Matunda na mboga ni nzuri kiafya lakini ni hatari

Matunda na mboga ni nzuri kiafya lakini ni hatari

MOSHIFST

Senior Member
Joined
Jun 4, 2014
Posts
136
Reaction score
262
Kula matunda na mboga fresh ni nzuri kwa afya yako lakini kuna vimelea vinavyoweza dhuru afya yako.

Jifunze dondoo za usalama wa chakula ufurahie chakula chako.

☞Matunda 🍓🍎🍉🍌na 🥬🥗 huongeza virutubisho kwenye mlo wako ambavyo hukusaidia kujikinga na magonjwa ya moyo,kiharusi na baadhi ya kansa.Kwa upande mwingine,kuchagua chakula cha matunda,mboga,jamii ya karanga na vyakula vingine dhidi ya chakula chenye kalori nyingi inaweza kusaidia kuratibu uzito wako.

Lakini wakati mwingine matunda na mboga ghafi/mbichi (zisizopikwa) hubeba vimelea hatari kwa afya, kama vile Salmonella, Escherichia coli na Listeria, ambavyo vinaweza kusababsha wewe na familia yako kuumwa.Nchini Marekani karibia nusu ya magonjwa/Maradhi yasababishwayo na chakula (foodborne illnesses) yanasabishwa na vimelea vilivyopo kwenye matunda/mboga mbichi (fresh produce)

Chakula salama zaidi ni kile kilichopikwa; na kinachofuata ni kile kilichooshwa.Furahia matunda na mboga zisizopikwa wakati ukichukua hatua ili kuepuka maradhi yasababishwayo na chakula (foodborne illiness) wakati mwingine yanajulikana kama "food poisoning"

1.SOKONI/SUPERMARKET
Ukiwa sokoni
-Chagua matunda/mboga zisizo na michubuko au majeraha
-Chagua matunda/mboga iliyoweka katika mazingira ya ubaridi (refrigerated).Mtaani kuna matunda yaliyokatwa huwa yanauzwa,epuka kununua hayo km huna uhakika na usafi wako ni hatari unaweza ukaumwa magonjwa ya tumbo
-Tenganisha matunda/mboga na nyama mbichi,kuku na vyakula vya baharini unapokua unaweka kwenye kikapu chako.

2.NYUMBANI.
-Nawa mikono
-safisha vifaa vya jikoni
-Osha matunda na mboga kwenye maji yanayotiririka
-Kata au toa sehemu za tunda au mboga zilizoharibika au kuchubuka.
-Tenganisha matunda na chakula kingine kama nyama mbichi nk
-Weka kwenye friji

Food poisoning
Mtu yoyote anaweza akapata food poisoning lakini kuna watu kwenye baadhi ya makundi wako hatarini zaidi kuumwa na kupata maradhi yanayoweza sabisha kifo.Makundi hayo ni:-

-Watoto chini ya miaka 5
-Wanawake wajauzito
-Watu wenye miaka 65 na zaidi na
- Watu wenye kinga dhaifu.

Kama wewe au yeyote unayemjali yupo kwenye hatari ya kupata foodborne illness,ni muhimu kuchukua hatua ili kuzuia.

Sambaza ujumbe huu kutoa elimu zaidi

Ujumbe huu umeandaliwa na Food Elimu Tanzania

Kwa msaada kuhusu biashara ya chakula hasa
-Usindikaji
-Usajili TBS
-Kufahamu viwango vya ubora (quality standards) kwa masoko ya Ulaya na Marekani
-Ukaguzi na uuandaji mfumo wa ubora (Food Quality system)
-Utafiti na kuboresha bidhaa pamoja na huduma zingine

Wasiliana na Food Elimu kupitia.

E-mail:foodelimu gmail.com

WhatsApp/Call: +255 784 8676 26.

Food Elimu; Enhancing quality and Safety for Local produces
 
Wasabato waliona mbali sana miaka 40 iliyopita kukataa kula vyakula feki(visivyo vyaasili), kunywa soda, majani ya chai, kitimoto n.k.

Soma kitabu kinaitwa TUREJEE BUSTANINI EDENI ili ujue kwanini Mungu aliona ni vyema sana Binadamu tule vyakula vya mizizi, mboga mboga, matunda ya mbegu mbegu, samaki na maji mengi.
 
Wasabato waliona mbali sana miaka 40 iliyopita kukataa kula vyakula feki(visivyo vyaasili), kunywa soda, majani ya chai, kitimoto n.k.

Soma kitabu kinaitwa TUREJEE BUSTANINI EDENI ili ujue kwanini Mungu aliona ni vyema sana Binadamu tule vyakula vya mizizi, mboga mboga, matunda ya mbegu mbegu, samaki na maji mengi.
Mungu alitutengenezea chakula kama dawa.Lakini binadamu tuligeuza dawa kuwa ndio chakula.
Watu wanapunguza uzito kwa kutumia dawa badala ya chakula.
 
Wasabato waliona mbali sana miaka 40 iliyopita kukataa kula vyakula feki(visivyo vyaasili), kunywa soda, majani ya chai, kitimoto n.k.

Soma kitabu kinaitwa TUREJEE BUSTANINI EDENI ili ujue kwanini Mungu aliona ni vyema sana Binadamu tule vyakula vya mizizi, mboga mboga, matunda ya mbegu mbegu, samaki na maji mengi.
Aizaki Ndodi yupo?
 
Hii ni moja ya thread bora na muhimu ila haina wachangiaji
 
wadau ili uweze kula mboga mboga zenye usalama hasa zile zisizopikwa, ni vizuri baada ya kuziosha uzisuze na maji yaliyochanganywa na vinegar. sijui vinegar inaitwaje kiswahili lakini inapatikana madukani kwa urahisi kabisa. changanya vinegar na maji kwa ratio ya 1:3 kisha mboga zako zioshe kwa vinegar baada ya kuwa umeziosha kwa maji safi hapo awali. ndipo zikatekate na kuzila. Nina hakika vimelea na magonjwa yatokanayo utasiyasikia wengine wakisimulia.
 
wadau ili uweze kula mboga mboga zenye usalama hasa zile zisizopikwa, ni vizuri baada ya kuziosha uzisuze na maji yaliyochanganywa na vinegar. sijui vinegar inaitwaje kiswahili lakini inapatikana madukani kwa urahisi kabisa. changanya vinegar na maji kwa ratio ya 1:3 kisha mboga zako zioshe kwa vinegar baada ya kuwa umeziosha kwa maji safi hapo awali. ndipo zikatekate na kuzila. Nina hakika vimelea na magonjwa yatokanayo utasiyasikia wengine wakisimulia.
Vinegar ni Siki
 
Back
Top Bottom