Mauaji ya JF Kennedy - rais wa 35 wa USA : Namna yalivyotokea!

Naomba uwe unatag kila unapoandika Toledo jingine,mie ni mpenz wa haya mambo
 
Tuendelee...

MAUAJI YA JF KENNEDY - RAIS WA 35 WA USA : NAMNA YALIVYOTOKEA

Sehemu ya sita.

Jim Marrs : Halafu mara tu, Lee Harvey Oswald akatokea.
James Files : Asubuhi iliyofuata Lee Harvey Oswald alikuja pale. Wakati alipogonga mlango, nilifungua na nikashtuka kumuona, kwasababu sikufikiri kuna yeyote anaejua nilipo isipokuwa kwa hao watu wengine wawili.

Swali : Kwanini unadhani Phillips ndiye pekee angeweza kumuagiza Lee Harvey Oswald pale?
Jibu : Kwasababu Charles Nicoletri hakuwahi kamwe kukutana na Lee Harvey Oswald.

Swali : Hakuwahi kumfahamu?
Jibu : Hakuwahi kumfahamu.

Swali : Unasema ulishtuka kumuona, kwani ulikuwa ukimfahamu Lee Harvey Oswald?
Jibu : Ndio, nilikuwa nikimfahamu Lee Harvey Oswald kabla ya happ.

Swali : Ulimfahamu kivipi?
Jibu : Nilimfahamu kutokea kwenye operesheni za nyuma tulizofanya na David Phillips wakati nikisafirisha bunduki 'semi automatic 45 caliber submachine' nikizipeleka Clinton, Louisiana. Nafikiri zilikuwa zikitengenezwa na 'Knoxville Arms'. Sio zile 'Thomson' za zamani, zilifanana na 'Thompson submachine gun', ila hazikuwa Thompson. Zilikuwa tu ni 'semi automatic' na zilitengenezwa kwa gharama ndogo tu.

Swali : Ulikutana vipi na Lee Harvey Oswald? Nani alikutambulisha?
Jibu : Nilikutana na Lee Harvey Oswald kwa kupitia David Atlee Phillips. Nilipoteremka Clinton, Louisiana alinitambulisha kwa Lee.

Swali : Uelewa wako juu ya Phillips kuwa pia mdhibiti wa Oswald kwa CIA ukoje?
Jibu : Nilijua hilo nilipoteremka kule. Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa Phillips kunitambulisha kwa Lee Harvey Oswald na akanielekeza kuwa Lee anaweza kuaminika na yeye ndio mdhibiti wa Lee.

Swali : Kwahiyo ndivyo ulivyofahamu. Huko ndiko neno lilikotokea kwa Oswald kuja kukutana na wewe Dallas?
Jibu : Hivyo ndivyo akili ya kawaida ilivyoniambia, mtu pekee ambaye angeweza kumtuma Lee Harvey Oswald, alikuwa David Atlee Phillips. Na nilipofungua mlango na kumwona Oswald pale, nilipata mshtuko flani hivi, kwasababu sikujua kama alijua nilikuwa pale. Na kwahivyo nikauliza : Lee umekuja kufanya nini hapa? Kwasababu nilishtuka, unajua.
Akasema : Nimeshauriwa kuja hapa na kukaa kidogo na wewe na kuona kama kuna kitu naweza kukusaidia. "Kunisaidia?" Akasema : Ndio, kuna mtu anataka nikutembeze kwenye haya maeneo.
Na mimi nikasema : Sawa, ingia ndani. Hivyo akaingia ndani na tukakaa na kuongea na nikasema : Nisubiri kwa dakika chache. Na nilikuwa kijana na mtundu kidogo kwa wakati ule na nilikuwa nimetoka kuoga na nilikuwa nikichana nywele na nilikuwa na kamera pale, hivyo nikamwambia Lee : Hey, nipige picha kadhaa nikiwa hapa Texas!

Na hivyo Oswald akanipiga picha kadhaa kisha akasema : Acha nichukue mkanda nikakutengenezee picha! Hapana, hapana, nikasema, nitatumia mkanda wote kupigia picha. Kwahiyo hivyo ndio nilipata picha kadhaa, ambazo watu wamekuwa wakiniulizia hivi karibuni.

Swali : Ilikuwa kamera gani? Yakwako au...?
Jibu : Kamera yangu. Ila alitaka kuchukua mkanda awapatie watu ili wafyatue picha. Ila nilisema : Hapana, hapana!

Swali: kwanini hukuruhusu mkanda uende?
Jibu : Huwa nafanya kazi zangu mwenyewe!

Swali : Oswald alifikaje hapo kwenye 'motel'?
Jibu : Alikuja akiendesha gari - Falcon ya bluu. Ford Falcon

Swali : Unakumbuka lilikuwa toleo la mwaka gani?
Jibu : Hapana, sikumbuki. Halikuwa jipya, lilishatumika miaka kadhaa.

Swali : Mmm, hivyo alikuwa anaweza kuendesha gari?
Jibu : Ndio, alikuwa anaweza kuendesha. Aliponikuta Clinton, Louisiana, alikuwa akiendesha ....aah... nataka kusema gari aina ya Chevrolet, inaweza kuwa Ford, ilikuwa ni 'pick-up', acha niiweke hivi; ilikuwa ni pick- up ya zamani. Tulikuwa tukiweka silaha mwisho wa bodi na kuzifunika kwa zulia.

