SoC01 Matumizi ya Simu na Afya ya Akili

SoC01 Matumizi ya Simu na Afya ya Akili

Stories of Change - 2021 Competition

Baba Swalehe

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2017
Posts
20,178
Reaction score
39,641
Tunaendelea na mada zetu za afya ya akili ambapo leo tutaangalia jinsi simu zinavyoathiri mfumo mzima wa akili na jinsi jamii inavyopeteza uwezo taratibu bila yenyewe kujijua na nini kinaweza kufanyika .

Tupo sasa katika ulimwengu wa kiteknolojia ambapo simu zimechukua nafasi ya vitu kama vile camera , redio saa , kalenda na hata vitabu na muda sio mrefu simu zitachukua hata nafasi ya ubongo , kwa sababu watu watakua hawafikirii tena kwa kina ila kila kitu itakua ni kukimbilia kwenda google kuangalia kwa kupitia simu zao .

Tafiti zinaonyesha kwamba watu wengi hutumia kila baada ya dakika nne kujihusisha na simu zao na kufanya vitu kama vile kujibu jumbe fupi , kupokea simu au kuperuzi na vitu vingine vingi vihusianavyo na simu , wengi wetu hata kama hakuna notification tutachukua simu na kuangalia chochote kama kuna message imeingia au hakuna au tutaingia kuangallia kitu chochote kile na hii ni moja ya dalili ya uraibu wa simu za mkononi kama ilivyo kwa pombe na vitu vingine na ukikosa kupata mambo ya mtandaoni kama vile instagram wengine hupata hasira na sonona hivyo kushindwa kufanya kazi zingine .

Madhara ya simu katika afya ya akili ni mengi tutayaangalia kwa uchache sana na nini kifanyike ile jamii iweze kukomboka katika tetemo kubwa linalokuja .

Tukianza na kifizikia simu hazitoi mionzi ambayo inaweza ku haribu ubongo wa binadamu kama wengi wavyofikiria au waliaminishwa katika hadithi mbali mbali za mtaani mionzi ya simu ipo katika ngazi ya ndogo ya mionzi( kwa lugha ya wenzetu huitwa low level non ionizing radiation ) kuweza hata kuharibu vinasaba vya mwili DNA , ila sasa madhara ya kutumia simu kupitiliza ni kwamba huleta kukosekana kwa uwiano sawa wa kemikali katika ubongo wa binadamu , katika maada zilizopita tuliona kwamba katika ubongo wa binadamu kuna kemikali mbali mbali ambazo zingine huleta furaha zingine maumivu na zingine nyingi na madhara ya ukosefu wa uwiano ni makubwa sana .

Matumizi ya Simu kupitiliza hupunguza kwa ujumla uwezo wa ubongo wa mtu kufikiria na kutatua changamoto zingine zilizopo katika maisha , kadri siku zinavyokwenda na tunavyotegemea taarifa zote kutoka kwenye simu tunapunguza uwezo wetu wa kiasili wa ubongo kutatua matatizo , unapotatua tatizo lolote mfano unafanya hesabu bila kifaa cha msaada nyuroni zilizopo kwenye ubongo hufanya miunganiko zenyewe kwa zenyewe kwa ufupi ni kwamba ubongo unakua unafanya mazoezi tofauti na kuupa kila saa taarifa ambazo zinafanya ubongo usitumie nguvu , sikatai simu ni nzuri zinaturahisishia mambo mbali mbali lakini matumizi yake yakizidi mtu hushindwa hata kufanya hesabu ya mbili mara nne mwenyewe kiufupi unakua mzembe sana

Matumizi ya simu kupitiliza kuperuzi kwenye mitandao ya kijamii kila saa huleta hali ya kutokujiamini na kuona labda umechelewa kufanya maendeleo na kwamba upo sana nyuma ya muda hii inaweza kupelekea kupata msongo mkubwa wa mawazo , unapita huko unakuta mtu kapost anakula kuku kavu na wewe hujala miezi minne unaumia pengine unaanza kujenga na chuki kwa huyo mtu kitu kikubwa ambacho watu hawafahamu ni kwamba kila mtu kwenye mitandao ya kijamii hupenda kuonyesha kwamba ana furaha ila ukweli huwa sio hivyo watu wana mawazo sana mtu utakayemwona amepost anaendesha hammer huwezi jua ana mkopo wa sh ngapi huko kwa hiyo kwa nini ujipe mawazo na upoteze uwezo wako wa kujiamini ?

