Matukio Halisi Yanayothibitisha Uchawi – Utashangaa!

Matukio Halisi Yanayothibitisha Uchawi – Utashangaa!

Davidmmarista

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2024
Posts
1,367
Reaction score
2,451
It's another beautiful day, another beautiful thread!

Mimi ni Davidmmarista, na leo tunakuja na Uzi mzito wa kutikisa akili! Uchawi upo ama ni hadithi tu? Leo tunachambua matukio halisi 12 yaliyothibitisha uwepo wa uchawi, hasa kwa wale ambao walikuwa hawaamini. Kama ulikuwa na mashaka, jiandae, maana baada ya kusoma haya, utaanza kuangalia dunia kwa jicho la pili!

UCHAWI NI NINI?

Uchawi ni matumizi ya nguvu zisizoonekana kwa macho ya kawaida ili kuleta mabadiliko fulani katika maisha ya mtu au mazingira. Katika historia, tamaduni mbalimbali duniani zimethibitisha uwepo wa uchawi kupitia simulizi, vitendo vya kishirikina, na hata matukio ambayo hayaelezeki kisayansi. Leo, tunapitia matukio 12 yaliyoacha watu midomo wazi!


MATUKIO 12 YALIYOTHIBITISHA UWEPO WA UCHAWI

1. Mtoto Mdogo Anaamka Akiwa Amenyolewa Nusu Bila Sababu


Hili ni tukio la kushangaza sana. Wazazi wanalala na mtoto wao akiwa mzima kabisa, lakini asubuhi wanakuta kichwa chake kimenyoa nusu, au hata kuna alama za ajabu mwilini mwake. Je, nani alimuingilia usiku bila mlango wa nyumba kufunguliwa? Hili ni jambo linaloripotiwa mara kwa mara, hasa katika maeneo yenye imani kali za kishirikina.

2. Ramli/Kupiga Chungu – Usiibe Kwa Mtu Hatari!

Ukiiba kwa mtu anayejua kuwatumia wataalamu wa ramli, basi jua kizazi chako kipo hatarini! Kuna matukio mengi ya watu walioiba, kisha wakaumwa vibaya au hata kupoteza maisha kwa njia za ajabu. Wengine wamekufa mfululizo kwenye familia moja hadi msiba wa mwisho, ndipo siri inajulikana!

3. Gari Lako Likiingia Kijijini Linakufa Bila Tatizo Lolote!

Wengi wamekutana na hili! Unaendesha gari lako vizuri, lakini ukifika kijijini, asubuhi gari haliwaki kabisa. Ukiita fundi, anakwambia gari halina tatizo lolote. Cha kushangaza, ukinunulia wazee pombe au kutoa kitu kidogo kwa waganga wa kienyeji, ghafla gari linaamka na linafanya kazi kama kawaida! Huu ni uchawi wa wazi kabisa.

4. Utajiri wa Majini – Kupata Mali Ndani ya Muda Mfupi!

Watu wengi wameshuhudia watu wanaotajirika ghafla kwa njia zisizoeleweka, lakini wakikaa kwa muda mrefu wanagundua kuwa wana masharti magumu. Wengine hawaruhusiwi kula baadhi ya vyakula, wengine hawatakiwi kugusa watu wa familia zao, na kuna wanaolazimika kutoa kafara ili kulinda mali zao!

5. Mazingaombwe – Je, Ni Uchawi au Ni Sanaa ya Ajabu?

Mazingaombwe yamekuwa yakifanywa na watu maarufu duniani, lakini yapo ambayo hayaelezeki kabisa. Mtu anapita ukutani, mwingine anatoweka mbele ya macho ya watu, mwingine anaweza kusoma mawazo ya mtu! Hii ni nguvu ambayo bado haijaeleweka kikamilifu.

6. Mapepo Kanisani – Mtu Msomi Anabadilika Kabisa!

Mtu msomi, mwenye akili zake timamu, akiingia kanisani, ghafla anaanza kurukaruka na kuzungumza kwa sauti ya ajabu. Watu hata 10 wanashindwa kumshika, na mara nyingi huwa na nguvu zisizoelezeka! Hili limekuwa likitokea kila mahali na ni uthibitisho mwingine kwamba kuna nguvu zisizoonekana.

