Nziku,
Ninachokipinga mimi ni CUF, Chadema,TLP,UDP,NCCR-Mageuzi, DP nk kuungana. Hii ni kujidanganya! pia ni kuweka rehani nchi yetu. Mkuu wangu, kweli unawajua vizuri hawa jamaa? mimi ninaamini kabisa kuwa ume-base kwenye dhana zaidi kuliko uhalisia. Kwangu mimi dhana ya kuwa na chama mbadala ina-sound kuliko hivi vyama kuungana.
Mkuu wangu soma vizuri maelezo yako mwenyewe utaona kwamba tatizo sio chama isipokuwa ni WATU..Je, ni wakati gani tunaweza kuamini watu ama viongozi wetu ktk chama chochote kile kitakachoweza kuundwa ili kifikie kuwa mbadala!..Ikiwa leo hii wewe na mimi hapa tunashindwa kuwaamini kina Dr. Slaa, au Lipumba na wao kati yao wanashindwa kuaminiana iweje iwe rahisi kusimamisha chama mbadala... kumbuka maneno ya FMES kuwa viongozi wetu ni reflection yetu!..sisi wote tunapendana Kichina tu tusidanganyane hapa...Unless kama tunaweza kuviua kabisa vyama hivi vyote yaani Chadema kife, CUF ife, TLP ife na kisha kipatikane chama kingine ambacho sijui kitakuja na sera au hoja zipi tofauti na vyama hivi vilivyotangulia.
Nitarudia kusema kuwa Chadema sio Mbowe wala Dr. Slaa, CUF sio chama cha Lipumba, Sief au sijui nani, vile vile TLP sio Mrema na kadhalika..
Tatizo letu kubwa ni kuendelea kujenga imani hizo na kuabudu kisiasa kuwa hawa ndio miungu au wajenzi wa vyama hivyo. Na kibaya zaidi ni kwamba hata maamuzi yote nje ya Policies za vyama hivi hutolewa na watu hawa hawa hata kama zinahusu personal issues zao.. vijembe na vituko vyote vimejengwa na kundi la watu wachache sana kupindisha ukweli ambao ni muhimu sana kwa maslahi ya Taifa...I believe kuwa wanachama wengi wa vyama hivi wana imani zaidi ya muungano ktk kupata ushindi kuliko viongozi ambao wana personal issues within..Ebu nipe sababu ya msingi hasa ktk kuvunjika kwa muungano wa awali kati ya CUF na Chadema!..
Hivyo, kwa nini tunazidi kufikiria kuwa TLP haitaki kuungana na Chadema wakati asiyetaka kuungana ni Mrema na kundi lake..Kwa nini tuamini kwamba CUF hawataki kuungana kwa sababu kasema Lipumba, hali kadhalika Mbowe na Mbatia kwa vyama vyao..Je, sisi sote tunawajua vizuri watu hawa!...jibu lake, hatuwajui hata wale wanaotuongoza leo kina Kikwete hatuwajui!..
Kama unakumbuka Kikwete aliwahi kutishia kujiunga na Chadema kama CCM isingemsimamisha, leo hii ni rais wa Jamhuri kwa tiketi ya CCM!..huyu mtu anaamini mrengo gani? au CCM wanamchagua kiongozi kwa malengo gani!..Kabourou alitoka Chadema yuko CCM na ukiuliza sababu utaambiwa ni mtu fulani sio chama na hakika problem ni yeye mwenyewe -MTU sio chama Chadema..Hivyo chama mbadala hakiwezi kupatikana ikiwa sisi tunashindwa kuelewa tatizo la siasa zetu ni kitu gani - WATU.
Let's do what is possible leo ya kesho yatafuata. Kuanzisha chama kipya kabisa from no where ni ndoto ya mwendawazimu kwa sababu mazingira yetu - chama ni WATU na hatuna watu hao isipokuwa kundi dogo ambalo tayari limekwisha jitoa mhanga..Nina hakika tukisha mwondoa CCM na utawala wake unaofuata watu, then huko mbele ndiko tunaweza kujenga vyama mbadala vinavyotetea maslahi ya wananchi..