Swali : Ilikuwa na rangi gani? Unaweza kukumbuka rangi ya hiyo pick-up?
Jibu : Naamini ilikuwa ya kijani. Ilikuwa kweli ....Sijui, chafu, iliyochokachoka, ya kijani, vyovyote unavyotaka kuiita. Kijani iliyokolea, unajua, haikuwa imeoshwa kwa muda mrefu na ilikuwa na kutu kibao. Hiyo ndiyo njia nzuri ya kuielezea.

Swali : Kwahivyo, wewe na Lee Oswald mliendesha gari kuzunguka Dallas?
Jibu : Tuliendesha kuzunguka Dallas, Lee Harvey Oswald na mimi, tulizunguka Dallas kwa siku tano mpaka kabla ya mauaji. Sikumuona Lee Harvey Oswald asubuhi ya siku ya mauaji.
Ila kabla ya hapo Lee Harvey Oswald alikuwa na mimi kila siku. Tulizunguka akanionyesha mitaa mbalimbali, maeneo mbalimbalo. Ni yeye aliyenipeleka sehemu fulani kusini mashariki mwa Mesquite pale, jirani na jalala kubwa. Tulienda kufanya majaribio, alisema : Hakuna atakayekubugudhi ukiwa hapa.

Kwasababu nilitaka kurekebisha vipimo vya darubini, unajua, sio tu kwa 'Fireball' ila kwa silaha nyingine pia. Na nilipokuwa pale nikipiga risasa na kutoa maganda ya risasi, Lee alikuwa akiyaokota na kuyashika kwenye mkono wake. Kwasababu sikutaka kuacha maganda ya risasi nyuma na niko 'busy' napiga risasi, hivyo nikamwangalia Lee na nikasema, "Lee, okota hayo maganda".

Na hicho ndicho alichofanya. Aliyaokota na akabaki nayo. Nikarekebisha darubini zangu, nikapangilia vitu vizuri, nikarudisha vitu kwenye gari na tukarudi kwenye gari.
Tulikuwa tukiendesha gari na nilitaka makutano ya barabara na reli, nilitaka kusubiri nijue ni muda gani treni zinapita, nilitaka kujua ni treni za abiria au za mzigo.
Kama zingesimama, makutano yangezuiliwa kupita. Mitaa ambayo barabara zake haziendelei, kazi za ujenzi zilizokuwa zikiendelea, sehemu makutano yote ya barabara yalipo, sehemu taa zote za kuongozea magari zilipo, muda gani taa zinabaki na mwanga mwekundu. Nilitaka kujua hizi taarifa zote ndogondogo.

Itaendelea....
 
Mbona stori umeishia njiani
 

Toka mwaka Jana au na wewe ulikufa
 
Jion the Navy to see the World '' John Kennedy ''
After he's graduated from The Havard University joined the Us Naval Force.
 
John F. Kennedy alikuwa Rais wa 35 wa Marekani kwa kipindi cha mwaka 1961 mpaka 1963 alipouwa kwa kupigwa risasi na Lee Harvey Oswald aliyekuwa mwanajeshi mstaafu wa Marekani.

Huyu ndiye mwanasiasa ambaye kifo chake kimeacha conspiracy theories/nadharia tata nyingi zaidi, hizi ni baadhi tu.

1. Israel;
Wa-Israeli walihusika baada ya kusemekana angekuwa kikwazo kwa mpango wao wa silaha za nuclear.

2.Ukomunisti na vita baridi;
Kikundi cha wahafidhina ndani ya CIA kilichokuwa kinachukia sana Ukomunisti na Castro kilihusika baada ya kuona haweki nguvu inayotakiwa kupambana na Ukomunisti.

3. UFO, NASA na CIA;
Inasemekana Kennedy alitaka files/taarifa za UFO( Unidentified Flying Objects)/Aliens zilizokusunywa na shirikia la anga la Marekani ambazo zilikiwa zimefichwa na CIA, siku 10 baadaye akapigwa risasa.

4. Wakomunisti wa USSR;
Kuna wanaodai muuaji wa Kennedy, Lee Oswald alitumwa na Warusi katika uhasama wa vita baridi, wanaunganisha story jinsi Lee alivyopata misukosuko ya kisheria jeshini, ajira yake ilivyokatizwa jeshini, akahamia Belarus na kuoa Mrusi kabla ya kurudi kuja kufanya hayo mauaji.

5. Mafia wa Chicago;
Wapo wanaodai Mafia wa Chicago walihusika pakubwa kumuingiza madarakani na walichukizwa vibaya na maamuzi yake ya kushughulika vikali na makundi ya uhalifu wa kupanga/mafia yaliyokuwa na nguvu sana kipindi hicho hivyo wakaamua kumuaa.

Hizi ni baadhi tu ya nadharia, bado zipo nyingine zikimuhusisha muuaji, silaha, mazingira n.k. Hata hivyo Serikali ya Marekani ilitoa taarifa rasmi baada ya uchunguzi wa tume maalum kwamba muuaji aliuhusika mwenyewe kwa sababu zake binafsi anazozifahamu mwenyewe, huo ndio msimamo wa serikali ya mpaka leo.

Lee Harvey Oswald aliuwa kwa kupigwa risasi siku mbili baadaye na mwananchi mwenye hasirika kali katika sehemu ya chini ya kuegesha magari Makao makuu ya Polisi Dallas wakati wanampeleka kwenye gari kumuhamishia remande nyingine. Katika siku 2 za mahojiano alikataa kabisa kuhusika na mauaji ya Kennedy na polisi mwingine aliyeuwawa katika tukio hilo.
 
Hivi uchunguzi kuhusu mauaji ya JFK ulishindikana kabisa ?
 
Wewe unachojua ni kipi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…