Matokeo ya shule iliyoongoza kitaifa darasa la 7! Ndiyo imeshinda! Lakini?

Matokeo ya shule iliyoongoza kitaifa darasa la 7! Ndiyo imeshinda! Lakini?

Judgement

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2011
Posts
10,326
Reaction score
4,785
Neno "mysterious" kwangu mie ktk issue kama hizi ndipo huchukua maada .
Distrust or lack of sureness of an alleged fact haiepukiki katika maumbile yetu binadamu .

Hebu fuatana nami mguu kwa mguu tuperuzi mafanikio ya shule husika 2014.

Twibhoki primary school , inayopatikana wilaya ya Serengeti mkoani Mara .
Shule inayokwenda na nambari ya usajili P-0904095 .

Jumla ya candidate waliyofanya mtihani mwaka 2014 ni 33 .
Kiwilaya imekua ya 1 kati ya shule 105 .
Kimkoa imekua ya 1 kati ya shule 723 .
Kitaifa imekua ya 1 kati ya shule 15867 .

Wanafunzi wote 33 wamepiga alama "A" katika kila somo .
Masomo ni matano yaliyofanyiwa mtihani .
Hivyo kila candidate amejilambia "A" zake 5 .
Hivyo kufanya 33 x 5 = 165 .
Alama "A" 165 zimezalishwa .

Na upande wa position ya Average grade napo wote wamejipigia grade "A" , na kuzalisha jumla ya grade "A" 33 .

My doubt , nashindwa kutopata kigugumizi cha kuamini pasiwepo walau hata candidate mmoja aliyepata alama "B" au "C" aidha katika Subjects au katika Grade position .

Wadau wa bodi JF Nini mtazamo wenu katika hili ?
 
Inawezekana walikuwa wanafanya mchujo mkali sana wakabakiwa na cream tu...au imetokea tu by chance
 
Inawezekana walikuwa wanafanya mchujo mkali sana wakabakiwa na cream tu...au imetokea tu by
chance
Kama kweli kilifanyika kitu ukisemacho Khantwe basi wamestahili !
But unachoniambia kinanizalishia another quiz , mathalan kama uchujaji wa style hii unawezekana vipi wauanze mwaka huu ?
Vipi shule nyingine zishindwe ? Wakati huo sio uchawi !
 
Last edited by a moderator:
Tatizo ni shule kutokea mkoa wa mara au tatizo ni nin?maana ingekua ni shule kutoka dar au kilimanjaro sidhan kama ungekuja kuhoji humu.

Perry !
Kua na mawazo huru!
Hapa tunadiscus Elimu , agenda hapa si Ukanda, Ukabila , Udini , Usiasa n.k
Issue ya Kilimanjaro sijui Dar si mada yangu hapa ni Kitanzania.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo ni shule kutokea mkoa wa mara au tatizo ni nin?maana ingekua ni shule kutoka dar au kilimanjaro sidhan kama ungekuja kuhoji humu.
Hahahaa kweli mkuu huyu jamaa anachukulia mkoa wa Mara ni vilaza hawawez kuyafanya haya??
 
Hahahaa kweli mkuu huyu jamaa anachukulia mkoa wa Mara ni vilaza hawawez kuyafanya haya??
Engineer
comments zako haiendani na username yako!
Mkoa uliyotoa viongozi waandamizi wa nchi hii , then uwe mkoa wa vilaza ?
Rais wa kwanza Tz, Pm na vice president mstaafu, gavana wa B.O.T mstaafu, Mkuu wa JWTZ mstaafu wanatoka Mara, hata Currently AG anatoka Mara!
Haya mawazo ya vilaza ni yako na si ktk agenda yangu!
 
Last edited by a moderator:
Engineer
comments zako haiendani na username yako!
Mkoa uliyotoa viongozi waandamizi wa nchi hii , then uwe mkoa wa vilaza ?
Rais wa kwanza Tz, Pm na vice president mstaafu, gavana wa B.O.T mstaafu, Mkuu wa JWTZ mstaafu wanatoka Mara, hata Currently AG anatoka Mara!
Haya mawazo ya vilaza ni yako na si ktk agenda yangu!
Ww ndo hujielewi mbona miaka mingine mikoa mingine ikiongoza huulizi upuuzi kama huu Mara kuongoza ndo uje na hoja ya kipuuzi hapa
 
uchunguzi ufanyike kama maswali waliyokosa ni ya aina moja hapo ndio matatizo yataanzia ila kama wamekosa maswali tofauti haina shida
ikitokea wamekosa ya aina moja wafutiwe matokeo
 
Katika taaluma hili linawezekana ikiwa vijana wameandaliwa vyema mentally na kisaikolojia unless otherwise kuwe kuna ujanja ujanja maana kuna kasumba nilipata kuisikia ya wenye shule kununua mitihani ama wakuu wa shule kuvujisha mitihani ili kuipa shule remark nzuri kwa manufaa ya kibiashara!
 
