matibabu kwa njia ya kompyuta

Hivi smile na ujanja wote unaliwa 50, unachunguliwa kirahisi namna hii! Loh! Isitoshe majitu yenyewe yaliyokuchungulia hayana hata ethics siku ukipita bar yanaanza kusimuliana. Duh! Wajinga ndio waliwao.
 

Sasa kama siyo cyst sasa waumwa nini? Naona umetuficha au ni siri nayo hiyo?
 
Hivi smile na ujanja wote unaliwa 50, unachunguliwa kirahisi namna hii! Loh! Isitoshe majitu yenyewe yaliyokuchungulia hayana hata ethics siku ukipita bar yanaanza kusimuliana. Duh! Wajinga ndio waliwao.
acha tu ndugu yangu yaani siamini hata sasa halafu watu wamepiga foleni pale balaa ,nenda uone
 
nyonga tu ndo inauma kidogo ni cause ya ovulation bwana

Hilo ulilijua hata kabla hujaenda kwa wamakompyuta maana hayo si ni maumivu tu? Je kiini chake ni nini?
 
Mkome!!!!mi nilishawahi kwenda kwa mmoja hivi,ilikua miaka ya 2005 kule Jet Lumo,eti kufanya check up ya hiyo kipimo,koz nilikua na maumivu ya tumbo,akaniambia eti kidney imeshindwa kupeleka CALCIUM kwenye utumbo mwembamba!!!nilichoka.....
 
Mie nataka wanipime nyonga yangu kwa ndani ina mfupa wa aina gani?? Kwa mouse lakini! Pole mwaya ndio mjini laaziz! Smile upo wangu?
 
Last edited by a moderator:
Duh umenijanjarusha nilikuwa na mpango wa kwenda kufanyiwa hivyo.Sasa ninatoka nduki kama ndege aliyepuruchuka kwenye mutego.
 
Pole sana
Kweli siku hizi town kuna usanii sana hususani hizi hospital zinazojidai ni za dot com
 
acha tu ndugu yangu yaani siamini hata sasa halafu watu wamepiga foleni pale balaa ,nenda uone

nipe ramani ya hapo mahali, ili nami niwe tomaso. Nitaenda kuwaambia kengele zangu zinaniuma
 

Hii dunia ya ajabu sana; Ukiwa mwanaume tabu, ukiwa mwanamke ndo kabisaaaaaaaaaaa! i wish huku mahala kungekuwa 'flat' nisingepata tabu kabisa!
 
Smile.. hao sio wachina? maana nakumbuka kuna kipindi nilipata allergy mwili ulikuwa unavimba kuna siku nikaenda Clinic ya wachina nilipofika pale wakanicheki halafu wakanilaza kitandani wakanitundikia Drip moja la dawa, wakanichoma sindano kwenye paja, halafu wakanivua shati wakanilaza kifudifudi wakaniwekea madudu fulani utadhani hirizi kama nane hivi mgongoni yameunganishwa na nyya na kuna kimtambo wakakiwasha kikaanza ku vibrate mwili wote ukawa una vibrate, wakahamia mapajani hivyo hivyo,,

walipomaliza wakaniandikia dawa vidonge 70, kwa siku niwe nakuywa kumi kwa siku 7 halafu nikimaliza nirudi tena kuendelea na matibabu yaani asubuhi nakunywa vidonge 4, mchana 2 na usiku 4.. nilichukua zile dawa, ilipofika wakati wa malipo wakania shilingi elfu 62 na shilingi elfu moja ya kumuona daktari, jumla 63,000.. dah roho iliniuma kuzitoa zile pesa bila kitu cha maana nilichofanyiwa,, zaidi ya utapeli... niliondoka nilipofika nje dawa nikaziweka kwenye ndoo la taka, sasa cha kushangaza wale wachina wakiandikisha jina wanataka mpaka namba ya simu.. niliandika namba yangu ya simu, na baada ya siku saba walinipigia eti wananiambia nirudi kwa ajili ya matibabu tena.. nikawaambia sipo mjini nipo sehemu nyingine nimesafiri... wakaanza kunipiga mkwara eti n isipotibiwa vizuri nitakufa ule ugonjwa utaenda mpaka kichwani nitakufa...

kumbe walikua longolongo tu nilipoenda Hospital za kawaida tena za kibongo nikaambiwa ni mchafuko wa damu na figo zina uchafu nikaandikiwa vidonge, siku mbili tu yale mauvimbe yakaanza kutoweka na nikapona kabisa...
Serikali iwe inawachunguza hawa wachumia tumbo Smile pole sana
 
duh!kweli globaliziton.kwamba unaweka mkono tu kwa dakika mbili halafu unafumbuliwa matatizo ya ndani,,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…