Matunda ya kinga kwa viongozi wetu yameanza kuonekana kupitia Spika wa Bunge

Matunda ya kinga kwa viongozi wetu yameanza kuonekana kupitia Spika wa Bunge

Lord OSAGYEFO

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2021
Posts
3,085
Reaction score
4,890
Hakika sasa ni dhahiri watanzania wamejua kwanini hayati magufuli na viongozi wa Mihimili walijiwekea kinga ya kutoshtakiwa.

Nilikuwa najiuliza kwanini wanajiwekea kinga wanataka kufanya kitu gani kibaya kwa watanzania?

Sababu za kujiwekea kinga zimeanza kujulika kupitia spika wa bunge kukiuka kwa makusudi katiba ya nchi kwa kuwakingia kifua wabunge fake 19 waliofukuzwa na chama chao cha Chadema na kuendelea kulipwa mishahara ambayo ni kodi za masikini. Kinachoshangaza Serikali ipo kimya wananchi ndio wanalalamika.

Katiba yetu ipo wazi kuwa mbunge anapofukuzwa uanachama ubunge wake unakoma. Mifamo hai ipo kwa wabunge 8 wa CUF na mbunge wa CCM walifukuzwa uanachama na vyama vyao Spika huyu huyu aliwafukuza bungeni kwa mbwembwe nyingi, leo iweje kwa sifa zile zile za wale wabunge kwanini hataki kuwafukuza wabunge 19?

Tunamwomba rais samia asilifumbie macho suala hili kwani ni ukiukwaji wa katiba unaofanywa na spika kwa makusudi na kuichafua serikali.
 
Pamoja na NIA NJEMA ya Mama Samia kutaka kurekebisha mengi lakini atafika mahali vingine atafunika kombe tuu.. Kwa maana ya kwamba yeye naye bado ni sehemu ya mfumo uleule

Walewale
 
Viongozi wetu wengi uzalendo wao Ni sifuri.Unakuwaje mzalendo wa taifa lako huku unavunja katiba ya nchi yako waziwazi?
 
Pamoja na NIA NJEMA ya Mama Samia kutaka kurekebisha mengi lakini atafika mahali vingine atafunika kombe tuu.. Kwa maana ya kwamba yeye naye bado ni sehemu ya mfumo uleule
Mkuu umesema kweli kabisa.

Naona hata Jobo ana dalili zote za kumvimbia Mama kwenye baadhi ya issues, ikiwemo hili hawa wabunge 19.
 
Pole sanatoa na mada na hongera kwa angalau kusema. Wengine wanashindwa kusema lolote wanaumia mioyoni mwao. Walitarajia kutoa adhabu kwenye uchaguzi wakafeli. Sasa hawana namna nyingine. Hawataki sikia chochote sasa kuhusu Siasa, suala ambalo ni baya zaidi.
 
Back
Top Bottom