Mwawado
JF-Expert Member
- Nov 2, 2006
- 993
- 259
Je unakubaliana na huyu Muungwana anayeandika matumizi ya haya maneno hapo chini?
Si vibaya tukapeana japo nyepesi nyepesi za lugha ya kiswahili baada ya kuonekana watu wengi kuitumia lugha hii ndivyo sivyo. Kwa uchache labda nichambue matumizi ya maneno yafuatayo.
1. Kuonyesha hali ya utashi baina ya vitu viwili. Wengi wetu hutumia, ...naweza panda aidha daladala au nikatembea. Usahihi wa hapa ni kwamba naweza panda ama daladala au nikatembea.
2. Tendo la kupiga mpira ili uweze kumkuta mchezaji mwingine. Wengi husema,...Juma alimpasia Hamad kabla ya kufunga bao. Usahihi ni kwamba, Juma alimpa mgongeo Hamad kabla ya...
3. Tendo la kutafasiri maana toka lugha moja hadi nyingine moja kwa moja. Wengi husema,...jamaa katafasiri moja kwa moja. Usahihi ni kwamba, ...fulani kafanya tafasiri sisisi.
4. Tendo la kupenyeza kitu kwenye tundu au kijishimo, mfano matumizi ya kadi ya ATM wakati wa kuchukua pesa. Wengi wetu husema ama kuingiza au kuweza. Kiswahili fasaha ni kubokoza kadi...
5. Binti mrembo apatikanae baada ya mashindano fulani ya urembo huitwa misi. Usahihi ni ama mlimbwende au banati. Mfano, ...juzi tulikwenda kushuhudia mashindano ya mabanati wa Tabata.
6. Mauaji yatokanayo na vita huitwa mauaji ya halaiki wakati usahihi ni mauaji ya kimbari...
7. Makubaliano ambayo yatamaliza uhasama wa muda fulani ambayo kwayo pande kinzani zitaweka ushuhuda wa maandishi, hii ilizoeleka kama azimio...usahihi wake ni mwafaka. (Azimio hutumika pale mtu au kundi fulani wanapotoa tamko na mara nyingi likionyesha muda ufuatao)
8. Hali ya kutokuwa na fedha hutumika kama ukwasi...usahihi wake ni ukata. (ukwasi huonesha utoshelevu na pengine ziada ya fedha)
9. Hali ya kuwa unadaiwa kiasi fulani cha fedha ili kutimiza hadi yako fulani watu huita balansi au salio. Usahihi ni bakaa.
10. Jini mkubwa ambaye husadikika kuishi kwenye miti mikubwa kama mbuyu huitwa subiani na wala si. pepo (Kinyamkela huwa ndiye pepo ambaye hupungwa/kufukuzwa kwa ngoma inayokesha)
Si vibaya tukapeana japo nyepesi nyepesi za lugha ya kiswahili baada ya kuonekana watu wengi kuitumia lugha hii ndivyo sivyo. Kwa uchache labda nichambue matumizi ya maneno yafuatayo.
1. Kuonyesha hali ya utashi baina ya vitu viwili. Wengi wetu hutumia, ...naweza panda aidha daladala au nikatembea. Usahihi wa hapa ni kwamba naweza panda ama daladala au nikatembea.
2. Tendo la kupiga mpira ili uweze kumkuta mchezaji mwingine. Wengi husema,...Juma alimpasia Hamad kabla ya kufunga bao. Usahihi ni kwamba, Juma alimpa mgongeo Hamad kabla ya...
3. Tendo la kutafasiri maana toka lugha moja hadi nyingine moja kwa moja. Wengi husema,...jamaa katafasiri moja kwa moja. Usahihi ni kwamba, ...fulani kafanya tafasiri sisisi.
4. Tendo la kupenyeza kitu kwenye tundu au kijishimo, mfano matumizi ya kadi ya ATM wakati wa kuchukua pesa. Wengi wetu husema ama kuingiza au kuweza. Kiswahili fasaha ni kubokoza kadi...
5. Binti mrembo apatikanae baada ya mashindano fulani ya urembo huitwa misi. Usahihi ni ama mlimbwende au banati. Mfano, ...juzi tulikwenda kushuhudia mashindano ya mabanati wa Tabata.
6. Mauaji yatokanayo na vita huitwa mauaji ya halaiki wakati usahihi ni mauaji ya kimbari...
7. Makubaliano ambayo yatamaliza uhasama wa muda fulani ambayo kwayo pande kinzani zitaweka ushuhuda wa maandishi, hii ilizoeleka kama azimio...usahihi wake ni mwafaka. (Azimio hutumika pale mtu au kundi fulani wanapotoa tamko na mara nyingi likionyesha muda ufuatao)
8. Hali ya kutokuwa na fedha hutumika kama ukwasi...usahihi wake ni ukata. (ukwasi huonesha utoshelevu na pengine ziada ya fedha)
9. Hali ya kuwa unadaiwa kiasi fulani cha fedha ili kutimiza hadi yako fulani watu huita balansi au salio. Usahihi ni bakaa.
10. Jini mkubwa ambaye husadikika kuishi kwenye miti mikubwa kama mbuyu huitwa subiani na wala si. pepo (Kinyamkela huwa ndiye pepo ambaye hupungwa/kufukuzwa kwa ngoma inayokesha)