Mateso wanayopata wastaafu

Mateso wanayopata wastaafu

NostradamusEstrademe

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2017
Posts
3,402
Reaction score
4,532
Mtu aliyezaliwa mwaka 1959 kwa sasa ana miaka 62. Kama alianza kidato cha kwanza mwaka 1975 ina maana amemaliza kidato cha nne mwaka1978. Kama amesoma kozi mathalani ya uuguzi kwa miaka minne maana yake amemaliza1982. Ajira ameanza mwaka1983.

Ukipiga hesabu hapo hadi mwaka 2019 atakuwa amefikisha miaka 60 ndio anastaafu na atakuwa amefanya kazi ya utumishi kwa miaka36.

Huyu muuguzi amefanya kazi kwa uadilifu mkubwa mno miaka yake yote amejitoa mhanga na amekumbana na hatari nyingi sana kukoswa koswa na kuambukizwa magonjwa mbali mbali siyataji ila kwa sasa ugonjwa wa changamoto za kupumua kama unavoitwa siku hizi wakati mwingine hata Ebola.

Muuguzi huyu amekutana na madhila wakati mwingine hata kuhatarisha ndoa yake kwa kufanya kazi usiku akiacha watoto wake na mumewe shauri ya kuingia night. Muuguzi huyu anapokwenda kazini usiku kwa usalama wake hata kuvamiwa na vibaka aidha akienda au akirudi. Muuguzi huyu wakati mwingine anakutana na wagonjwa waliokengeuka akili kumuambia maneno machafu. Muuguzi huyu hata pia amehatarisha maisha yake maana amekutana na wagonjwa wenye akili pungufu wanaweza kumdhuru. Hivi karibuni kuna mgonjwa alimchoma kisu muuguzi akafariki dunia. Muuguzi huyu kazi yake alikuwa hana siku kuu ilimradi kama ni zamu yake hakuna sikukuu mfano hizi za pasaka.

Muuguzi huyu sisi masikini, wanasiasa, watu wakubwa sana wa serikali, mashirika, vyama vya siasa, maraisi, wafalme, malkia n.k unapozidiwa anageuka anakuwa kama mama au mke wako anakuogesha na kukulisha chakula. Hapa hata aibu yako anaiona anakutunzia siri hata kama una kovu mahali flani.

Kimbembe sasa ngoja kinakuja siku ya kustaafu pamoja na wema woote na kujitolea maisha yake yote anaonekana kama vile tinga tinga linalochimba barabara linatengeneza barabara vizuri sana lakini barabara ikiisha halitakiwi tena kuikanyaga hiyo barabara na hata likipita litaambiwa linabomoa barabara. Na sana sana likionewa huruma sana litapita kwa ungalizi maalum likiwa limebebwa na Trailer lingine.

Basi mfanyakazi wa umma,sekta binafsi ndio inakuwa hivyo mtu akistaafu hatakiwi tena.Mfuko wake mwenyewe aliojinyima maisha yake yote anaupata kwa shida sana au kwa mateso makubwa mno hii hata mbele ya mungu ni machukizo makubwa taifa linaingia kwenye laana bila kujua nasikia eti laana inaweza kwenda hadi kizazi cha nne labda atokee mjanja mmoja ashtuke kwa kufanya tambiko au maombi.

Hii mifuko ya jamii nauliza inamsaidia vipi mstaafu au ni siasa maana kipindi unapoanza kazi wanavyokuja kukubembeleza ni sawa na konda ukipanda gari anakubembeleza anakuambia kuna siti za kulala ila gari likifika kituo cha mwisho hataki hata kukuona usoni afadhali kwenye ndege. Hapa nimetoa mfano huu afadhali kwenye ndege nikiamanisha baadhi ya nchi hasa zilizoendelea mtu akistaafu anaishi maisha raha mustarehe japo sio ya kifahari hadi kifo chake kwa sisi ni tofauti.

Naandika haya kwa uchungu dada mmoja amefanya kazi miaka niliyoianisha na amestaafu december mwaka2019 kwa maana hiyo anatafuta mwaka wa pili sasa achilia mbali kinywa mgongo chake hajapata hata senti tano.

Kama ni faili na mahesabu ni mahesabu gani yanapigwa kwa muda wa miaka miwili? inauma sana hii kitu. Last few months kuna askari walistaafu mhe Marehemu John Pombe Magufuli(Mungu amuweke pema) aliweka biti flani kuwa waliostaafu hao askari wapewe mafao yao haraka nina uhakika hili lilifuatiliwa na marehemu inaonekana anajua kuna mizengwe kwenye kulipa wastaafu. Je, huyu Muuguzi, daktari, mfamasia, mkutubi, mwalimu n.k ni nani anayewalilia?

Nimeshapata jibu kuna usemi unasema mtu akistaafu anaishi maisha mafupi sio kweli ni kwamba angeishi lakini kwa frustration kama hizi lazima kweli mtu atakufa na tena nachelea kusema wengine wanakufa kabla hata ya kuchukua mafao yao.

