Sungurampole
JF-Expert Member
- Nov 17, 2007
- 984
- 205
Leo nilipoenda benki moja niliona yule teller alivyokua ananinihesabia pesa mashine aliiweka ikawa inamwelekea yeye kiasi kua nilikua sioni ilivyokua inahesabu. Ili mimi nijiridhishe kuwa pesa nilizopewa ziko sawa ilibidi nirudie kuzihesabu noti zote jambo ambalo sikufikiri lilikua la lazima. Hii ilinipelekea kujiuliza swali hili - "Hivi ipi njia sahihi ya kutumia mashine za kuhesabia noti na je, kwa sasa zinatumikaje na baadhi ya mateller wa benki?"