Elections 2010 Matokeo ya uraisi....

Nimewasikitikia Singida mjini...wamempa jk 19,000 dhidi ya 5,000 za daktari wa ukweli..

kinachokusikitisha ni nini?si kila mtu ana haki ya kidemokrasia kumchagua kiongozi anayemtaka?mbona mnapenda kuingilia uhuru wa kidemokrasia wa wenzenu!
mbona watu mnalalamika sana nchi mtaiweza kweli mkipewa?
 
utayapata... chakachua inendelea, maana JK bado yuko ikulu, badala ya kuhamia kwake hadi majibu yatoke
 
wasije wakawa katika mchakato wa uchakachuaji maana kwenye ubunge ngoma imekuwa ngumu kuchakachua

ndio tunakoelekea mkuu ...slaa na timu yake kokote uliko ...kwa nini matokeo ya urais hayaji?????.....kama itv wamepiga stop yabandikeni hapa....hakuna mtu mwenye link itv tupenyezewe matokeo hapa!!!.....tunaibiwa !!!.tunaibiwa!!!....kokote mlipo wakiwemo wazalendo wa usalama leteni taarifa!!
 
hoja iliyo mbele yetu haijajibiwa, urais vp
 

Acha hizo kaka. Unaupotosha umati tu hapa. Mshindi akiwa Chadema matokeo halali, akishinda CCM yamechakachuliwa. Ebu tuwe na ukomavu na tuache demokrasia ichukue mkondo wake. So far Upinzani una viti 20, which is good. Ukichanganya na Zanzibar, bunge la jamhuri lijalo litakuwa la ukweli. Tusubiri tu hayo ya Uraisi na tuwe tayari kuyakubali. Either way.
 
People contol your excitement!
Otherwise CCM might be doing wonders underground
 

vipi bado mnategemea apate asilimia 88%%.....kumbuka hata dr slaa akipata 45%...ni hatua kubwa ....!!!.....lakini mmeona wenyewe maeneo mengi slaa ameongoza .....tunasubiri .....ccm wachakachue ili kupata turn out ya 20 million waliyoahidi labda ndo atapata 70%% bati haki bin haki ameanguka na pua!!
 

maneno ya wakosaji hayo....
 

Kumbe hata wewe ni adui wa maendeleo(ukombozi)
 

sele hatujali kama dr anashind au hashindi ...tunalalamika kwa nini matokeo ya urais yamesitishwa kutangazwa live....tunatangaziwa ya ubunge tu ...hii italeta tension bure alafu askari waingile kujifanya wanazima vurugu...tunataka amani!!
 
Jamani SLAA anachukua nchi kwa mtu mwenye akili anaweza kuelewa ninachoongea, yaani pale ambapo JK kampita SLAA, kampita kwa tofauti ya kura chache sana, na pale ambapo SLAA kampita JK kampita mara mbili au hata mara tatu, mwenye kubisha abishe tu lakini ukweli ndo huo!! so ukicombine utaona yale ma-gap yanazibwa kwa urahisi sana na SLAA na hivyo kupaa zaidi
 
Jamani eeeh matokeo ya uraisi vipi? Mbona hakuna anayeyazungumzia? Maana kila mtu kajikita kwenye ubunge...kwa nini ya uraisi hayazungumziwi wala kutolewa?

I am curbing my enthusiasm.
 

Ngumu kumeza ila inabidi tu, sasa ufanyaje?
 

akuibie nani wewe jamani?
wanavyokuibia mkeo nyumbani ndio unaona kila kitu unaibiwa tu!
 
Jamani eeeh matokeo ya uraisi vipi? Mbona hakuna anayeyazungumzia? Maana kila mtu kajikita kwenye ubunge...kwa nini ya uraisi hayazungumziwi wala kutolewa?

Fingers crossed🙂) Dr. sijui atapita, inshallah!!
 

Source mkuu!!
 
Singida ukame upo..so mmeona alama ya kijani mkanadhani neema imepotea njia..ole wenu..mtapigwa mnada mnajiona hivi hivi!
 
sele hatujali kama dr anashind au hashindi ...tunalalamika kwa nini matokeo ya urais yamesitishwa kutangazwa live....tunatangaziwa ya ubunge tu ...hii italeta tension bure alafu askari waingile kujifanya wanazima vurugu...tunataka amani!!

kinachokuwasha na kukuumiza ni hii hali ya amani iliyopo tz unatamani wewe askari wafanye fujo na amani itoweke huna lolote!
wazowea nazi samli hawaiwezi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…