ppole sana mdada nenda ocean road kacheki kansa ya titi aisee..
Habari
Nina tatizo la matiti {yote mawili} kuhisi yamekuwa mazito na yanauma kwa kuvuta na kuacha..nikivua braa nahisi yanadondoka kwa maumivu ninayopata. Nilidhani ni kawaida ila mbona hayaponi...ni tatizo au ni mfumo tu wa hormones umebadilika pia nikiminya minya nahis maumivu na wakati wa kuoga shurti nioge kwa adabu nikigusa vibaya naweza hata kulia.
Ushauri tafadhali
NB: Siku ya 4 sasa
Sina ujauzito na wala sipo kwenye ovulation
Mzunguko wangu ni mrefu wa siku 30
Asante mkuu,kwanini mpaka pm,tufanye hapa kwa faida ya wengine pia
Usijali shemeji...
ukiwa huna pesa warembo wote wamjini utawaita shemeji.hahahahaha am jst kidin lakini.
kwa upande wa Chocs me nadhani angeenda kwa Dr kupata ushauri wa uhakika zaidi maana hii miili ya kike ni very complicated unaweza dhania hivi kumbe kuna tatizo linazidi kudevelop tu
I do appreciate your good intentions and thank you so much for your concerns md4doctor2000 Marnah mtoto matataa kabanga Malafyale kumbe wataka tuskypike,wewe ni daktari? coz mficha maradhi kifo humuumbua
Nimemwona daktar leo,ameyatizama na tukaongea kirefu kuhusu mzunguko wangu wa hedhi, jibu ni kwamba this is hormonal imbalance, so nimepewa dawa za kupunguza maumivu pia nimeambiwa nisibane sana matiti (nisivae bra au nivae ambazo ni loose kidogo but muda mwingi niyaache huru) wala nisiyaminye minye na nijitahidi kula mlo kamili....Nawashukuru sana
Lazima ayaone jamani ili ajue shida ni nini