KERO Matumizi ya vitambulisho vingi, kwanini kisitumike kitambulisho cha NIDA pekee?

KERO Matumizi ya vitambulisho vingi, kwanini kisitumike kitambulisho cha NIDA pekee?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Bususwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2021
Posts
468
Reaction score
1,116
Husika na mada tajwa hapo juu.

Tanzania ni Nchi ya ajabu sana kuwahi kutokea hapa Duniani, Tanzania ni Nchi ambayo bado iko nyuma sana na mambo ya teknolojia.

Tanzania tuna Kitambulisho cha Taifa, maarufu kwa jina la NIDA, Kwa mawazo yangu nilifikiri kwamba kitambulisho hiko kitabeba kila aina ya Kitambulisho kilicho chini ya taasisi za Serikali kuanzia na

1. Leseni ya Udereva
2. Kadi ya Bima ya NHIF
3. Kadi ya mwanachama wa NSSF au PSSSF
4. Kadi ya Mpiga kura
5. Kitambulisho cha kazi
6. Cheti chakuzaliwa
7. Cheti cha Ndoa
8. Cheti cha Darasa la Saba, Kidato Cha Nne na Sita, Chuo Kikuu, Cheti, Stashahada, Stashahada ya Juu Shahada, Uzamili na Uzamivu
8. Mengineyo

Lakini jambo la ajabu kabisa, unakuta mtu anatembea na makadi mengi au kuna kadi kaziweka nyumbani kama vile ni takataka sasa,maana yanakua mengi hadi kero. Hapo bado sijaweka kadi za banks, mfano mtu una account zaidi ya moja kwenye bank,hapo napo pia unakua umebeba kadi za banks zakutosha.

Swali langu nyinyi watu wa serikali, hivi ni kwa nini mmeshindwa kabisa kufanya kadi ya NIDA ikabeba baadhi ya kadi za taasisi za serikali? Kuna haja gani ya mimi kuwa na NIDA,kuwa na kadi ya NHIF,Leseni ya udereva,kadi ya mfuko wa Jamii.kadi ya kupigia kura? Wakati hivi vitu vyote vilipaswa kubebwa na NIDA

Mnakera sana, na mbaya zaidi ikitokea vikapotea hivi vitu,kuvipata kwake ni kazi kweli kweli, mfano upoteze NIDA au Passport ,mambo yako mengi yanasimama.

Tunaomba hili suala lifanyiwe kazi
 
Nadhani itakuwa ngumu kuwa hivyo kwa sababu, sio watanzania wote watahitaji kuwa na NSSF, kadi ya bima ya afya, udereva, kazi inayohitaji kuwa na kitambulisho n.k
 
Nadhani itakuwa ngumu kuwa hivyo kwa sababu, sio watanzania wote watahitaji kuwa na NSSF, kadi ya bima ya afya, udereva, kazi inayohitaji kuwa na kitambulisho n.k
NIDA ibebe hivyo vyote kwa mtu ambaye anavitu vingi,kama hana hizo mambo nyingi basi
 
Husika na mada tajwa hapo juu...

Tanzania ni Nchi ya ajabu sana kuwahi kutokea hapa Duniani, Tanzania ni Nchi ambayo bado iko nyuma sana na mambo ya teknolojia....

Tanzania tuna Kitambulisho cha Taifa, maarufu kwa jina la NIDA, Kwa mawazo yangu nilifikiri kwamba kitambulisho hiko kitabeba kila aina ya Kitambulisho kilicho chini ya taasisi za Serikali kuanzia na
1. Leseni ya Udereva
2. Kadi ya Bima ya NHIF
3. Kadi ya mwanachama wa NSSF au PSSSF
4. Kadi ya Mpiga kura
5. Kitambulisho cha kazi
6. Mengineyo

Lakini jambo la ajabu kabisa, unakuta mtu anatembea na makadi mengi au kuna kadi kaziweka nyumbani kama vile ni takataka sasa,maana yanakua mengi hadi kero... Hapo bado sijaweka kadi za banks, mfano mtu una account zaidi ya moja kwenye bank,hapo napo pia unakua umebeba kadi za banks zakutosha.

