Matumizi ya Video Queens: Wasanii wa Bongo wanaboa

Sele Mkonje

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2011
Posts
643
Reaction score
845
Nimetoka kuangalia Video mpya ya Mr bluu "mboga saba" na nasikitika kusema kwamba sijaipenda sio kwamba nyimbo ni mbaya bali ni kwa haka katabia ka wasanii wa Bongo kuwaweka kwenye video Madem weupe(waarabu,wahindi,wazungu na wale wenye muonekano wa light skins). Hii inaonesha ni jinsi gani sisi watu weusi hatujikubali wenyewe na ndo mana sishangai kuona idadi ya wanawake wetu weusi wakijichubua ngozi zao.

Kila Msanii anataka ashoot na dem mweupe. Rejea video za Diamond, Alikiba,Ommy Dimpoz,Blue,Hamonaiza na wengine kibao. Hata hao wazungu wenyewd wanatushangaa kuona jinsi tunavyowanyenyekea. Mfano yule dem alioshuti "Bado" ya Hamonaiza ilitokea ajali kidogo basi dem akagoma, Wacha majamaa wampigie magoti kisa dem mweupe mpaka akakubali na dau wakapandishiwa.

ACHENI USHAMBA WASANII WA BONGO FLEVA..
====================

MREJESHO
 
Uko sahihi tena siku hiz wanatafuta machotara na wazungu kabisa
 



Ninyi bado mnafuatilia bongo flava??

Bora muwe mnaangalia mchiriku kuliko huo uchafu
 
Mbona kawaida sana hao watoto rangi ya sheshe wapo kila kona
Iringa
Tabora
Tanga
Dom
So na wao ni wa tz so mkiona hivyo ujue ni kawaida sana.
Kilosa mashombe kama hao wapo kibao
Ni wa tz jamani ni rangi tu.
 
Mbona kawaida sana hao watoto rangi ya sheshe wapo kila kona
Iringa
Tabora
Tanga
Dom
So na wao ni wa tz so mkiona hivyo ujue ni kawaida sana.
Kilosa mashombe kama hao wapo kibao
Ni wa tz jamani ni rangi tu.
majority ya watanzania ni black sidhan kama hao weupe wanazidi 5% ya population yote ya Tz. Pia inatoa taswira mbaya kuwafanya dada zetu kuona kuwa being white ndo uzuri. mziki wetu unatakiwa ureflect maisha yetu bt sadly haureflect chochote
 

Makala yako ina mantiki bro, ila kwa Alikiba utakuwa umekosea ye hana hiyo tabia, kwanza waga ni mgumu kutumia video Queen kwenye video zake, rejea mwana, chekecha, Aje na hizo za kitambo
 
bongo fleva kimbilio mnaonyesha ulimbukeni wenu
 
Bongo kila mtu ni msanii.
Hata mambo ya uhalisia yanapindishwa yaonekane meupe.
 

Duhhh kumbe mkuu ata kwa msanii ambae ametumia video Queen wa kigeni mara 1 nayy anakaa kwenye list yako, ata hivo huyo video Queen wa kwenye lupela ni black america na kwenye hii video kuna mabinti weusi kuliko yeye sema huyu alipata tu hiyo chance ya kuwa main model na pia video imeshutiwa marekani so huyo umuonae ndo black mwenyewe wa huko, anyway me nilizani unazungumzia wasanii ambao imekuwa kasumba kwao kutumia warembo unaowaongelea

Pia kitu kingine mziki ni kazi (biashara) so wao km wasanii ndo wanajua tofauti iko wapi kati ya mabinti black na white katika target zao, haiwezekani eti aturidhishe sisi then yeye asipate kile alichokuwa anakitarajia, na sio bongo tu, tunaona south Africa, Nigeria, ata nchi za magharibi video Queen wanaotumika wengi ni weupe, so kuna kitu nyuma ya watoto weupe, cc km washabiki kazi yetu ni kutoa support tu na kuenjoy mziki haya mengine ni yakiufundi zaidi. Mtazamo tu
 
kumbe lupela imeshutiwa unyamwezini na sio Sauz.?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…