Ww ndo hujielewi mbona miaka mingine mikoa mingine ikiongoza huulizi upuuzi kama huu Mara kuongoza ndo uje na hoja ya kipuuzi hapa

When arguin with fools , don't answer their foolish arguments!
Otherwise you will become as foolish as they are !
It's difficult to free fools frm the chains they revere!
Mjadala unajadili maharage wewe unajadili dengu!
Mimi nilikua nadhani viazi kama nyinyi humu mmekwisha kumbe bado mmo!
 
When arguin with fools , don't answer their foolish arguments!
Otherwise you will become as foolish as they are !
It's difficult to free fools frm the chains they revere!
Mjadala unajadili maharage wewe unajadili dengu!
Mimi nilikua nadhani viazi kama nyinyi humu mmekwisha kumbe bado mmo!
We ongea hata kijerumani ila ktk wajinga ww ni wa kwanza....
 
KWANI HII SHULE ILIKUWA YA NGAPI MWAKA JANA. Au ni miujiza ya mwaka huu tu??!! Na waalimu ni wale wale au wamehamia wengine labda.?? Haya ndio mambo ya kujiuliza
 
  • Thanks
Reactions: bdo
Kaka hoja ni kuangalia matokeo ya darasa hili kwa vichachawizo vinavyotumika kimataifa kutathimini matokeo ya watahiniwa. Dhana moja ni Normal Distribution Curve. Katika model hii inasadikika kuwa katika kila kundi la watahiniwa patakuwa na 10-15% ya watu wanye akili sana (above average) 70-75% wenye akili za wastani 15-20% wenye akili hafifu yaani chini ya wastani. Kama mtihani umetungwa vizuri na darasa ni la kawaida tunatarajia wanafunzi wengi zaidi watapata alama za wastani. Ni nadra sana darasa zima kupata A au kupata F.
Huu ndiyo msingi wa mashaka haya, haijalishi shule ingalikuwa iko Dar, Moshi au Mbeya. Kuna nadharia kuwa inawezekana kulikuwa na mchujo wa mara kwa mara kwa wanafunzi kabla ya mtihani hivyo 85% ya wanafunzi wenye uwezo wa wastani na hafifu walifukuzwa shule kabla ya mtihani, Inawezekana wanafunzi walikaririshwa majibu, inawezekana ufundishaji ulikuwa mzuri kutokana na kuwa na idadi ndogo ya wanafunzi katika darasa, inawezekana walisaidiwa kwa kupewa majibu na walimu wao.
Ili utoke na jibu sahihi ni lazima ufanye utafiti wa kisayansi utakao kuja na jibu sahihi na kureject hypothesis zingine zote.
Ni muhimu pia kuangalia matokeo ya maendeleo ya shule hii tokea miaka ya nyuma. Wanafunzi wamekua wakifauluje. Kama shule hii miaka ya nyuma imepata kuwa kati ya shule kumi bora, ikashika nafasi ya tano, ya tatu halafu ikawa ya kwanza. Tatizo halipo. Kama mazingira ya kusomea kwa maana ya majengo, walimu, zana za kufundishia, vitabu vipo kwa nini wasishike nafasi ya kwanza huku wakishindanishwa na shule zisizo na walimu, hazina vifaa wala vitabu?
Perry !
Kua na mawazo huru!
Hapa tunadiscus Elimu , agenda hapa si Ukanda, Ukabila , Udini , Usiasa n.k
Issue ya Kilimanjaro sijui Dar si mada yangu hapa ni Kitanzania.
 
We ongea hata kijerumani ila ktk wajinga ww ni wa kwanza....

If a wiseman has an argument with a fool one , the fools only rages and laughs , and there is no quiet!
Kama kisw kimekuvuruga basi lugha zingine zitakupeleka clinic.
 
If a wiseman has an argument with a fool one , the fools only rages and laughs , and there is no quiet!
Kama kisw kimekuvuruga basi lugha zingine zitakupeleka clinic.
Jifunze kuandika kingereza mkuu naona ushamaliza ka-english course ka miezi mitatu
 
Back
Top Bottom