Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
MAULIDI SHEIN MWANAMAPINDUZI, ''TRADE UNIONIST'' NA MWANA-ASP...USHAMSIKIA?
Mazishi yana hulka ya kuwakutanisha watu waliopoteana kwa miaka.
Leo nimebahatika kukutana na Mzee Maulidi Sheni sasa ana umri wa miaka 93.
Mara ya mwisho kukutana na Maulid Shein ilikuwa mwaka wa 2008 niko na Dr. Harith Ghassany ndiyo kaja Tanga katika siku zake za mwisho kukamilisha utafiti wake wa historia ya Zanzibar uliopelekea kuandika kitabu, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' ambayo ni historia ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka wa 1964 ambayo kabla yake hakupata kutokea mwandishi kuandika kwa namna alivyofanya Dr. Ghassany.
Ikutoshe kuwa kitabu kina kurasa 497 kiasi cha kumuogopesha yeyote aliye mvivu wa kusoma lakini kumtia hamu yule apendae kusoma.
Wakati wa utafiti wa kitabu hiki kwa upande wa Tanganyika na hasa mjini Tanga na Dar es Salaam sehemu muhimu za mipango ya mapinduzi nilikuwa mara nyingi niko pembeni ya Daktari kama dereva wake wa kumkimbiza huku na kule.
Kwa ajili hii basi nimemfaidi sana Dr. Ghassany kwa kushuhudia nyakati zake za furaha na wakati mwingine akiwa na huzuni kubwa kwa yale aliyosikia yamepitika katika mapinduzi ya Zanzibar alipoelezwa na wale walioshiriki katika kuiangusha serikali ya Sheikh Mohamed Shamte .
Nimemwona Daktari kwa mara ya kwanza akiwa katika simanzi mchana kwa mara ya kwanza Kisosora Tanga nyumbani kwa Mzee Mohamed Omari Mkwawa nilipompeleka kumkutanishanae.
Mzee Mkwawa jina lake lingine maarufu ni ''Tindo'' alilopewa na Mzee Karume wakati wa kupigania uhuru wa Zanzibar.
Mkwawa siku ile katika kikao chao cha kwanza alikuwa kamfungulia Daktari yale ambayo hakuwa amepata kuyasikia popote au kusoma kokote si katika maktaba kubwa za Marekani kama Library of Congress au Uingereza Rhodes House Oxford.
Aliyosikia kutoka kwa Mzee Mkwawa yalimyong'onyeza kiasi Dr. Ghassany alikuwa na dua yake akipenda kisoma kila mara, ''Mola wangu ikiwa kitabu hiki kitaleta maelewano kwa Wazanzibari kijaalie kikamilike lau kama si hivyo na kipotelee mbali.''
Nimemuona Daktari akiwa katika furaha kubwa akiwa pembeni ya Mzee Mkwawa Kipumbwi maili chake kutoka Tanga asubuhi moja Mzee Mkwawa alipompeleka hapo kumuonyesha sehemu ilipokuwa kambi ya Wamakonde kutoka mashamba ya mkonge ya Sakura.
Hawa Wamakonde walikuwa msaada mkubwa katika kuipindua serikali ya Sheikh Mohamed Shamte.
Siku ile na asubuhi ile TIndo alimwonyesha Daktari pango kubwa lililofunikwa na kichaka kikubwa ambako chini ya kichaka kile pangoni vyombo viliegeshwa mchangani na kutolewa kiza kikiingia kuanza safari kwenda Zanzibar yeye Mkwawa na jeshi lake wakiwa abiria ndani ya chombo.
Furaha ya Daktari ilikuwa furaha ya mwanasayansi yeyote katika maabara anapofikia tamati ya kupata ufumbuzi wa tatizo lilikuwa likiwahangaisha wanasayansi wote.
Turejee kwa Mzee Maulidi Sheni.
Safari ya kumtafuta Maulidi Sheni ilifungwa Tanga na kiongozi wa msafara kuja Dar es Salaam alikuwa Mzee Mkwawa mimi nikiwa dereva.
Kituo chetu cha kwanza ulikuwa Msikiti wa Mzee Mwinjuma Mwinyikambi, Mwananyamala na haukuchukua muda mrefu tukampata Mzee Maulidi Sheni.
Maulidi Sheni na Mzee Mkwawa walikuwa hawajaonana miaka mingi sana.
Wanamapinduzi hawa mnyororo wao uliokuwa ukiwaunganisha ulikatika baada ya kifo cha Mzee Karume mwaka wa 1972.
Maulidi Sheni ndiye mtu wa kwanza kumfahamisha Mzee Mkwawa kuhusu kambi ya Sakura kama sehemu ya kutayarisha Mapinduzi ya Zanzibar.
Safari hii ya kumtafuta Mzee Maulidi Sheni ilikuwa kupata na yeye kauli yake kuhusu Kipumbwi na Sakura.
Daktari hakuwa anapenda taarifa nusu nusu za upande mmoja.
Vipi leo nimebahatika kukutana na Mzee Maulidi Sheni?
Tumefiwa na mzee wetu Ashraf Himidi na nilipofika msibani nikamuona Salim Msoma mmoja kati ya wasomi makini na bingwa wa lugha ya Kiingereza kukizungumza na kukiandika.
Salim kakaa na watu wengine na baada ya kusalimiana akanionyesha mtu mmoja mtu mzima sana, ''Unamjua huyu?''
Nimemtazama yule mzee lakini sikuweza kumtambua na yule mzee akawa ananiangalia lakini kwa ule mtazamo wake nikajua na yeye pia hakunitambua.
Lakini niliahidi pia kwa ajili ya utu uzima Maulidi Sheni hakuwa hadhir.
''Maulid Sheni huyo mwanamapinduzi, anayo mengi sana lakini hataki kusema. Sasa ana miaka 93,'' Salim alinifahamisha.
Hapo hapo sura ya Mauidi Sheni ikarejea katika kumbukumbu zangu.
Miaka 12 ilikuwa sasa imepita toka siku ile nilipomwendesha Daktari kutoka Tanga hadi Msikiti wa Mwinjuma Mwinyikambi, Mwananyamala kwenda kumtafuta tukiongozwa na Mzee Mohamed Omari Mkwawa.
Salim Msoma hakuwa anafahamu kuwa Maulidi Sheni alishazungumza na Dr. Harith Ghassany mazungumzo ambayo naamini ndiyo yalikuwa ya mwisho katika mstari mrefu wa wale walioeleza waliyoyajua kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar.
Nilikuwepo siku Mzee Maulidi Sheni alipokuwa anahojiwa na Daktari tumekaa ufukweni Sea View Dar es Salaam na kwa utulivu mkubwa nilisikiliza mazungumzo yao.
Baadhi ya yale ambayo alieleza katika historia ya mapinduzi yalitufadhaisha sote.
Baada ya mahojiano haya nilipobaki na Daktari tulisema mengi kuhusu yale tuliyosikia.
Baada ya mahojiano haya Dr. Ghassany alirejea Washington DC kukamilisha kitabu.
Nimefurahi sana kukutana tena na Mzee Maulid Sheni na ingawa utu uzima umemtopea na hakuweza hata kuitikia salamu yangu na muda wote mfupi niliokuwa pale na Salim Msoma yeye alikuwa kama hayupo, kanzu yake nyeupe aliyovaa ilikuwa safi imemkaa vema pamoja na kofia yake ya Kiomani.
Allah atuhifadhie mzee wetu na amjaalie siha njema.
PICHA;
Kushoto Mohamed Omari Mkwawa, Maulidi Sheni na Mwandishi Tindo kakishika kitabu, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.''
Mazishi yana hulka ya kuwakutanisha watu waliopoteana kwa miaka.
Leo nimebahatika kukutana na Mzee Maulidi Sheni sasa ana umri wa miaka 93.
Mara ya mwisho kukutana na Maulid Shein ilikuwa mwaka wa 2008 niko na Dr. Harith Ghassany ndiyo kaja Tanga katika siku zake za mwisho kukamilisha utafiti wake wa historia ya Zanzibar uliopelekea kuandika kitabu, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' ambayo ni historia ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka wa 1964 ambayo kabla yake hakupata kutokea mwandishi kuandika kwa namna alivyofanya Dr. Ghassany.
Ikutoshe kuwa kitabu kina kurasa 497 kiasi cha kumuogopesha yeyote aliye mvivu wa kusoma lakini kumtia hamu yule apendae kusoma.
Wakati wa utafiti wa kitabu hiki kwa upande wa Tanganyika na hasa mjini Tanga na Dar es Salaam sehemu muhimu za mipango ya mapinduzi nilikuwa mara nyingi niko pembeni ya Daktari kama dereva wake wa kumkimbiza huku na kule.
Kwa ajili hii basi nimemfaidi sana Dr. Ghassany kwa kushuhudia nyakati zake za furaha na wakati mwingine akiwa na huzuni kubwa kwa yale aliyosikia yamepitika katika mapinduzi ya Zanzibar alipoelezwa na wale walioshiriki katika kuiangusha serikali ya Sheikh Mohamed Shamte .
Nimemwona Daktari kwa mara ya kwanza akiwa katika simanzi mchana kwa mara ya kwanza Kisosora Tanga nyumbani kwa Mzee Mohamed Omari Mkwawa nilipompeleka kumkutanishanae.
Mzee Mkwawa jina lake lingine maarufu ni ''Tindo'' alilopewa na Mzee Karume wakati wa kupigania uhuru wa Zanzibar.
Mkwawa siku ile katika kikao chao cha kwanza alikuwa kamfungulia Daktari yale ambayo hakuwa amepata kuyasikia popote au kusoma kokote si katika maktaba kubwa za Marekani kama Library of Congress au Uingereza Rhodes House Oxford.
Aliyosikia kutoka kwa Mzee Mkwawa yalimyong'onyeza kiasi Dr. Ghassany alikuwa na dua yake akipenda kisoma kila mara, ''Mola wangu ikiwa kitabu hiki kitaleta maelewano kwa Wazanzibari kijaalie kikamilike lau kama si hivyo na kipotelee mbali.''
