Mavipunda
JF-Expert Member
- Jun 27, 2012
- 7,072
- 7,891
Kuna taarifa za kupotea kwa motto mwengine anasoma shule ya Roman Catholic pale Mabibo maarufu farasi, Matukio haya yanaongezeka lakini hadi sasa hakuna kauli yeyote ya serikali kuhusu kadhia hii. Watoto wa wanyonge wanapotea lakini rais wa wanyonge hajawahi hata kutoa pole kwa walezi na wazazi.
Ziliokotwa maiti za watoto watatu kwenye gari bovu kule Wilaya ya Temeke hatukuona hata sura ya ocd kusema chochote. Alipotea Mo tu kwa vile ana ukwasi watu hawakulala na RC alifika eneo la tukio kama mshale.
Hebu tuvae viatu vya wazazi wanaopoteza watoto hao ni simanzi kwa kweli tunaomba tupatiwe taarifa za kintelejensia kuhusu matukio haya kwani wananchi wameshanza kuhisi yana mkono wa sirikali au wanansiasa wa chama tawala
Ziliokotwa maiti za watoto watatu kwenye gari bovu kule Wilaya ya Temeke hatukuona hata sura ya ocd kusema chochote. Alipotea Mo tu kwa vile ana ukwasi watu hawakulala na RC alifika eneo la tukio kama mshale.
Hebu tuvae viatu vya wazazi wanaopoteza watoto hao ni simanzi kwa kweli tunaomba tupatiwe taarifa za kintelejensia kuhusu matukio haya kwani wananchi wameshanza kuhisi yana mkono wa sirikali au wanansiasa wa chama tawala