Matokeo ya form four 2008


kwa nini wengi wetu tumekuwa tunaongelea mambo ya makabila sana unakutana na mtu atkulizawewe eti ni kabila gani hususan wasichana hii inatokana na nini kwa nini au kuna nini ndani yake
 
Kinachoniboa na hayo matokeo ni kutokuandika majina halisi ya watahiniwa badala yake wametumia namba za mtihani. What is so special about namba za mtihani? Wanalinda privacy ya nani?

Itawasaidia sana wazazi na sisi tuliombali tunaowasomesha ndugu huko tufahamu matokeo. Hapa nilishadanganywa namba ya mtihani ya mtu aliyepata Div 1 huku najua fika huyo mtoto hana uwezo wa kupata Div 1 na nimeshathidbitishiwa hivyo kuwa amepata 0.

Warudi kuandika majina kama walivyokuwa wakifanya siku zote.
 
Kinachoniboa na hayo matokeo ni kutokuandika majina halisi ya watahiniwa badala yake wametumia namba za mtihani. What is so special about namba za mtihani? Wanalinda privacy ya nani?
Wabongo bwana....wewe mbona hutumii jina lako halisi?
Unalinda privacy ya nani?
 
Haya sasa nini, ugomvi huo!

Mimi simo...
"Tatizo CCM....." Wazenji hawawezi kufeli namna hii kila mwaka....yaani wenyewe ni kusema hawana akili? hapana......tatizo ni CCM....

Seif for president.......
 
Wabongo bwana....wewe mbona hutumii jina lako halisi?
Unalinda privacy ya nani?

Yo Yo wewe ni soo!

Yaani nimecheka sina hamu!

Ama kweli bongo kila mtu ana zake!

On a serious note, nadhani baraza halijakosea..kuweka namba ni vyema. Kama una mtoto wako au ndugu yako ni swala la kumwambia akupe namba tuu. Mengine yatajiset. JAMANI, kama alivyoainisha mkuu hapa Yo Yo..kila mtu anapenda privacy yake ilindwe.. so is here kwenye board. Tusiwaonee hawa watoto. Put yourself in their shoes...hivi kweli leo hata kama unafanya masters UK au US..ungependa matokeo yako ya semister yatundikwe kila mtu aone? Think about it! Sana sana hapa tunataka majina kusudi tuanze kuchambua personalities..mtoto wa fulani nk...Which I think is not good.

Ni mtizamo tuu
 
Ukija Ufisadi wachaga wanashambuliwa wao ndio masteering

Likija suala la watu wenye nyazifa mbali mbali wachaga wanaitwa wakabila na kupendeleana.

Likija Suala la kilimanjaro kutoa warembo wengi wanaambiwa walitoa rushwa ya ngono.

Linapokuja suala la kuoana wanaambiwa wao ni wabaguzi hawataki makabila mengine

Likija shule za kilimanjaro kufanya vizuri....

Ni lini tutaacha kuongelea wachaga????

Je, hatuoni kwa kuwaongelea kila wakati ndio tuna wapa umaarufu na pia tunawaongezea comfidence ya kufanya mambo makubwa zaidi?????? we are creating superiority and inferiority complex)
 
Ila aise kwa haya matokeo..tunahitaji kufanya kazi ya ziada.

Duh..harafu mmeangalia zile centre za private? ambako watu wanafanya mtihani wakiwa uraiani kama kujiendeleza? yaani watu wamefeli vibaya mno! Na hao ndo unakuta ni walimu wanafundisha shule kibao za hapa TANZANIA. Now, kama mwalimu kafeli..ataweza kufaulisha wengine?

Masomo ya sayansi yanakwammisha wengi sana. I hope we can do something to aleviate this looming disaster. Harafu wanaoumia zaidi ni watoto wa wakulima, maana wanasoma vijijini na huko hakuna walimu wa kutosha.
 
Wakuu,
Mimi naomba kufahamishwa kitu kimoja hapa... hawa jamaa zetu wanaweza vipi kutaja mkoa fulani kuongoza/kushika mkia ikiwa kila mkoa una idadi tofauti ya shule na wanafunzi wake?..

Mathalan. tuseme mkoa wa Kilimanjaro una shule za secondari 30 na mkoa wa Pwani una 3 tu lakini katika matokeo Pwani shule moja imechukua mshindi wa pili na zile nyingine hazipo ktk idadi ya 20 za juu lakini pia hazipo ktk idadi ya shule za chini kabisa.. iweje izidiwe na Kilimanjaro yenye shule 30 na kati yake 6 zimechukua nafasi ya shule bora 20..(mind U huu ni mfano tu)....
Kwa maana hii nashindwa kuelewa pale tunapochukua idadi ya shule ktk top 20 toka mkoa fulani na kuupa ushindi wakati mkoa mwingine hauna idadi sawa ya shule na wanafunzi..

Mimi nadhani ingekuwa bora sana watumie hizo asilimia kulingana na idadi ya shule au wanafunzi wenyewe mashuleni. Kwa mfano Mkoa wa Dar yenye shule za sekondari 40 wamekaa mtihani wanafunzi 40,000 na walioshinda ni 20,000 ipewe asilimia yake na Mkoa wa Shinyanga wenye shule za sekondari 10, wanafunzi waliokaa mtihani ni 10,000 walioshinda ni 7,000 ichukuliwe kuwa mkoa wa Shinyanga umechukua nafasi ya juu kuliko Dar kwa sababu ya asilimia kubwa ya wanafunzi walioshinda kulingana na shule na wanafunzi wake..