Nimemuona Daktari akiwa katika furaha kubwa akiwa pembeni ya Mzee Mkwawa Kipumbwi maili chake kutoka Tanga asubuhi moja Mzee Mkwawa alipompeleka hapo kumuonyesha sehemu ilipokuwa kambi ya Wamakonde kutoka mashamba ya mkonge ya Sakura.
Hawa Wamakonde walikuwa msaada mkubwa katika kuipindua serikali ya Sheikh Mohamed Shamte.
Siku ile na asubuhi ile TIndo alimwonyesha Daktari pango kubwa lililofunikwa na kichaka kikubwa ambako chini ya kichaka kile pangoni vyombo viliegeshwa mchangani na kutolewa kiza kikiingia kuanza safari kwenda Zanzibar yeye Mkwawa na jeshi lake wakiwa abiria ndani ya chombo.
Furaha ya Daktari ilikuwa furaha ya mwanasayansi yeyote katika maabara anapofikia tamati ya kupata ufumbuzi wa tatizo lilikuwa likiwahangaisha wanasayansi wote.
Turejee kwa Mzee Maulidi Sheni.
Safari ya kumtafuta Maulidi Sheni ilifungwa Tanga na kiongozi wa msafara kuja Dar es Salaam alikuwa Mzee Mkwawa mimi nikiwa dereva.
Kituo chetu cha kwanza ulikuwa Msikiti wa Mzee Mwinjuma Mwinyikambi, Mwananyamala na haukuchukua muda mrefu tukampata Mzee Maulidi Sheni.
Maulidi Sheni na Mzee Mkwawa walikuwa hawajaonana miaka mingi sana.
Wanamapinduzi hawa mnyororo wao uliokuwa ukiwaunganisha ulikatika baada ya kifo cha Mzee Karume mwaka wa 1972.
Maulidi Sheni ndiye mtu wa kwanza kumfahamisha Mzee Mkwawa kuhusu kambi ya Sakura kama sehemu ya kutayarisha Mapinduzi ya Zanzibar.
Safari hii ya kumtafuta Mzee Maulidi Sheni ilikuwa kupata na yeye kauli yake kuhusu Kipumbwi na Sakura.
Daktari hakuwa anapenda taarifa nusu nusu za upande mmoja.
Vipi leo nimebahatika kukutana na Mzee Maulidi Sheni?
Tumefiwa na mzee wetu Ashraf Himidi na nilipofika msibani nikamuona Salim Msoma mmoja kati ya wasomi makini na bingwa wa lugha ya Kiingereza kukizungumza na kukiandika.
Salim kakaa na watu wengine na baada ya kusalimiana akanionyesha mtu mmoja mtu mzima sana, ''Unamjua huyu?''
Nimemtazama yule mzee lakini sikuweza kumtambua na yule mzee akawa ananiangalia lakini kwa ule mtazamo wake nikajua na yeye pia hakunitambua.
Lakini niliahidi pia kwa ajili ya utu uzima Maulidi Sheni hakuwa hadhir.
''Maulid Sheni huyo mwanamapinduzi, anayo mengi sana lakini hataki kusema. Sasa ana miaka 93,'' Salim alinifahamisha.
Hapo hapo sura ya Mauidi Sheni ikarejea katika kumbukumbu zangu.
Miaka 12 ilikuwa sasa imepita toka siku ile nilipomwendesha Daktari kutoka Tanga hadi Msikiti wa Mwinjuma Mwinyikambi, Mwananyamala kwenda kumtafuta tukiongozwa na Mzee Mohamed Omari Mkwawa.
Salim Msoma hakuwa anafahamu kuwa Maulidi Sheni alishazungumza na Dr. Harith Ghassany mazungumzo ambayo naamini ndiyo yalikuwa ya mwisho katika mstari mrefu wa wale walioeleza waliyoyajua kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar.
Nilikuwepo siku Mzee Maulidi Sheni alipokuwa anahojiwa na Daktari tumekaa ufukweni Sea View Dar es Salaam na kwa utulivu mkubwa nilisikiliza mazungumzo yao.
Baadhi ya yale ambayo alieleza katika historia ya mapinduzi yalitufadhaisha sote.
Baada ya mahojiano haya nilipobaki na Daktari tulisema mengi kuhusu yale tuliyosikia.
Baada ya mahojiano haya Dr. Ghassany alirejea Washington DC kukamilisha kitabu.
Nimefurahi sana kukutana tena na Mzee Maulid Sheni na ingawa utu uzima umemtopea na hakuweza hata kuitikia salamu yangu na muda wote mfupi niliokuwa pale na Salim Msoma yeye alikuwa kama hayupo, kanzu yake nyeupe aliyovaa ilikuwa safi imemkaa vema pamoja na kofia yake ya Kiomani.
Allah atuhifadhie mzee wetu na amjaalie siha njema.
PICHA;
Kushoto Mohamed Omari Mkwawa, Maulidi Sheni na Mwandishi Tindo kakishika kitabu, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.''