7. Kulogwa – Mtu Anaweza Kuwa Kichaa Bila Sababu!

Mtu anayeishi maisha ya kawaida ghafla anabadilika; anakuwa kichaa au anaumwa kwa njia isiyoelezeka. Wengi wakienda hospitali hawapati ugonjwa wowote, lakini wanapopelekwa kwa maombi au kwa mganga wa kienyeji, wanapona! Je, hii ni nguvu gani?

8. Vyama vya Kishirikina – Illuminati na Freemasons

Dunia imejaa vyama vya kushangaza kama Illuminati na Freemasons, ambavyo vinadaiwa kutumia nguvu za giza ili kudhibiti ulimwengu. Watu wengi waliokuwa wanachama wa vyama hivi wamekiri kuona mambo yasiyo ya kawaida, na wengine wanasema walitoa kafara ili kupata mafanikio!

9. Msukule na Kafara – Watu Wanazikwa Wanarudi!

Kuna matukio ya kutisha ambapo mtu anazikwa, lakini baada ya muda anarudi akiwa mzima! Hili limeshuhudiwa sehemu nyingi, hasa maeneo ya Kanda ya Ziwa. Watu waliodhaniwa kuwa wamefariki walirudi na kusema walichukuliwa msukule!

10. Kuzuiwa Kuingia Kwenye Nyumba au Kijiji Fulani!

Watu wamewahi kwenda kijijini au kwenye nyumba fulani na wanashindwa kuingia, hata mlango ukiwa wazi. Baadhi yao wanasema wanahisi ukuta usioonekana, wengine wanasikia sauti zinazowazuia, na wengine hata hupoteza fahamu!

11. Uchawi wa Kupoteza Kitu Machoni pa Watu!

Watu wameshuhudia pesa au vitu vikitoweka ghafla, lakini vikipatikana baada ya matambiko fulani kufanywa. Wengine wanapoteza vitu kwenye meza mbele yao, lakini vikijulikana vimefichwa sehemu isiyoelezeka!

12. Nyoka wa Ajabu Katika Maeneo ya Watawala wa Kienyeji

Watu wengi wameeleza kushuhudia nyoka wakubwa wenye akili tofauti, wanaojua kupiga kelele au hata kuwasiliana na binadamu kwa ishara! Wengine wanasema nyoka hawa hawawezi kuuawa kwa risasi za kawaida, na baadhi yao huonekana kwa watu fulani tu.

Niwape ka stori kidogo.
Siku moja nilipita kwenye makaburi ya manispaa usiku. Nilipokuwa karibu na kaburi fulani, niliona mtu amevaa suti kali sana, akizunguka makaburini kwa mwendo wa taratibu. Nilijaribu kumuita, lakini hakuitika. Niliposogea karibu, nilifikiria kupapasa mfuko wake wa koti, na cha kushangaza, nilikuta ndani kuna makaratasi meupe tupu!

Nilipohisi kuna jambo la ajabu, niligeuka kukimbia, lakini ghafla miguu yangu ilihisi kama imefungwa na kamba isiyoonekana. Nikajaribu kupiga kelele, lakini sauti haikutoka! Baada ya dakika chache za kupambana, ghafla hali ikarudi kawaida, na nilikimbia bila kuangalia nyuma! Hadi leo sijui kilichotokea.

Watu wengi hawaamini uchawi kwa sababu sayansi haijaupa nafasi kubwa. Lakini mbona sayansi haijawahi kutoa maelezo ya kuridhisha kuhusu matukio haya yote? Wanasayansi wafanye utafiti wa kweli – ukweli upo wazi!

Upo upande gani? Uchawi upo au ni fikra tu? Tuachie maoni yako!
 
Kiimani uchawi upo kisayansi haupo.
Mimi naamini upo kwa sababu kila siku wanakuja usiku kwangu hata Leo watakuja lkn Mimi siwaogopi kwa sababu hawawezi nifanya kitu nikadhurika
 
Mimi huwa naona vivuli vya watu usiku ndani mwangu wakati mwingine namuona mke wangu anainuka nikiwa nusu macho, nikifumbua macho tu anapotea inakuwa mida ya alfajili.
Nimefatilia kwa waonaji wa pande zote mbili sijapata majibu yanayofanana.

1 . Wengine wanasema ni michezo unachezewa ili umchukie mkeo umuache.

2.Wengine wanasema yupo kwenye vyama anatumika kwa kujua au kutojua huyo, thus hivyo vivuli uvionavyo ndani ni members wenzake.