Pia matumizi ya simu yamepunguza ile hali ya kushirikiana kwenye jamii mfano unatoka kazini unapitiliza moja kjwa moja kutumia simu yako hukai na watoto kuwauliza habari za shule hukai na majirani kuongea kuhusu mambo mbali mbali yanayotokea kwenye jamii husika ikuzungukayo

Matumizi ya simu kupitiliza kutokana na ukosefu wa uwiano wa kemikali mwilini hupelekea mtu kukosa usingizi kwa muda mrefu na sisi wataalamu wa afya huwa tunashauri mtu apate usingizi wa kutosha ili aboreshe afya yake ya akili , ukosefu wa usingizi huweza pelekea mtu kupata sonona na sonona tumeiangalia sana kwenye mada zilizopita , mtu anakosa usingizi hivyo mchana anashindwa kufanya kazi zake kwa umakini na ajabu ni kwamba hata huko kazini atashinda kwenye mitandao na jana kashoinda mpaka usiku wa manane kwenye simu au televisheni
na mwisho kabisa ni ajali za barabarani .

Je tufanye nini sasa kama wewe upo na uraibu wa kutumia simu kupitiliza , hatuwezi sema tuache kutumia simu kwa sababu simu zinaturahisishia wanadamu kazi mbali mbali ila tunatakiwa tujifunze namna ya kuishi na hizi simu na vifaa vingine vya kiteknolojia , kama upo kwenye uraibu kitu cha kwanza unaweza fanya ni kuzuia baadhi ya taarifa ambazo application huwa inakuletea mfano sio lazima kujua kila saa kwamba baba swalehe amependa picha yako instagram sababu ukienda kule utatumia muda mwingine kuangalia vitu vingine , pia unaweza kutenga muda wako wa siku maalumu kwa ajili ya kupita kwenye mitandao mbali mbali ya kijamii, ukishindwa kabisa itabidi utoe baadhi ya application zinazokutinga kwa muda na uzirudishe pale ambapo unaona kwa sasa unaweza kuzitawala.

Katika saikolojia mbinu mojawapo kubwa huwa inatumika katika kuondoa uraibu wa mtu ni kubadilisha kile kitu alikua anafanya kwa muda mrefu na kitu kingine mfano unaweza badilisha tabia yako ya kutumia simu kwa muda mrefu na ule muda unautumia kwa vitu vingine mfano kusoma vitabu , kucheza na watoto kuongea na ndugu na majirani au kufanya mazoezi

Mwisho kabisa niseme kwamba matumizi ya simu kupitiliza inaweza kuwa ni ishara mojawapo kubwa ya matatizo ya akili na unatumia simu kujiliwaza hivyo LINDA SANA UBONGO WAKO NDIO UNAOENDESHA KAZI ZOTE ZA MWILI PANGILIA VIZURI MATUMIZI YAKO YA SIMU

usisahau kupigia kura makala hii nzuri .
 
Upvote 13
Jaribu kuwa na marafiki unaokutana nao physically inasaidia kupunguza matumizi ya simu. Wengine wanatumia simu kama companion, hii ndiyo dunia yabutandawazi ni rahisi kushindwa ku balance ya kushare na ya kuhold.
 
Jaribu kuwa na marafiki unaokutana nao physically inasaidia kupunguza matumizi ya simu. Wengine wanatumia simu kama companion, hii ndiyo dunia yabutandawazi ni rahisi kushindwa ku balance ya kushare na ya kuhold.
Ndio ndio hii pia inasaidia sanaaa
 
Ku vote si ndio unaclick kwenye Ile icon ya ku subscribe?
Hapana mkuu unatumia web browser kuna sehemu chini kuna alama ya ^
Jaribu kuwa na marafiki unaokutana nao physically inasaidia kupunguza matumizi ya simu. Wengine wanatumia simu kama companion, hii ndiyo dunia yabutandawazi ni rahisi kushindwa ku balance ya kushare na ya kuhold.

Jaribu kuwa na marafiki unaokutana nao physically inasaidia kupunguza matumizi ya simu. Wengine wanatumia simu kama companion, hii ndiyo dunia yabutandawazi ni rahisi kushindwa ku balance ya kushare na ya kuhold.
Hutakiwi kutumia simu kila saa kama njia ya kureplace binadamu wenzako
 
Yaani muda sio mrefu tulikuwa tunazilaani hizi smart phone[emoji2297][emoji2297][emoji2297]
Yaani uraibu wa simu ni mbaya jamani.
 
