tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 24,225
- 22,632
Kuna taarifa za siri na kiintelijensia zinazobainisha kwamba matokeo ya Mitihani ya kuhitimu Kidato cha Sita (ACSEE) yamepikwa kisiasa. Inadaiwa kwamba matokeo hayo yalichakachuliwa (standardized) mara 3 na kikosikazi kilichopewa majukumu ya 'kuyaboresha' kabla ya Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kuyatangaza hadharani.
Habari zinabainisha kwamba baada ya matokeo ya kwanza kutoka, ambayo yalikuwa mabaya sana, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dr Shukuru Kawambwa, aliunda timu ya watu 6 ili 'kuboresha' matokeo hayo. Timu hiyo ilijumuisha watu wawili kutoka NECTA, watatu kutoka Wizara ya Elimu, na mtaalamu mwelekezi kutoka Kitivo cha Elimu cha Chuo Kikuu cha Dar es laam, kampasi ya Mlimani.
Inaelezwa kwamba lengo kubwa la 'kuboresha' matokeo ni kuwavisha wazazi kilemba cha ukoka, hasa baada ya serikali kushindwa kuboresha kiwango cha elimu kwa vitendo. Ni matokeo yanayolenga kuwafurahisha wazazi na kuwafanya waamini kwamba kiwango cha elimu nchini kimepanda. Hii ni hatari kuliko maelezo!
:israel:
Habari zinabainisha kwamba baada ya matokeo ya kwanza kutoka, ambayo yalikuwa mabaya sana, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dr Shukuru Kawambwa, aliunda timu ya watu 6 ili 'kuboresha' matokeo hayo. Timu hiyo ilijumuisha watu wawili kutoka NECTA, watatu kutoka Wizara ya Elimu, na mtaalamu mwelekezi kutoka Kitivo cha Elimu cha Chuo Kikuu cha Dar es laam, kampasi ya Mlimani.
Inaelezwa kwamba lengo kubwa la 'kuboresha' matokeo ni kuwavisha wazazi kilemba cha ukoka, hasa baada ya serikali kushindwa kuboresha kiwango cha elimu kwa vitendo. Ni matokeo yanayolenga kuwafurahisha wazazi na kuwafanya waamini kwamba kiwango cha elimu nchini kimepanda. Hii ni hatari kuliko maelezo!
:israel: