Makuku Rey
JF-Expert Member
- Dec 31, 2013
- 3,497
- 3,823
Kwako mrisho mpoto,
Imekuwa ni muda sasa toka tukupe nauli,pengine tingo alikupitiluiza kituo.
Maana umepita muda sasa,pengine uliogopa kushuka kwa sababu kulikuwa na mvua tena ya mafuriko ya damu na nyama.
Kama umepitiliza,ukifanikiwa kukutana na mwanzilishi wa taifa au mzimu wake.
Mwambie ile nyumba aliyoiacha yenye vijana wavivu,sasa ina vijanana wachapakazi na waoga.
Na sasaivi wanaogopa zaidi ushuru na makoro.
Msisitizie zaidi huyu baba wa kambo ameshindwa kutunza kitabu chake,amefuta sehemu za aya zake tena kwa damu.
Kibaya zaid njaa imetamalaki ndani ya nyumba,mpaka ng'ombe wanakula udongo.
Mashamba yote yamewekwa uzio,watu wamehamia shamba moja liliachwa wazi ili kunusuru matumbo yao.
Mwambie huku wameibuka wadudu wapya na wanakula mazao ya aina moja tuu
Mwisho kabisa koroboi tuliyokuwa nayo imeisha mafuta na kidumu tulikupa ww mpoto ukawekea maji ulipoondoka.
By Mauki J.S
copied&by [HASHTAG]#Makuku[/HASHTAG]
Imekuwa ni muda sasa toka tukupe nauli,pengine tingo alikupitiluiza kituo.
Maana umepita muda sasa,pengine uliogopa kushuka kwa sababu kulikuwa na mvua tena ya mafuriko ya damu na nyama.
Kama umepitiliza,ukifanikiwa kukutana na mwanzilishi wa taifa au mzimu wake.
Mwambie ile nyumba aliyoiacha yenye vijana wavivu,sasa ina vijanana wachapakazi na waoga.
Na sasaivi wanaogopa zaidi ushuru na makoro.
Msisitizie zaidi huyu baba wa kambo ameshindwa kutunza kitabu chake,amefuta sehemu za aya zake tena kwa damu.
Kibaya zaid njaa imetamalaki ndani ya nyumba,mpaka ng'ombe wanakula udongo.
Mashamba yote yamewekwa uzio,watu wamehamia shamba moja liliachwa wazi ili kunusuru matumbo yao.
Mwambie huku wameibuka wadudu wapya na wanakula mazao ya aina moja tuu
Mwisho kabisa koroboi tuliyokuwa nayo imeisha mafuta na kidumu tulikupa ww mpoto ukawekea maji ulipoondoka.
By Mauki J.S
copied&by [HASHTAG]#Makuku[/HASHTAG]