Yaani muda sio mrefu tulikuwa tunazilaani hizi smart phone[emoji2297][emoji2297][emoji2297]
Yaani uraibu wa simu ni mbaya jamani.
Ni mbaya sana aisee

Inabidi tujifunze jinsi ya kuzicontrol
 
Ni mbaya sana aisee

Inabidi tujifunze jinsi ya kuzicontrol
Kuna mambo tumejizoesha bila simu hayawezekani najiuliza mbona kabla ya hizi simu mambo yaliwezekana vizuri tu? Kuamka lazima alarm, jambo fulani kulitekeleza basi unaweka reminder[emoji2297][emoji2297][emoji2297]
 
Kuna mambo tumejizoesha bila simu hayawezekani najiuliza mbona kabla ya hizi simu mambo yaliwezekana vizuri tu? Kuamka lazima alarm, jambo fulani kulitekeleza basi unaweka reminder
emoji2297.png
emoji2297.png
emoji2297.png
Uraibu wa simu ni mbaya sana espy
 
Tunaendelea na mada zetu za afya ya akili ambapo leo tutaangalia jinsi simu zinavyoathiri mfumo mzima wa akili na jinsi jamii inavyopeteza uwezo taratibu bila yenyewe kujijua na nini kinaweza kufanyika .

Tupo sasa katika ulimwengu wa kiteknolojia ambapo simu zimechukua nafasi ya vitu kama vile camera , redio saa , kalenda na hata vitabu na muda sio mrefu simu zitachukua hata nafasi ya ubongo , kwa sababu watu watakua hawafikirii tena kwa kina ila kila kitu itakua ni kukimbilia kwenda google kuangalia kwa kupitia simu zao .

Tafiti zinaonyesha kwamba watu wengi hutumia kila baada ya dakika nne kujihusisha na simu zao na kufanya vitu kama vile kujibu jumbe fupi , kupokea simu au kuperuzi na vitu vingine vingi vihusianavyo na simu , wengi wetu hata kama hakuna notification tutachukua simu na kuangalia chochote kama kuna message imeingia au hakuna au tutaingia kuangallia kitu chochote kile na hii ni moja ya dalili ya uraibu wa simu za mkononi kama ilivyo kwa pombe na vitu vingine na ukikosa kupata mambo ya mtandaoni kama vile instagram wengine hupata hasira na sonona hivyo kushindwa kufanya kazi zingine .

Madhara ya simu katika afya ya akili ni mengi tutayaangalia kwa uchache sana na nini kifanyike ile jamii iweze kukomboka katika tetemo kubwa linalokuja .

Tukianza na kifizikia simu hazitoi mionzi ambayo inaweza ku haribu ubongo wa binadamu kama wengi wavyofikiria au waliaminishwa katika hadithi mbali mbali za mtaani mionzi ya simu ipo katika ngazi ya ndogo ya mionzi( kwa lugha ya wenzetu huitwa low level non ionizing radiation ) kuweza hata kuharibu vinasaba vya mwili DNA , ila sasa madhara ya kutumia simu kupitiliza ni kwamba huleta kukosekana kwa uwiano sawa wa kemikali katika ubongo wa binadamu , katika maada zilizopita tuliona kwamba katika ubongo wa binadamu kuna kemikali mbali mbali ambazo zingine huleta furaha zingine maumivu na zingine nyingi na madhara ya ukosefu wa uwiano ni makubwa sana .

Matumizi ya Simu kupitiliza hupunguza kwa ujumla uwezo wa ubongo wa mtu kufikiria na kutatua changamoto zingine zilizopo katika maisha , kadri siku zinavyokwenda na tunavyotegemea taarifa zote kutoka kwenye simu tunapunguza uwezo wetu wa kiasili wa ubongo kutatua matatizo , unapotatua tatizo lolote mfano unafanya hesabu bila kifaa cha msaada nyuroni zilizopo kwenye ubongo hufanya miunganiko zenyewe kwa zenyewe kwa ufupi ni kwamba ubongo unakua unafanya mazoezi tofauti na kuupa kila saa taarifa ambazo zinafanya ubongo usitumie nguvu , sikatai simu ni nzuri zinaturahisishia mambo mbali mbali lakini matumizi yake yakizidi mtu hushindwa hata kufanya hesabu ya mbili mara nne mwenyewe kiufupi unakua mzembe sana

Matumizi ya simu kupitiliza kuperuzi kwenye mitandao ya kijamii kila saa huleta hali ya kutokujiamini na kuona labda umechelewa kufanya maendeleo na kwamba upo sana nyuma ya muda hii inaweza kupelekea kupata msongo mkubwa wa mawazo , unapita huko unakuta mtu kapost anakula kuku kavu na wewe hujala miezi minne unaumia pengine unaanza kujenga na chuki kwa huyo mtu kitu kikubwa ambacho watu hawafahamu ni kwamba kila mtu kwenye mitandao ya kijamii hupenda kuonyesha kwamba ana furaha ila ukweli huwa sio hivyo watu wana mawazo sana mtu utakayemwona amepost anaendesha hammer huwezi jua ana mkopo wa sh ngapi huko kwa hiyo kwa nini ujipe mawazo na upoteze uwezo wako wa kujiamini ?

