Matumizi sahihi ya vipaza sauti ( microphones)

Matumizi sahihi ya vipaza sauti ( microphones)

Big L

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2022
Posts
502
Reaction score
820
Habari zenu wanajamvi,

Leo nimekuja na suala hili la matumizi sahihi ya vipaza sauti nikiwa naomba mawazo yenu na hoja zenu kuhusiana na hili.

Makanisani, Mikutanoni, kwenye sherehe mbalimbali na sehemu nyingine nyingi tumekuwa tukitumia vipaza sauti tena kwa kupokezana yaani unakuta kipaza sauti kimoja mnatumia hata watu 30.

Wataalamu wa afya na microbiology pamoja na watu wengine je hili lina athari yoyote ya kiafya? Na kama zipo ni zipi na kipi kifanyike ili kuzuia athari hizo?

Leo mimi nilikuwa kwenye sherehe fulani sasa kuna mtu alipewa kipaza sauti aongee jambo fulani kwa bahati mbaya alikuwa anaongea kwa kutoa mate mengi sana juu ya kile kapaza sauti na baada ya yeye ilifuata zamu yangu kiukweli nilishindwa kuvumilia nikiaenda kwa DJ kuzuga kama naongea nae nikatoa kitambaa nikafuta sehemu ya juu ya kile kipaza sauti kisha nikarudi kuongea sasa.

Naombeni michango yenu tafadhali najua itakuwa msaada pia kwa watu wengine humu jukwaani.

Big L.
 
Kama jina linavyojieleza kwa haraka haraka ni kwa ajili ya Kupazia sauti. Labda wataalam watueleze kitaalamu!
 
Katika miwili wa binadamu mdogo ndiyo sehemu kuna bacteria wengi sana
Hapo mnapeana magonjwa tuu
Jiandae kumeza madawa
 
Kama haupo kwenye Tasnia ya Mc's,wachungaji,waalimu,manabii,msanii,mtangazaji,mwanasiasa msemaji wa taasisi idara n.k
Kwako kutumia siku moja haina madhara kwako ila kwa kanuni ya afya ulivyofanya kufuta mate uko sahihi.
Mm nimekuepo eneo moja wapo ktk tajwa hapo juu,Kinachofanyika ,Ili kuepuka maambukizi ya kwa njia ya hewa kwa maana ya kulamba lamba microphone au kupumulia alipopumulia mwenzio, ni kuandaa microphone ya main speaker ya kwake peke yake, au kubadilisha sponge mara kwa mara kwa mic zinazotumika na kuhakikisha ziko safi (sponge)
Hii ni kupunguza hatari kubwa ya kupata magonjwa kwa njia hewa ikiwemo Tb.(kifua kikuu)
Ukiona TID anamwambia mwana habari sogeza mbali microphone ,sio tu kichekesho kile bali anaelewa anachokifanya.
 
Back
Top Bottom