Matumizi ya dawa za kuandaa mwili kabla ya kubeba ujauzito: Nimetolewa ushamba

Matumizi ya dawa za kuandaa mwili kabla ya kubeba ujauzito: Nimetolewa ushamba

Strong ladg

Senior Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
170
Reaction score
445
Katika harakati za maisha nikakutana na mdada anatokea nchi fulani sitaitaja. Yule mdada alikuwa anakunywa dawa za kuongeza damu, folic acid, vitamin B supplements na nyingine sikuzitambua. Nikamuuliza" wewe ni mjamzito"? Akajibu hapana. Nikashangaa maana najua hizo dawa hutumiwa na wajawazito.

Akaniambia amejipanga kushika ujauzito miezi kadhaa ijayo hivyo anaandaa mwili uwe tayari kupokea mtoto.

Akanambia pia amebadilisha mtindo wa maisha kama vile kuacha pombe, kulala muda mrefu pamoja na kutumia vyakula vyenye mafuta kidogo na visivyochakatwa viwandani. Kwa kweli nilishangaa, sikuwahi kujua kuna watu wana huu utaratibu wa kuandaa mwili miezi kadhaa kabla ya kubeba ujauzito.

Je unadhani ni wakati mwafaka na sisi tuanze kupewa elimu hii na kuifanya sehemu ya maisha yetu? Je utamaduni wetu na mtindo wetu wa maisha vitaendana na watu kuandaa afya zao kabla ya kushika ujauzito?

Asante
 
Vyakula tunavyokula vina virutubisho vya kutosha..
Wengi wa wake zetu hawana changamoto hizo za upungufu wa virutubisho kama hao washindia mikate, chipsi na Coka.

Tahadhari: Epuka kumezameza madawa kwa influence za mitandaoni.
 
Mbona hiyo elimu ipo miaka mingi tu? Jaribu kutembelea kliniki ya mama na mtoto hasa kitengo cha uzazi wa mpango na majira utagundua mengi yaliyowazi wala hakuna siri hapo. 😳
 
Kuna raia mmoja wa kigeni aliniambia hata wababa watarajiwa hutumia baadhi ya supplements wakati wakijiandaa.
 
ephen_ hili darasa linakuhusu. Nataka siku ukimpata mtoto wa kiume, basi umuite TATE, na pia uhakikishe unajiandaa mapema kama huyu mdada aliyezungumziwa hapo juu ili mjukuu wangu awe na akili nyingi kama mimi babu yake. 😎
 
ananajiandaa kubeba wa kumpa anaye? raha ya kusoma kuwe na paper
 
wakati unalindaa lishangazi kitoto cha 2000s kinakuja unasema ngoja nionje fasta mara unaambiwa imo utajua hujui.
 
Kama wanawake wangekuwa wanajiandaa kimwili kama hivyo ulivyoeleza, then kwa pamoja mwanamke na mwanaume wanajiandaa kwa malezi ya mtoto, wanaandaa bajeti ya Prenatal, delivery, na post natal ingekuwa poa sana, kwa mapenzi ya Mungu mtoto anazaliwa akiwa na baraka zote na afya njema.
 
ndo maana watoto wajinga wajinga wanazidi kuwa wengi siku hizi
 
Kama wanawake wangekuwa wanajiandaa kimwili kama hivyo ulivyoeleza, then kwa pamoja mwanamke na mwanaume wanajiandaa kwa malezi ya mtoto, wanaandaa bajeti ya Prenatal, delivery, na post natal ingekuwa poa sana, kwa mapenzi ya Mungu mtoto anazaliwa akiwa na baraka zote na afya njema.
Ingekuwa raha sana. Mtoto anasubiriwa. Sio zile kauli za " wewe nae hukujua kama ulikuwa kwenye siku za hatari ?". Mtoto anakataliwa hata kabla hajazaliwa.
 
Ingekuwa raha sana. Mtoto anasubiriwa. Sio zile kauli za " wewe nae hukujua kama ulikuwa kwenye siku za hatari ?". Mtoto anakataliwa hata kabla hajazaliwa.
Movie ya BINTI kuna wale partners ambao walikuwa hawapati mtoto ila suala la kujiandaa walikua vizuri hadi nilivutiwa.
 
Back
Top Bottom