Mimi binafsi ingekuwa ni choice mtu aamue mafao yake yaingie wapi nisingechagua mfuko wowote wa kijamii ila sana sana ningefungua akaunti maalum benk ambayo naweka sharti siruhusiwi kuchukua ili angalau wakati nachukua wakati huo kutakuwa tayari na faida kuliko mifuko yetu hii inayozingua zingua sana. Naelewa mifuko iko tofauti ila samaki mmoja akioza ni wote.

Mimi ningependekeza kitu kimoja mtu anapokaribia kustaafu mwaka mmoja kabla taarifa inatolewa mahesabu yanaanza kupigwa kabla muda wa kustaafu ukifika analipwa muda huo huo.Wakati wa utawala wa JK kuna chombo kiliwekwa kusimamia hii mifuko yote je hicho chombo kinasemaje kwenye hili? Mimi nina uhakika kabisa kuna baadhi ya kada za kazi humu nchini hizi shida haziwagusi wanasiasa wakiwepo ambao ndio watunga sera hizo hizo za mafao.

MAMA SAMIA NAKUOMBA SANA MAMA YETU NAJUA UNA KAZI NYINGI NA CHANGAMOTO NYINGI MNO KAZI YA URAISI SIO RAHISI KAMA WATU WANAVYOFIKIRIA NAOMBA UCHUNGULIE HUKU KWENYE HIVI VYUNGU VINAVYOWEKA HELA ZA WATU HAZITOKI KULIKONI.
 
Mzee wangu mwezi wa tatu wamemtaarifu kabakiza siku tisini kustaafu,yani mwezi wa saba ndo mwisho wa kazi hivo apeleke taarifa zake, anepeleka wiki ilopita wamemwambia mwajiri wako hakuweka pesa yako tangu mwaka 1998, nikwamba zaidi ya miaka 20, amekatwa pesa ila waliko peleka wanajua wao, huyu mzee yuko ugenini mana alihamishwa, kwa hali mtu unaishije jamani.
 
Mzee wangu mwezi wa tatu wamemtaarifu kabakiza siku tisini kustaafu,yani mwezi wa saba ndo mwisho wa kazi hivo apeleke taarifa zake, anepeleka wiki ilopita wamemwambia mwajiri wako hakuweka pesa yako tangu mwaka 1998, nikwamba zaidi ya miaka 20, amekatwa pesa ila waliko peleka wanajua wao, huyu mzee yuko ugenini mana alihamishwa, kwa hali mtu unaishije jamani.
Daaaaaa!
 
Kuna mtumishi mmoja alimuona mstaafu wa kada yake jins anavyo teseka baada ya kustaafu , yule jamaa akasema kama hali ni hii basi ni bora kufa kabla ya kustaafu
 
Mifuko ya kulipa wastaafu ipo hoi bin taabani. Wanasiasa walikomba kupeleka kwenye miradi ya maendelekeo. Hii ndiyo maana ya msemo punda afe mzigo ufike. Wanasiasa nikiwakuta ama nikasikia wameingia peponi ntakata rufaa.
 
Mzee wangu mwezi wa tatu wamemtaarifu kabakiza siku tisini kustaafu,yani mwezi wa saba ndo mwisho wa kazi hivo apeleke taarifa zake, anepeleka wiki ilopita wamemwambia mwajiri wako hakuweka pesa yako tangu mwaka 1998, nikwamba zaidi ya miaka 20, amekatwa pesa ila waliko peleka wanajua wao, huyu mzee yuko ugenini mana alihamishwa, kwa hali mtu unaishije jamani.
Mmhhh!!!, Kauli km hii aliwahi kuambiwa mstaafu mmoja aliyekuwa Karani wa mahakama nakwambia pale pale ofisi za watu wa Mafao alianguka chini akapoteza fahamu akakimbizwa hospitali na ndo ukawa mwisho wa uhai wake.Jamani Mama Samia afanye kitu kuwasaidia Wastaafu, vinginevyo wengi watakufa kwa mawazo.
 
Magufuli alikuwa mzee wa mindgame akiwa na sisi anajifanya kuwakaripia maafisa wa mifuko ya kijamii ukweli anaujua kuwa pesa amechukua yote

Lkn bado anayo misukule yake inayomuamin had leo na hawaamin Kama amekufa

Alianzisha kikokotoo kipya ili aendelee kuiba vizur pesa zetu kwenye mifuko na alijua hata achia nchi hii hata mda wake ukifika

Kifo cha cha jiwe kimeipa fundisho nchi na suala la kuangalia katiba anaweza akapatikana Rais chizi mwingne akatuburuza Zaid ya jiwe
 
Namshukuru sana Mhe. Rais ambaye ametufungua macho na kusema kwamba PSSSF ambalo ni Shirika linaloshughulikia mafao ya Wafanyakazi wa Umma lipo hoi bin taaban kifedha. Hii ndio sababu mstaafu anapoulizia mafao yake hupewa majibu ya ajabu sana. Mbona kikokotoo, pamoja na kwamba si rafiki, kinaeleweka kabisa? Ni kiasi cha kujaza kwenye hiyo program na paaa jibu linatoka. Mimi ninacho kwenye kompyuta mpakato yangu na nalijua hilo. Inavyoelekea hakuna uwazi katika hili na matokeo yake wastaafu wanapata usumbufu kwa kutoambiwa ukweli.
 