Pia matumizi ya simu yamepunguza ile hali ya kushirikiana kwenye jamii mfano unatoka kazini unapitiliza moja kjwa moja kutumia simu yako hukai na watoto kuwauliza habari za shule hukai na majirani kuongea kuhusu mambo mbali mbali yanayotokea kwenye jamii husika ikuzungukayo

Matumizi ya simu kupitiliza kutokana na ukosefu wa uwiano wa kemikali mwilini hupelekea mtu kukosa usingizi kwa muda mrefu na sisi wataalamu wa afya huwa tunashauri mtu apate usingizi wa kutosha ili aboreshe afya yake ya akili , ukosefu wa usingizi huweza pelekea mtu kupata sonona na sonona tumeiangalia sana kwenye mada zilizopita , mtu anakosa usingizi hivyo mchana anashindwa kufanya kazi zake kwa umakini na ajabu ni kwamba hata huko kazini atashinda kwenye mitandao na jana kashoinda mpaka usiku wa manane kwenye simu au televisheni
na mwisho kabisa ni ajali za barabarani .

Je tufanye nini sasa kama wewe upo na uraibu wa kutumia simu kupitiliza , hatuwezi sema tuache kutumia simu kwa sababu simu zinaturahisishia wanadamu kazi mbali mbali ila tunatakiwa tujifunze namna ya kuishi na hizi simu na vifaa vingine vya kiteknolojia , kama upo kwenye uraibu kitu cha kwanza unaweza fanya ni kuzuia baadhi ya taarifa ambazo application huwa inakuletea mfano sio lazima kujua kila saa kwamba baba swalehe amependa picha yako instagram sababu ukienda kule utatumia muda mwingine kuangalia vitu vingine , pia unaweza kutenga muda wako wa siku maalumu kwa ajili ya kupita kwenye mitandao mbali mbali ya kijamii, ukishindwa kabisa itabidi utoe baadhi ya application zinazokutinga kwa muda na uzirudishe pale ambapo unaona kwa sasa unaweza kuzitawala.

Katika saikolojia mbinu mojawapo kubwa huwa inatumika katika kuondoa uraibu wa mtu ni kubadilisha kile kitu alikua anafanya kwa muda mrefu na kitu kingine mfano unaweza badilisha tabia yako ya kutumia simu kwa muda mrefu na ule muda unautumia kwa vitu vingine mfano kusoma vitabu , kucheza na watoto kuongea na ndugu na majirani au kufanya mazoezi

Mwisho kabisa niseme kwamba matumizi ya simu kupitiliza inaweza kuwa ni ishara mojawapo kubwa ya matatizo ya akili na unatumia simu kujiliwaza hivyo LINDA SANA UBONGO WAKO NDIO UNAOENDESHA KAZI ZOTE ZA MWILI PANGILIA VIZURI MATUMIZI YAKO YA SIMU

usisahau kupigia kura makala hii nzuri .
Ningekuwa na uwezo ningerudisha utaratibu wa mawasiliano kama zamanj,,,, visimu vidogo vya batani.. Kama mtandao kwenye compyuta tena cafe... Kiukweli sasa hivi jamii imeharibika sana pamoja na Mimi nilikuwa mmoja wapo singawa sasahivi nipo kwenye mapambano ya kutoka... Luna msemo unasema "technologia imekuja kutatua tatizo LA uchumi LA muda mrefu lakini imeleta janga LA akili na kisaikologia"
Sasa kama Akili za watu mbovu, huo uchumi utaletaje Tija kwa watu?
Ifike wakati tubadilike hasa waafrika tuachane na masmartphone hebu tuishi kama zamani na muda wetu tuutumie zaidi kwenye kazi... Unanunua zako computer desktop ama laptop unaweka ndani na siku ya mkononi kinokia Obama au visimu vya kufunua ambavyo having internet vyenye kazi ya kutuma SMS na kupiga simu tu... Jamii forum mpaka wikiend upate muda ama uende cafe kama huna kompyuta... Hata radha ya mtandao itakuja kwa kufanya vitu vya maana
Mi nawaambieni kufanya hivyo tutakuwa mbali sana kiafya na kiuchumi....
 
Back
Top Bottom