Pana siku aliamka saa kumi alfajili anasali sebuleni nimelala chumbani akiwa kwenye maombi nikaona kivuli chake kaamka akapotea nikasema Leo lazima nimwambie nikamfata sebuleni kumwambia mbona nakuona huwa unapaa akasema mbona Mimi nipo sawa sihisi kitu,akampigia mchungaji wake akamwambia wwe nafsi yako unatumika.

So hadi sasa sijapata jibu.
Which is which au na ishi na members ndani,but Mimi siwaogopi naona kawaida tu.
Mimi hata nikutane na jini siogopi mwili utasisimuka then kila mmoja na na hamsini lakini kichwani mwngu najua.

Mwenye dawa ya kuwauwa wachawi tuwasiliane au jinsi ya kuwapa adabu hawa wapumbavu wakosa kazi usiku wakome kuja
 
Nilimuuliza mtaalam mmoja inakuwaje huyo mtu anayesadikika mchawi anaishi maisha ya kifukara nyumba ya makuti, akasema usione ananyumba ya makuti huyo ni tajiri mkubwa kwenye ulimwengo wa roho.. anamiliki usafiri daraja la kwanza na mizigo hatari ya bei ghali.. so ukimuona kwa macho ya nyama ni broke ila usiku kwenye vikao vyao ni don
 
Mimi huwa naona vivuli vya watu usiku ndani mwangu wakati mwingine namuona mke wangu anainuka nikiwa nusu macho, nikifumbua macho tu anapotea inakuwa mida ya alfajili.
Nimefatilia kwa waonaji wa pande zote mbili sijapata majibu yanayofanana.
1 .
Wengine wanasema ni michezo unachezewa ili umchukie mkeo umuache.
2.Wengine wanasema yupo kwenye vyama anatumika kwa kujua au kutojua huyo, thus hivyo vivuli uvionavyo ndani ni members wenzake.
Pana siku aliamka saa kumi alfajili anasali sebuleni nimelala chumbani akiwa kwenye maombi nikaona kivuli chake kaamka akapotea nikasema Leo lazima nimwambie nikamfata sebuleni kumwambia mbona nakuona huwa unapaa akasema mbona Mimi nipo sawa sihisi kitu,akampigia mchungaji wake akamwambia wwe nafsi yako unatumika.
So hadi sasa sijapata jibu.
Which is which au na ishi na members ndani,but Mimi siwaogopi naona kawaida tu.
Mimi hata nikutane na jini siogopi mwili utasisimuka then kila mmoja na na hamsini lakini kichwani mwngu najua.
Mwenye dawa ya kuwauwa wachawi tuwasiliane au jinsi ya kuwapa adabu hawa wapumbavu wakosa kazi usiku wakome kuja
Dawa yao ni maombi tu au upate wachawi safe(white) hao wakusaidie
 
Nilimuuliza mtaalam mmoja inakuwaje huyo mtu anayesadikika mchawi anaishi maisha ya kifukara nyumba ya makuti, akasema usione ananyumba ya makuti huyo ni tajiri mkubwa kwenye ulimwengo wa roho.. anamiliki usafiri daraja la kwanza na mizigo hatari ya bei ghali.. so ukimuona kwa macho ya nyama ni broke ila usiku kwenye vikao vyao ni don
Duh 🙄 haya mambo yana shangaza alafu inaambiwa mchawi akikamatwa kwa kuonekana tu bila kushikwa ndio cheo kinapanda
 
Kuna tatizo la kufikiria uchawi ni matukio ya ajabu ajabu tu ila kwa upande wangu hiyo sio njia sahihi kuthibitisha uwepo wa uchawi kwanza sio kila tukio la ajabu ni uchawi bali mengine ni vitendo ambavyo hufanywa na majini na sio uchawi.

Kuuelezea uchawi kwa kutumia matukio kama hayo ni kufanya ionekane kama uchawi ni mambo ya kusimulika ila uhalisia ni kwa afrika uchawi upo sehemu kubwa ya maisha na ndio maana waganga wamekuwa ni wengi.
 
Kuna tatizo la kufikiria uchawi ni matukio ya ajabu ajabu tu ila kwa upande wangu hiyo sio njia sahihi kuthibitisha uwepo wa uchawi kwanza sio kila tukio la ajabu ni uchawi bali mengine ni vitendo ambavyo hufanywa na majini na sio uchawi.