Swali langu nyinyi watu wa serikali, hivi ni kwa nini mmeshindwa kabisa kufanya kadi ya NIDA ikabeba baadhi ya kadi za taasisi za serikali??? Kuna haja gani ya mimi kuwa na NIDA,kuwa na kadi ya NHIF,Leseni ya udereva,kadi ya mfuko wa Jamii.kadi ya kupigia kura?? Wakati hivi vitu vyote vilipaswa kubebwa na NIDA

Mnakera sana, na mbaya zaidi ikitokea vikapotea hivi vitu,kuvipata kwake ni kazi kweli kweli, mfano upoteze NIDA au Passport ,mambo yako mengi yanasimama....

Tunaomba hili suala lifanyiwe kazi
NIDA zilizo nyingi zina taarifa za bima ya afya,mpiga kura,cheti cha kuzaliwa,vyeti vya darasa la saba,kidato cha IV na kidato cha VII.Changamoto ni kwamba si wote waliviandika kwenye fomu ya NIDA.Ndiyo maana ili kuepuka usumbufu utatakiwa uwe navyo vinapohitajika.
 
NIDA zilizo nyingi zina taarifa za bima ya afya,mpiga kura,cheti cha kuzaliwa,vyeti vya darasa la saba,kidato cha IV na kidato cha VII.Changamoto ni kwamba si wote waliviandika kwenye fomu ya NIDA.Ndiyo maana ili kuepuka usumbufu utatakiwa uwe navyo vinapohitajika.
Bora iwe hivyo ndugu yangu,itasaidia sana kutokuwa na lundo la kadi na vyeti,mfano NIDA iwe na kila kitu,wakikuita kwenye usaili,wakiweka tu namba yako ya NIDA kwenye system inaleta particulars za mtahiniwa kuanzia kuzaliwa kwake hadi kusoma kwake
 
Kwanza itapunguza gharama za kuboresha Kila wakati. Mtanzania mmoja unabeba kadi ya bima ya afya, Kitambulisho cha mpiga kura, leseni sijui kadi ya utaifa na nyingine nyingi tu.

Serikali nashauri Ije na kadi Moja yenye taarifa zote hizo mtu anapokwenda ofisi yeyote anapata huduma. Chukulia mfano hii kadi ya mpiga kura inavoboreshwa serikali inaingia gharama kubwa bila sababu wakati huyo mtu ana Kitambulisho cha Taifa au namba ya NIDA.
 
Wakikusikia katika hili waambie na mtandao wa simu uwe mmoja, waamue tuhakiki mara moja kwa ulimi maana kila kukicha madudu hayaishi.
 
Kwa kweli ni changamoto sana,
kwa mfano South Africa, kila kitu insurance, drivers licence, bank cards
Yaani unaweza kwenda bank na kitambulisho cha mwananchi, (nida) ukapata pesa bila card,
Unaweza kwenda hosp na hiyo nida ya hapa ukapata huduma,
Nilikuwa na jamaa yangu kasahau drivers licence tukakutana na police mwenye kuelewa akauliza nida no ID akaiita on air itakuja na daraja lako la licence valid or expired, akapewa ticket na onyo
Labda bus ticket hapo ndio utakuwa na kadi ya ile company ile mambo
mengine hauhitaji huo mzigo wa cards sababu hata wallet itakuwa full
Na sasa wamefanya card nyingi kuwa virtual unadownload an app na zinakuwa kwenye simu
Wahusika waliopewa hiyo dhamana wanabidi waliangalie hilo
Hauhitaji kuwa na mfuko wa macard
 
Nadhani itakuwa ngumu kuwa hivyo kwa sababu, sio watanzania wote watahitaji kuwa na NSSF, kadi ya bima ya afya, udereva, kazi inayohitaji kuwa na kitambulisho n.k
Inaeza kutengenezwa ya digital ambayo taarifa znaeza kuongezwa na kufutwa mkuu
 
Back
Top Bottom