Mzee wangu mwezi wa tatu wamemtaarifu kabakiza siku tisini kustaafu,yani mwezi wa saba ndo mwisho wa kazi hivo apeleke taarifa zake, anepeleka wiki ilopita wamemwambia mwajiri wako hakuweka pesa yako tangu mwaka 1998, nikwamba zaidi ya miaka 20, amekatwa pesa ila waliko peleka wanajua wao, huyu mzee yuko ugenini mana alihamishwa, kwa hali mtu unaishije jamani.
😡😡 Huu ni uonevu. Unaweza nunua godoro ukahamia kabisa kwenye ofisi zao.
 
Magufuli alikuwa mzee wa mindgame akiwa na sisi anajifanya kuwakaripia maafisa wa mifuko ya kijamii ukweli anaujua kuwa pesa amechukua yote

Lkn bado anayo misukule yake inayomuamin had leo na hawaamin Kama amekufa

Alianzisha kikokotoo kipya ili aendelee kuiba vizur pesa zetu kwenye mifuko na alijua hata achia nchi hii hata mda wake ukifika

Kifo cha cha jiwe kimeipa fundisho nchi na suala la kuangalia katiba anaweza akapatikana Rais chizi mwingne akatuburuza Zaid ya jiwe
👊👊
 
😡😡 Huu ni uonevu. Unaweza nunua godoro ukahamia kabisa kwenye ofisi zao.
Nini godoro,sema unaweza kuingia na panga kwenye ofisi zao na ghafla ofisi zinageuka bucha ya nyama ya binadamu.Mambo mengine yanakera sana mkuu
 
Serikali ya ccm ilichukua hela hela zote ikajenga mamiradi na hao wazee wakashangilia.


Vijana tulipowaambia ukweli wakatuita chadema au ukawa na tupo tuliohamishiwa vijijini.

Tutaelewana tu. 2035 vijana tuanze harakati za kudai pension nzuri, tukipiga harakati kwa miaka 10 watasarenda tu, tunastaafu kwa heshima.
 
Jiwe alikua mwizi sana yule dingi na peponi hataenda yule jamaa.

Ametesa wastaafu sana yule jamaa.
 
Hivi mifuko imechezewa sana. Kipindi cha Kikwete ilijiingiza kwenye miradi isiyoleta faida kama kujenga maghorofa makubwamakubwa kwa sifa. Kipindi cha jiwe ikageuka ndiyo hazina.

Seriakali inatakiwa kuhakikisha usalama wa hii mifuko, kuhakikisha hela za watumishi zinawekezwa kwenye miradi salama ambayo yenyewe inaigarantii na si kugeuza mifuko hii kuwa kibubu chake.

Ilitakiwa mtu apate pesa yake siku ileile anastaafu na si kuzungushana na longolonho kumbe pesa wametafuna.
 
Najikuta nawachukia wasukuma kwa sababu ya mtu mmoja tu jiwe
 
Hivi hii mifuko haiwezi kushitakika mahakamani kwa kuchelewesha mafao ya watu?
 
Nini godoro,sema unaweza kuingia na panga kwenye ofisi zao na ghafla ofisi zinageuka bucha ya nyama ya binadamu.Mambo mengine yanakera sana mkuu
Hii ni hatari maana wengine wanaweza kwenda na petroli wakajilipua na wakaweza kulipua ofisi pia. Huu uonevu kweli umalizike. Shemeji yenu anastaafu mwaka kesho yasije yakamkuta hayo sijui itakuwaje yakitokea hayo maana ameshaaza kujimwambwafai kwamba atatoka na donge nono. Yakitokea nitakuwa na kazi ya ziada kumtuliza.
 
Mzee wangu mwezi wa tatu wamemtaarifu kabakiza siku tisini kustaafu,yani mwezi wa saba ndo mwisho wa kazi hivo apeleke taarifa zake, anepeleka wiki ilopita wamemwambia mwajiri wako hakuweka pesa yako tangu mwaka 1998, nikwamba zaidi ya miaka 20, amekatwa pesa ila waliko peleka wanajua wao, huyu mzee yuko ugenini mana alihamishwa, kwa hali mtu unaishije jamani.
Inafanana na hii picha Nurse kafanya hospitali kubwa private siku anastaafu anaambiwa michango yako mwajiri alikuwa hapeleki inauma sana ni bora kutungwe sheria kuingia mifuko ya jamii iwe ni hiari wanaatamka hivyo kwa hiari lakini ukweli sio hiari.Hivi ukiweka account maalum CRDB kuwe na sharti hakuna kuchukua hela si bora zaidi kuliko hii mifuko yao?

nurse.PNG
 
Back
Top Bottom