Kuuelezea uchawi kwa kutumia matukio kama hayo ni kufanya ionekane kama uchawi ni mambo ya kusimulika ila uhalisia ni kwa afrika uchawi upo sehemu kubwa ya maisha na ndio maana waganga wamekuwa ni wengi.
Ni kweli mkuu.
 
Wanasemaga lisemwalo lipo na HILI la uchawi limesemwa kupitiliza,uchawi upo,ulikuwepo,na utazidi kuwepo.
 
It's another beautiful day, another beautiful thread!

Mimi ni Davidmmarista, na leo tunakuja na Uzi mzito wa kutikisa akili! Uchawi upo ama ni hadithi tu? Leo tunachambua matukio halisi 12 yaliyothibitisha uwepo wa uchawi, hasa kwa wale ambao walikuwa hawaamini. Kama ulikuwa na mashaka, jiandae, maana baada ya kusoma haya, utaanza kuangalia dunia kwa jicho la pili!

UCHAWI NI NINI?

Uchawi ni matumizi ya nguvu zisizoonekana kwa macho ya kawaida ili kuleta mabadiliko fulani katika maisha ya mtu au mazingira. Katika historia, tamaduni mbalimbali duniani zimethibitisha uwepo wa uchawi kupitia simulizi, vitendo vya kishirikina, na hata matukio ambayo hayaelezeki kisayansi. Leo, tunapitia matukio 12 yaliyoacha watu midomo wazi!


MATUKIO 12 YALIYOTHIBITISHA UWEPO WA UCHAWI

1. Mtoto Mdogo Anaamka Akiwa Amenyolewa Nusu Bila Sababu


Hili ni tukio la kushangaza sana. Wazazi wanalala na mtoto wao akiwa mzima kabisa, lakini asubuhi wanakuta kichwa chake kimenyoa nusu, au hata kuna alama za ajabu mwilini mwake. Je, nani alimuingilia usiku bila mlango wa nyumba kufunguliwa? Hili ni jambo linaloripotiwa mara kwa mara, hasa katika maeneo yenye imani kali za kishirikina.

2. Ramli/Kupiga Chungu – Usiibe Kwa Mtu Hatari!

Ukiiba kwa mtu anayejua kuwatumia wataalamu wa ramli, basi jua kizazi chako kipo hatarini! Kuna matukio mengi ya watu walioiba, kisha wakaumwa vibaya au hata kupoteza maisha kwa njia za ajabu. Wengine wamekufa mfululizo kwenye familia moja hadi msiba wa mwisho, ndipo siri inajulikana!

3. Gari Lako Likiingia Kijijini Linakufa Bila Tatizo Lolote!

Wengi wamekutana na hili! Unaendesha gari lako vizuri, lakini ukifika kijijini, asubuhi gari haliwaki kabisa. Ukiita fundi, anakwambia gari halina tatizo lolote. Cha kushangaza, ukinunulia wazee pombe au kutoa kitu kidogo kwa waganga wa kienyeji, ghafla gari linaamka na linafanya kazi kama kawaida! Huu ni uchawi wa wazi kabisa.

4. Utajiri wa Majini – Kupata Mali Ndani ya Muda Mfupi!

Watu wengi wameshuhudia watu wanaotajirika ghafla kwa njia zisizoeleweka, lakini wakikaa kwa muda mrefu wanagundua kuwa wana masharti magumu. Wengine hawaruhusiwi kula baadhi ya vyakula, wengine hawatakiwi kugusa watu wa familia zao, na kuna wanaolazimika kutoa kafara ili kulinda mali zao!

5. Mazingaombwe – Je, Ni Uchawi au Ni Sanaa ya Ajabu?

Mazingaombwe yamekuwa yakifanywa na watu maarufu duniani, lakini yapo ambayo hayaelezeki kabisa. Mtu anapita ukutani, mwingine anatoweka mbele ya macho ya watu, mwingine anaweza kusoma mawazo ya mtu! Hii ni nguvu ambayo bado haijaeleweka kikamilifu.

6. Mapepo Kanisani – Mtu Msomi Anabadilika Kabisa!

Mtu msomi, mwenye akili zake timamu, akiingia kanisani, ghafla anaanza kurukaruka na kuzungumza kwa sauti ya ajabu. Watu hata 10 wanashindwa kumshika, na mara nyingi huwa na nguvu zisizoelezeka! Hili limekuwa likitokea kila mahali na ni uthibitisho mwingine kwamba kuna nguvu zisizoonekana.

