Matumizi ya AC ya gari, Je, ni kweli inakula mafuta?

Matumizi ya AC ya gari, Je, ni kweli inakula mafuta?

sisi ni ndugu

Senior Member
Joined
Sep 4, 2018
Posts
121
Reaction score
136
Natumai wote tu wazima. Naomba kueleweshwa katika hili, hivi AC katika gari inakula mafuta sana? Au ni wastani tu?

Majibu yaliyotolewa na wadau
Mkuu kwa kifupi jibu halipo straight foward. AC ya gari unatumia nguvu kutoka kwenye engine,no maana hata unapowasha AC muungurumo huwa unabadilika. Kwa hiyo unatumia mafuta zaidi,hiyo ni sehemu ya kwanza.

Sehemu ya pili ni kwamba unapofungua vioo haswa kwenye high speed ili kuokoa mafuta, upepo unaingia ndani na kusababisha 'drag' yaani gari inakuwa kama inazuiwa kwenda kwa sababu ya upepo unaojaa ndani na hapo inasababisha gari kutumia mafuta mengi zaidi ya unapokuwa umewasha AC.

kumbuka kuwa gari inapokuwa designed na kuwekwa kwenye "wind tunnel" madirisha huwa yamefungwa. kama umeweza kunua gari,sidhani kama suala la mafuta linatakiwa kukuumiza kichwa.Chagua sumu yako hapo.
---
Nipo kwenye hii Field. Uliyosema yana ukweli kabisa.

Nashauri tu kwamba wewe unaetumia A/C hakikisha mfumo wake uwe katika hali nzuri.

Kuna kifaa kinaitwa Compressor huwa kina engage na kudisengage kutokana na demand ya ubaridi ndani ya gari sasa kama mfumo wa a/c haupo vizuri kufikisha ubaridi unaotakiwa inamaana compressor yako itaengage kwa muda mrefu sana au moja kwa moja na hivyo kuweka mzigo kwenye injini kwa muda mrefu.

Pia hakikisha unafunga vioo na hakikisha pia seals kwenye milango na sehemu zenye upenyo zipo madhubuti ili zisiingize hewa kutoka nje ambayo ni ya moto vitavyofanya uhitaji wa compressor kuengage kwa interval fupifupi.

Otherwise Mfumo wa A/C wa gari ukiwa madhubuti hautaongeza sana Fuel Consumption ya gari lako.
 
Mkuu kwa kifupi jibu halipo straight foward. AC ya gari unatumia nguvu kutoka kwenye engine,no maana hata unapowasha AC muungurumo huwa unabadilika. Kwa hiyo unatumia mafuta zaidi,hiyo ni sehemu ya kwanza.

Sehemu ya pili ni kwamba unapofungua vioo haswa kwenye high speed ili kuokoa mafuta, upepo unaingia ndani na kusababisha 'drag' yaani gari inakuwa kama inazuiwa kwenda kwa sababu ya upepo unaojaa ndani na hapo inasababisha gari kutumia mafuta mengi zaidi ya unapokuwa umewasha AC.

kumbuka kuwa gari inapokuwa designed na kuwekwa kwenye "wind tunnel" madirisha huwa yamefungwa. kama umeweza kunua gari,sidhani kama suala la mafuta linatakiwa kukuumiza kichwa.Chagua sumu yako hapo.
 
Kwangu sijawahi kuona tofauti gari ikiwa full AC au vioo chini. Tofauti niliyoiona ni pale vumbi linapojaa ndani ya gari baada ya kushusha vioo na pale gari inapokuwa safi ndani kwa kutumia AC muda wote. Naona ninatumia mafuta yaleyale tu ya laki na 20 hadi 50 kwa mwezi kulingana na misele.
 
Kwangu sijawahi kuona tofauti gari ikiwa full AC au vioo chini. Tofauti niliyoiona ni pale vumbi linapojaa ndani ya gari baada ya kushusha vioo na pale gari inapokuwa safi ndani kwa kutumia AC muda wote. Naona ninatumia mafuta yaleyale tu ya laki na 20 hadi 50 kwa mwezi kulingana na misele.
Ubishi usio na tija,car proffessionals wenyewe wanakwambia AC ni moja ya vitu vinavyosababisha utumiaji wa mafuta kuongezeka,lakini kuna watu mara zote wamekuwa wakipinga hili swala, sio kwamba unakatazwa kutumia,kama mfuko wako unakuruhusu tumia ila usidanganye watu palipo na ukweli.

