Matrafiki wa Mwenge ndio wanaosababisha foleni, bora waache taa ziongoze

Matrafiki wa Mwenge ndio wanaosababisha foleni, bora waache taa ziongoze

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Kuna muda huwa sipendi kupita katika njia ya pale Mwenge kwenye Jiji letu la Dar es Salaam hasa majira ya jioni, maana wale trafiki wanaoongoza magari mitaa hiyo ni wazinguaji hasa.

Kwa ufupi wao ndio wanaosababisha foleni iwe kubwa, bora wangeacha taa zifanye kazi, wanazingua sana.

Ikifika jioni, sijui huwa ndio wanataka waonekane wanafanya kazi au vipi, mfano nimefanya research isiyo rasmi ndani ya wiki mbili, kuna muda wanauweka upande mmoja kwenye break na kuruhusu upande mwingine kwa dakika 15

Hivi unapowasubirisha watu kwenye foleni kwa dakika 15 wakati upande wa pili wanapotakiwa kwenda hakuna foleni wala hakuna msongamano wowote, unategemea nini?

Sijui huwa wanapigiwa simu na watu wao kuwa upitishe upande huu ili wapiti fasta, nina hasira sana na trafiki wa kibongo, ukiachana na mambo ya ‘kutupiga’ sisi tunaoendesha vyombo vya moto, hili la pili nalo ni jibu

Naomba Serikali iangalie jinsi ya kufanya kuhusu usumbufu huu wa matrafiki kuwa sababu ya foleni
 
simlishakubaliana kwamba wanatafuta za kubrashi viatu ama! vumilia tu ndio nchi yenyewe hiyo, na majamaa yamenenepa mpaka masikio kwa sababu ya rushwa.
 
Kuwa na akili traffic wanavuta upande wenye magari mengi haiwezekan upande wako unamagari 7 wavute dakika sawa na magari yanayotok mjin ambapo kuna magari 10000, mjini traffic akidelay kidog tu foleni itaanza mwenge hadi posta

Note taa zikivuta kwa dk 2 kila upande inasababisha foleni kuongezek upande mmoja ambao magari yanakuja kwa wingi kama njia ya mjin
 
vivuko via ubungo vilipo jengwa tulidhani mwa 40 wa foledi dar umeisha kumbe sio kweli

ukweli hua hapa magali yanyo toka buguluni yakelekea mwenge yakisha vuka yanapeleka foleni kuanzia mawasiliano

yanayo toka mbezi kwenda kariakoo yanapeleka foreni kuanzia shekilango

mwa 4 ni kujenga kivuko magomeni moroco mwenge
 
Kuwa na akili traffic wanavuta upande wenye magari mengi haiwezekan upande wako unamagari 7 wavute dakika sawa na magari yanayotok mjin ambapo kuna magari 10000, mjini traffic akidelay kidog tu foleni itaanza mwenge hadi posta

Note taa zikivuta kwa dk 2 kila upande inasababisha foleni kuongezek upande mmoja ambao magari yanakuja kwa wingi kama njia ya mjin
Umemjibu kwa akili sana

Mfano kutokea posta kwenda tegeta Jion hiyo njia ina magari mengi kuliko

Kutokea mawasiliano kwenda tegeta

Hvyo bhac gari zinazotoka posta lazima zipewe kipaumbele

Afu kingine tukiacha taa ziongoze kwa muda wa jioni au asubuh automatically tutasababisha foleni sehemu zingine
 
Kuna muda huwa sipendi kupita katika njia ya pale Mwenge kwenye Jiji letu la Dar es Salaam hasa majira ya jioni, maana wale trafiki wanaoongoza magari mitaa hiyo ni wazinguaji hasa...
Acha lawama mkuu, trafk huwa hawaruhusu tu kiholela, isipokuwa huwa wanawasiliana na maeneo mengine kujua hali ya foleni ipoje, wewe huwezi kujua kwa sababu moyo wako umejaa kisirani. Nikupe mfano mwenge - posta huwa kuna mawasiliano kujua hali ya foleni ipoje maeneo ya kati kati kwa sababu kuna makutano ya njia kubwa mfano morocco ili waweze kucontol floo ya magari kwenye maeneo mengine, wakiruhusu kiholela kama unavyotaka wewe watasababisha foleni kwenye maeneo mengine, pengine hata uelekeo wako washapata taarifa njia imeziba so ni lazime wafungue upande mwingine ili flow ya magari isiathiri pande zote. Ndo maana sometimes anaweza kuruhusu hata kwa dakika 30 na usione jam huko yanakoenda, hiyo ni kwa sababu wenzako wana taarifa ya barabara yote toka mjini mpaka Bagamoyo kwa sababu kila baada ya umbali fulani wana mtu wao ambaye anawapa updates zote. Tatizo mnakazaga shingo tu lkn hata wewe unaweza kumuuliza trafk na akakupa update ya barabara yote na pengine kukushauri ili ukwepe foleni upite wapi.

Wabongo punguzen lawama, hivi kwa mfano morocco au hapo mwenge asipokaa askar jioni au asubuhi si itakuwa vurugu kila mtu anataka kuwahi mwisho wa siku inatokea ajari mnazidi kuchoma mahindi hapo hapo, unapowaona wanaongea na zile simu zao usidhani wale ni customer care wa sport pesa wanajadili mikeka na wateja waliobeti halaf hawaamini kama wameliwa.
 
Kuwa na akili traffic wanavuta upande wenye magari mengi haiwezekan upande wako unamagari 7 wavute dakika sawa na magari yanayotok mjin ambapo kuna magari 10000, mjini traffic akidelay kidog tu foleni itaanza mwenge hadi posta

Note taa zikivuta kwa dk 2 kila upande inasababisha foleni kuongezek upande mmoja ambao magari yanakuja kwa wingi kama njia ya mjin
Sio kweli yawezekana hata madai ya mwandishi hujayaelewa vizuri lakini pia inaonekana wewe ni abiria ukiendesha gari utamuelewa vizuri mtoa mada.

Naongezea hili la kuongoza manually wakati taa zinawaka na zinapokuwa zimezimika kwa kukatika umeme au itilafu nyingine trafiki hao hukaa pembeni na kuwaachia wenye magari kumanoeuvre kivyao vyao!
 
Back
Top Bottom