Nadhani hata ktk Utajiri na Umaskini wa nchi hupimwa kutokana na pato la Taifa against idadi ya watu wake kuliko kutazama namba ya watu au pato peke yake..Hivyo inaturahisishia kufahamu ni mkoa gani unahitaji sana kuboreshwa elimu iwe ni kutokana na vifaa, walimu au fedha kwa sababu kutajwa kwa shule moja kuwa juu/chini ya daraja haitupi picha kamili ya elimu mkoa mzima..

Haya ni mawazo yangu tu sijui kama nimekosea!
 
Kwani hao watoto wanaosoma kwenye hizo shule za mkoa kwa Kilimanjaro wanatoka Kilimanjaro pekee? As far as I know wanatoka sehemu yeyote ya Tanzania as long as wamekidhi qualification na kupata nafasi ya kusoma kwenye shule hizo.
 
Hivi hayo makabila yameandikwa wapi ktk report hiyo hapo juu!... au uzee tena maanake mimi sijaona kitu hiyo!
 
Tatizo la Zenj,elimu na dini viko mutually exclusive.

Tukirudi kwenye somo la hesabu kwa ujumla.Ingawa ubora wa walimu unachangia,mzizi wa tatizo uko kwenye preconceived notions kuwa Maths ni ngumu.Mtoto wa miaka 12 anakwambia,''I am not a Maths person'' au ''Maths ni genetic disorder kwenye ukoo wetu''.Huyu hata apewe mwalimu wa aina gani,hesabu itakuwa mbinde.Hata hivyo,katika baadhi ya shule ambazo wanahimiza (if not force) wanafunzi wao kujifikiria as Maths oriented students...speaking for myself,St.Francis and Marian Girls,sio kwamba wote wanaosoma huko hawana imani za ''ugonjwa wa hesabu'',ila system inawasaidia kutambua kuwa imani hizo hazina mashiko na kuwapa nafasi ya kuprove it so.Je hii inawezekana katika shule nyingine pia?Without doubt.

Vitengo vya elimu aside,majumbani mwetu-wazazi,makaka na madada tuache tabia ya kuendekeza imani za kutoweza hesabu kwa wanafamilia wenu.Utakuta mzazi anawaka moto ukifeli Biology,Chemistry au English,ikija kwenye hesabu unasikia,''Oh well,Maths jitahidi tahidi''.And that's it!Wrong!Every student should be able to perfom well in Maths as in any other subject.And don't give me one of those,''Aaa bwana,unajua watu wamejaliwa vipaji tofauti''.I'll tell you what vipaji tofauti means....a 98 in Chemistry and an 85 in Maths.Not average enough?Then a 75 in History and a 68 in Maths.Au ufeli masomo yote kabisa on average tujue kweli hii special needs.Vinginevyo,tunajipotezea tu competent human resource kwa kuendeleza vijidesturi vya kipuuzi.
 
Last edited:

Couldn't have been said any better.
 



Duu asante sana mkuu nashukuru sana tena sana....Maana nilikuwa nasumbua kichwa nifanye nini maana shule nyingi alafu sina jinsi asante sana mkuu kwa utaalaam wako mzuri!!
 


Kwa sababu zina facilities bora kuliko shule nyengine nyingi, mfano walimu bora, maabara, vitabu nk.
The Roman catholic institutions nyingi zikiwemo shule hapa duniani huwa zinaendelezwa na kupata backup fundings kutoka RC na ndio ukaona wanaweza kumiliki kutoa best Education na kuajiri walimu bora, na hii sio kwa Bongo tu hadi Ulaya na Marekani RC faith schools ziko juu pengine nyuma ya Jewish schools tu ambazo ndio ziko top zaidi.
 
....matokeo hayana tofauti na kazi waliyofanya hao waliotengeneza website, website gani huwezi hata navigate,huwezi hata kutafuta jina la shule mpaka ufinye macho juu chini juu chini...yaani unaweza kutumia saa nzima kutafuta unachotafuta,huu ulipuaji wa kazi sijui utaisha lini,ni aibu kubwa kwa watu wanaosimamia elimu kama NECTA kuwa website mbovu kama hii,next year tafadhari msionyeshe watu hii aibu!
 
"Tatizo CCM....." Wazenji hawawezi kufeli namna hii kila mwaka....yaani wenyewe ni kusema hawana akili? hapana......tatizo ni CCM....

Seif for president.......

Mkuu Yo Yo
Hapa unatukumbusha au?
 

Hamna pesa za kigeni!
 
sasa na wengine vuteni soksi mfanye vizuri kama Kilimanjaro...acheni kupiga piga kelele!

Facts speak for themselves!
 
Last edited:
Kuna haja ya kuwakutanisha Walimu wa sekondari toka Kilimanjaro na mikoa mingine ili wale wa Kilimanjaro wawaambie walimu wa kutoka mikoa mingine siri kubwa ya mafanikio yao ili nao wajaribu katika mikoa waliyomo ili kupata matokeo ya juu kama Kilimanjaro. Hongera Walimu na wanafunzi wa Kilimanjaro mafanikio mliyoyapata hayaanguki toka mbinguni bali yanatokana ni kujituma kwenu na kuthamini umuhimu wa elimu katika dunia ya leo.
 

Mh..!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…