7. Kulogwa – Mtu Anaweza Kuwa Kichaa Bila Sababu!

Mtu anayeishi maisha ya kawaida ghafla anabadilika; anakuwa kichaa au anaumwa kwa njia isiyoelezeka. Wengi wakienda hospitali hawapati ugonjwa wowote, lakini wanapopelekwa kwa maombi au kwa mganga wa kienyeji, wanapona! Je, hii ni nguvu gani?

8. Vyama vya Kishirikina – Illuminati na Freemasons

Dunia imejaa vyama vya kushangaza kama Illuminati na Freemasons, ambavyo vinadaiwa kutumia nguvu za giza ili kudhibiti ulimwengu. Watu wengi waliokuwa wanachama wa vyama hivi wamekiri kuona mambo yasiyo ya kawaida, na wengine wanasema walitoa kafara ili kupata mafanikio!

9. Msukule na Kafara – Watu Wanazikwa Wanarudi!

Kuna matukio ya kutisha ambapo mtu anazikwa, lakini baada ya muda anarudi akiwa mzima! Hili limeshuhudiwa sehemu nyingi, hasa maeneo ya Kanda ya Ziwa. Watu waliodhaniwa kuwa wamefariki walirudi na kusema walichukuliwa msukule!

10. Kuzuiwa Kuingia Kwenye Nyumba au Kijiji Fulani!

Watu wamewahi kwenda kijijini au kwenye nyumba fulani na wanashindwa kuingia, hata mlango ukiwa wazi. Baadhi yao wanasema wanahisi ukuta usioonekana, wengine wanasikia sauti zinazowazuia, na wengine hata hupoteza fahamu!

11. Uchawi wa Kupoteza Kitu Machoni pa Watu!

Watu wameshuhudia pesa au vitu vikitoweka ghafla, lakini vikipatikana baada ya matambiko fulani kufanywa. Wengine wanapoteza vitu kwenye meza mbele yao, lakini vikijulikana vimefichwa sehemu isiyoelezeka!

12. Nyoka wa Ajabu Katika Maeneo ya Watawala wa Kienyeji

Watu wengi wameeleza kushuhudia nyoka wakubwa wenye akili tofauti, wanaojua kupiga kelele au hata kuwasiliana na binadamu kwa ishara! Wengine wanasema nyoka hawa hawawezi kuuawa kwa risasi za kawaida, na baadhi yao huonekana kwa watu fulani tu.

Niwape ka stori kidogo.
Siku moja nilipita kwenye makaburi ya manispaa usiku. Nilipokuwa karibu na kaburi fulani, niliona mtu amevaa suti kali sana, akizunguka makaburini kwa mwendo wa taratibu. Nilijaribu kumuita, lakini hakuitika. Niliposogea karibu, nilifikiria kupapasa mfuko wake wa koti, na cha kushangaza, nilikuta ndani kuna makaratasi meupe tupu!

Nilipohisi kuna jambo la ajabu, niligeuka kukimbia, lakini ghafla miguu yangu ilihisi kama imefungwa na kamba isiyoonekana. Nikajaribu kupiga kelele, lakini sauti haikutoka! Baada ya dakika chache za kupambana, ghafla hali ikarudi kawaida, na nilikimbia bila kuangalia nyuma! Hadi leo sijui kilichotokea.

Watu wengi hawaamini uchawi kwa sababu sayansi haijaupa nafasi kubwa. Lakini mbona sayansi haijawahi kutoa maelezo ya kuridhisha kuhusu matukio haya yote? Wanasayansi wafanye utafiti wa kweli – ukweli upo wazi!

Upo upande gani? Uchawi upo au ni fikra tu? Tuachie maoni yako!
Nilidhani umekuja na concrete evidence za uwepo wa UCHAWI kumbe na wewe umekuja na blah blah tu

Tuanze na mfano wako
Unapita makaburini usiku
Unakuta kuna mtu kavaa suti kali nyeusi anazunguka kaburi
Unamuita haitiki
Unaamua kwenda kumpekua mfukoni kwake na unakutana na makaratasi meupe

Hii stori hata mwanangu wa darasa la 5 hawezi kukuelewa
Huo ujasiri wa kwenda kupekua watu wanazunguka makaburini usiku uliutoa wapi mkuu?
Mbona mnatunga Hadithi za kitoto sana
 
Back
Top Bottom