangi nyekundu.

Washamba hawa sijui wanataka gari iweje, coolant 15k na sio kwamba unaweka kila siku wao wanaona bora wajaze maji. Mimi ninayo ya diesel 2010 model oil yake 15w 30 ni 130,000 kwa eneo nilipo unaenda hadi km 6000 kwa service, unatakaje tena?

Kwahiyo unataka udoee oil ya boda iliyomwagwa na kuweka maji ya chumvi badala ya coolant alafu unalaumu gari. Pathetic
 
Wabongo Kwa kutishana Tu tuko vizuri sanaa..
Kilasiku nawaambia watu shida sio magari tunayotumia Bali ni Sisi wamiliki, haiwezekani gari inatoka Japan ikiwa haina shida yeyote na ikishafika bongo ndani ya miezi 3 inakufa
 
Washamba hawa sijui wanataka gari iweje, coolant 15k na sio kwamba unaweka kila siku wao wanaona bora wajaze maji. Mimi ninayo ya diesel 2010 model oil yake 15w 30 ni 130,000 kwa eneo nilipo unaenda hadi km 6000 kwa service, unatakaje tena?

Kwahiyo unataka udoee oil ya boda iliyomwagwa na kuweka maji ya chumvi badala ya coolant alafu unalaumu gari. Pathetic
Hahaaaaaa inasikitisha sana. Mi.ndiga nadunda nayo tu ki old school.
 
Kwa
Hivi karibun kumeibuka wimbi la watu wengi wakiuza gari hii kwa gharama ya chini sana na baadhi ya watu wakiogopa kununua na wamiliki nao wakiwa wanayachukia magari yao.

NISSAN X TRAIL
Ina block ya aluminium inawahi mno kupata moto kama injin ya Noah voxy 1az. Hivyo ukizembea kidogo tu katika mfumo wa upozaji wa injin basi gari hii itakusumbua sana. Hakikisha hawatoi thermostat. Hakikisha rejeta haina uchafu yani kutu, kuwa na kawaida ya kufanyia service rejeta. Ukifika carwash usioshe injini kwa pressure ya maji.

Gari hii usipo zingatia nilichokuelekeza hapo juu itaanza kusumbua na Ikisumbua ukipeleka kwa mafundi wa mtaani wakishindwa kurekebisha tatizo wanaanza kuwaambia wamiliki kuwa gari hizo mbovu na ndio kawaida yake mmiliki atatoka ataenda sehemu nyingine atakutana na mafundi wa mtaani tena maneno yatakuwa ndio hayo utasikia wanasema gari hii ni jini. Haya sasa ukimuuliza ambazo sio majini ni zipi?


Watakutajia gari ambazo wao wanaweza kubahatisha kutengeneza ndio kwao wanaona bora wakati tatizo sio gari tatizo ni wao wameshindwa kutengeneza na ukiangalia wanaoongoza kwakusema hivyo na kuwakatisha tamaa ni wale wanaoitwa mafundi wakuu.

Sasa akishasema hivyo mpaka wanafunzi wake wote wimbo ni mmoja majini hayo! Kama jana nilienda sehemu nikakuta Nissan Xtrail haibadili gia, fundi kapima na mashine ina mwambia kuna sensor imekufa kanunua nyingine kafunga tatizo liko pale pale nafika namuhoji ananiambia Mimi hiyo gari imenishinda yani nilikaa kimya tu mana huyo ndie fundi ambae anategemewa na vijana anafundisha.

Sasa hapo wamekaa pembeni na vijana wake unasikia wana sema hizi gari ndivyo zilivyo yani hawana muda wakuumiza kichwa fikra na maarifa yamefungwa ndani ya mashine anayo itegemea ikifika kikomo na yeye hana muda wakujifunza zaidi wala kutafuta maarifa kazi yao nikutisha wamiliki wa magari tu.

Nissan Xtrail ina sensor nyingi mno sasa mafundi wa mtaani somo la sensor hawalijui lazima wasumbuke na pia kwenye injin huwa ikianza kuchemsha hawajui wafanye nini.

Ni hayo tu kwa leo🙏🙂
Kwa nini uweke maji ya bomba kwa rejeta bana?
 
Ninayo Nissan namba A natumia mpaka sasa na ni jana tu nimetoka nayo Kigoma kuja hapa Dar bila kusimama popote
 
Mu acknowledge mtu aliyeandika nawe uka copy na kuleta hii thread hapa.

We umeshawahi kumiliki Xtrail? Mbona hazina shida wazee tunazitumia miaka dahali sasa hizo gari ikiwemo lile tolea la 2005 wakati wewe hujazaliwa?
Kujua uzuri wake au shida zake si lazima umiliki gari husika. Lakini pia sidhani kama mtoa mada ameilalamikia gari moja kwa moja labda kama umesoma kichwa cha habari na sentensi 1 au 2 za kwanza. Kwa mtazamo wangu ameongea vizuri na kutoa angalizo zuri.
Binafsi xtrail ni gari nazozipenda lakini hata mimi nimeshasikia sana story zake za kutisha, hasa generation ya kwanza. Na nakiri mpaka leo, bado naiogopa hiyo generation ya kwanza. Ila generation ya pili kuendelea sijasikia hizo horror stories.
Na natamani kuendelea kupata ushauri zaidi jinsi ya kuishi nayo, ukiacha suala la engine oil ambalo nalijua, na utunzaji wa gear box (hasa kama ni CVT za jatco)
 
Washamba hawa sijui wanataka gari iweje, coolant 15k na sio kwamba unaweka kila siku wao wanaona bora wajaze maji. Mimi ninayo ya diesel 2010 model oil yake 15w 30 ni 130,000 kwa eneo nilipo unaenda hadi km 6000 kwa service, unatakaje tena?

Kwahiyo unataka udoee oil ya boda iliyomwagwa na kuweka maji ya chumvi badala ya coolant alafu unalaumu gari. Pathetic
Mkuu nisaidie kujua uzuri na mabaya ya Nissan xtrail ya diesel nawaza kuinunua. Masuala ya diesel filter upatianaji wake, ulaji wa diesel
 
Mkuu nisaidie kujua uzuri na mabaya ya Nissan xtrail ya diesel nawaza kuinunua. Masuala ya diesel filter upatianaji wake, ulaji wa diesel
Ulaji n mzuri sana, filter zake zipo ingawa gharama kidgo mfano, oil filter genuine unapata kwa 20k, na diesel filter genuine unapata kwa 70k
 
Back
Top Bottom