Unapowasha AC engine unaiongezea mzigo ndio maana utakuta hata mlio wa gari unaongezeka au baadhi ya gari utaona ina vibrate, kwahiyo automatically lazima matumizi ya mafuta yapande.Hii nimeitoa google, Air conditioning uses fuel, using a vehicle's air-conditioning system increases its fuel consumption more than any other auxiliary feature.
An air-conditioning (a/c) system can increase fuel consumption by up to 20% because of the extra load on the engine.
 
Ubishi usio na tija,car proffessionals wenyewe wanakwambia AC ni moja ya vitu vinavyosababisha utumiaji wa mafuta kuongezeka,lakini kuna watu mara zote wamekuwa wakipinga hili swala,sio kwamba unakatazwa kutumia,kama mfuko wako unakuruhusu tumia ila usidanganye watu palipo na ukweli...
Mimi sijabisha, punguza mzuka. Mimi nimetoa experience kwenye chombo changu. Nimeanza na sentensi inasema "Kwangu sijawahi kuona tofauti gari ikiwa full AC au vioo chini".

Kwenye chombo changu tofauti ni insignificant, ambayo hata kugundua kwamba nimetumia mafuta mengi kwa sababu ya kutumia AC ni ngumu. Wewe stick na data za Google, sijazipinga.

Tupe pia experience yako kwenye gari lako, kwamba ukishusha vioo unapata 13km kwa lita, na ukiwasha AC unapata 10km kwa lita.
 
Mkuu kwa kifupi jibu halipo straight foward. AC ya gari unatumia nguvu kutoka kwenye engine,no maana hata unapowasha AC muungurumo huwa unabadilika. Kwa hiyo unatumia mafuta zaidi,hiyo ni sehemu ya kwanza...
Mimi karibu mara zote hufunga vioo na kuwasha AC heat kwa kutotaka upepo, na polollution.
 
Mkuu kwa kifupi jibu halipo straight foward. AC ya gari unatumia nguvu kutoka kwenye engine,no maana hata unapowasha AC muungurumo huwa unabadilika. Kwa hiyo unatumia mafuta zaidi,hiyo ni sehemu ya kwanza...
Nipo kwenye hii Field. Uliyosema yana ukweli kabisa.

Nashauri tu kwamba wewe unaetumia A/C hakikisha mfumo wake uwe katika hali nzuri.

Kuna kifaa kinaitwa Compressor huwa kina engage na kudisengage kutokana na demand ya ubaridi ndani ya gari sasa kama mfumo wa a/c haupo vizuri kufikisha ubaridi unaotakiwa inamaana compressor yako itaengage kwa muda mrefu sana au moja kwa moja na hivyo kuweka mzigo kwenye injini kwa muda mrefu.

Pia hakikisha unafunga vioo na hakikisha pia seals kwenye milango na sehemu zenye upenyo zipo madhubuti ili zisiingize hewa kutoka nje ambayo ni ya moto vitavyofanya uhitaji wa compressor kuengage kwa interval fupifupi.

Otherwise Mfumo wa A/C wa gari ukiwa madhubuti hautaongeza sana Fuel Consumption ya gari lako.
 
Mkuu kwa kifupi jibu halipo straight foward. AC ya gari unatumia nguvu kutoka kwenye engine,no maana hata unapowasha AC muungurumo huwa unabadilika. Kwa hiyo unatumia mafuta zaidi,hiyo ni sehemu ya kwanza...

Thanks sana brother umetoa uchambuzi safi sana, umenitoa ushamba
 
Kwangu sijawahi kuona tofauti gari ikiwa full AC au vioo chini. Tofauti niliyoiona ni pale vumbi linapojaa ndani ya gari baada ya kushusha vioo na pale gari inapokuwa safi ndani kwa kutumia AC muda wote. Naona ninatumia mafuta yaleyale tu ya laki na 20 hadi 50 kwa mwezi kulingana na misele.

Thanks sana brother kwa kunipa experience yako.
 
Watu wa ajabu sana! Kwa hiyo walioweka Ac kwenye gari walifanya makosa au...ukikshaambiwa gari yako inakula km/lt kadhaa unafikiri Ac ilitolewa au?
Nadhani unajua pia kuna (cars without factory A/C).
 
Back
Top Bottom