Pre GE2025 Matukio ya watu kupotea na waganga kuhusishwa na vifo vyao ajenda ya kuisafisha serikali na polisi kwenye tuhuma hizo?

Pre GE2025 Matukio ya watu kupotea na waganga kuhusishwa na vifo vyao ajenda ya kuisafisha serikali na polisi kwenye tuhuma hizo?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa zinatolewa kuwa aidha maiti zimefukuliwa kwa mganga wa kienyeji na maiti hizo unakuta ni za watu ambao walipotea na kutafutwa na ndugu, au mtu kafia kwa mganga na mtu huyo alitoweka akawa anatafutwa.
Sisemi haiwezekani kuwa ni kweli mganga kuua kutokana na imani za kishirikina ila kwa nini matukio haya yamekuwa yanaripotiwa kwa wingi sana siku za hivi karibuni, hasa ukizingatia kumekuwa na wingi wa taarifa za kupotea, kutekwa na kuuawa watu na watu wasiojulikana?

Najaribu kuwaza ina maana hao waganga wameanza kuua watu siku hizi wakati wa sintofahamu hii au kuna ajenda ya watu wasiojulikana kutaka kujivua lawama na kuwasingizia waganga ili watu waache kupiga kelele kwa kuwa wataona ni matukio yanayofanywa na watu tulionao uraiani yaani waganga pale zinapotokea changamoto za kiufundi kwenye mambo yao au waganga kutoa kafara?
Napata mashaka huenda kuna kitu kinapikwa hasa ukizingatia kauli tata za wenye mamlaka kuonesha kuwa masuala haya ya utekaji ni "vijidrama" au wengine wakisema kujiteka tu kuteka ili watu wapate pesa, kauli hizi nilizichukilia kama kuufanya umma uone hakuna jambo la hatari na mambo yako shwari na waachane na kelele zinazodai kuna utekaji, kama waliweza kuita drama wanashindwa kuseti ajenda kuwa ni watu wanauawa kwa mganga?
Naona harufu ya mchezo mchafu katika hii ya maiti kufukuliwa kwa mganga, mganga kukiri kuua na kuwapeleka kuonesha miili, miili kukutwa ndani au nyuma ya nyumba ya mganga, mganga kuwazika watu porini au shambani, kuna harufu mbaya dhidi ya janga la watu wasiojulikana na hawa waganga. Yawezekana sasa kila anayepotea atakutwa kafa kwa mganga!

Pia soma:
 
Siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa zinatolewa kuwa aidha maiti zimefukuliwa kwa mganga wa kienyeji na maiti hizo unakuta ni za watu ambao walipotea na kutafutwa na ndugu, au mtu kafia kwa mganga na mtu huyo alitoweka akawa anatafutwa.

Siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa zinatolewa kuwa aidha maiti zimefukuliwa kwa mganga wa kienyeji na maiti hizo unakuta ni za watu ambao walipotea na kutafutwa na ndugu, au mtu kafia kwa mganga na mtu huyo alitoweka akawa
Zamani intelijensia ilianzia kwa watu mitaani mfano mafundi viatu, wauza bar na wengine walikuwa waajiriwa wa TISS na kazi ilikuwa rahisi kufanyika na pengine matukio hayakutokea kabla wahalifu kunaswa. Leo hii Askari Polisi anamnyanyasa raia ambaye ni prime kwa kumpa taarifa.

Matukio yote ya waganga hawa yametokea bila polisi kuwa na taarifa. Hii inasababishwa na tabia yenu kujitenga na raia.

Kitengo cha intelijensia au detective hamtakiwi kuwa makatili kwa raia, utapataje taarifa wewe? Oneni sasa mnapata taarifa za miezi kadha iliyopita, mfano halisi hii issue ya mganga wa Singida. Change is highly needed!
 
Back
Top Bottom