Nilipata tatizo la jino langu kutoboka, kiasi kwamba nilishauriwa na daktari wa meno kung'oa, baada ya daktari kung'oa jino pamekuwa na maumivu kwenye pengo na kwenye fidhi karibu na pengo pale ninapotafuna chakula, ingawa kama sitafuni kitu chochote sipati maumivu yoyote, mwanzo nilifikiri ni mamivu ya kawaida baada ya kung'oa jino, lakini hii ni siku ya nne nahisi maumivu kwenye fidhi pembeni na pengo kila napo tafuna chakula. Msaada tafadhali, nipo sehemu ambayo siwezi kupata huduma ya meno kwa sasa