Bhangi
Majani ya bhangi huvutwa kama sigara pia inaweza kuchanganywa na vyakula na kuliwa.
Madhara yake ni tofauti kwa kila mtu. Kwa watu wengi hupumbaza kama pombe. Humfanya mtu kusahau au kuelewa mambo, kutoweza kuwasiliana vyema, na magonjwa mengine.
Walio na uraibu huongea wakivuta maneno na macho yao huwa kama yenye usingizi.
Crystal Meth
Methamphetamine ilitengezwa kutoka kwa Amphetamine na ina matokeo mamoja. Hupoteza hamu ya kula, kuongeza nguvu na kujiamini sana. Ina tengezwa kinyume cha sheria kote ulimwenguni
Huwa katika hali tofauti,y aweza vutwa, nuswa, kuliwa au kudungwa.
Methamphetamines humfanya mtu kuwa na tabia za kihalifu na kufanya vitu kwa mabavu.
Heroini
Huwa katika hali ya poda nyeupe au rangi ya mchanga. Hudungwa kwa sindano moja kwa moja kwenye damu,au hunuswa au kuvutwa kama sigara. Muda mfupi baada ya kutumia miili yao huwa mizito hisia zao hupotea.
Watumizi katika hatari ya kuitegemea kwa maisha yao ambapo ikikosekana kufa ni rahisi. Husababisha ugonjwa wa mapafu, moyo, na afya kudhoofika.
Kwa sababu ya kutumia sindano wamo hatarini mwa kuupata ugonjwa wa Ukimwi kwa sababu ya kutumia sindano moja.
Methadone ndio dawa inayosaidia wanaotumia kuwacha lakini pia inaweza kumfanya kutegemea dawa hii lazima maagizo ya daktari kufuatwa.
Kokeini
Rock kokeini ni bei rahisi na hupatikana kwa urahisi. Madhara yake ni kuwa humpa mtu msisimuko wa nguvu mwilini jambo linaloweza kuwaelekeza vijana kusuka na uhalifu au ngono bila kujikinga.
Huvutwa kwa kutumia kiko na baadhi ya vifaa vingine ni:
- Neli ya majaribio
- Bomba
- Waya
- Mifuko ya plastiki
- Kiberiti cha sigara
- Nyaya za stima
Dalili zinazoonyesha kuwa mtu anatumia kokeini:
- Kutokwa na kamasi
- Kutokwa damu puani
- Kupunguka uzito kwa haraka
- Kuzubaa
- Ushari
- Kujiamini zaidi
- Wasiwasi
- Mkakamavu
Rohypnol
Ni dawa inayofahamika ulimwenguni, hutumbukizwa katika kinywaji cha mtu hasa wasichana kisha kupoteza fahamu na kwenda kunajisiwa bila ya hata yeye mwenyewe kufahamu. Liwe onyo hasa unapokuwa katika vilabu vya pombe au sherehe popote, jihadhari dhidi ya kuwacha pombe yako bila mtu kuichunga. Huzidisha nguvu za pombe na kumlewesha mtu haraka.
Sukari
Sukari ni mchanganyiko wa madawa kama kokeini na heroini, ni dawa iliyo mfano wa poda, watumiaji hutajika kuwa na mrija ili wavute. Sukari sio bei ghali na wanaotumia hushindwa kuwacha matumizi yake