Mavazi yapi yalikua maarufu sana kipindi chako cha Kununuliwa NguonChristMass?

Mavazi yapi yalikua maarufu sana kipindi chako cha Kununuliwa NguonChristMass?

bryan2

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2016
Posts
3,323
Reaction score
4,679
Tujikumbushe leo kipindi cha kununuliwa nguo za Christmass ni Mavazi gani yalikua maarufu sana anzia nguo mpaka viatu...

Enzi zangu mavazi yaliyokua maarufu sana ni Suruali za TOKYO,SAVCO,Shati za Van Basten na Bahamas na Viatu ilikua ni Dingi hawana Uwezo(DH) na Njumu kama vile maradona...nk Mzazi alikua asipokununulilia kati ya viwalo tajwa ni kununa na kulia siku nzima unaeza kususia hata chakula,Ilikua ni mwendo wa kulala ndani siku nzima.

Mbaya zaidi ukute watoto wa mtaa wa karibu wamenunuliwa nguo mpya.

Tukumbushe na wewe Mavazi aina gani yalikua maarufu sana Enzi zako.
 
We hizi jeans za Savco na Tokyo ni za juzi juzi hapa miaka ya 1992 hadi 1996 hivi.

Enzi zetu Christmas tulikuwa tunapiga suruali za Michael Jackson.
Shikamoo...ndo Zile Pekosi/masarawili/bwaga/juu pima chini kadiria izo zijafanikiwa kuvaa zaidi kuona kwenye Video za michael jackson na kusoma kwenye vitabu Ngengemkeni mitomingi(Penzi kitovu cha Uzembe)
 
Suruali za timbaland, zikiwa na mifuko mifuko mpaka magotini tu inaitwa timbaland.
-pensi nyanya
-ribbon ya kichwa kama kina nelly, lil bow wow na fabulous, pamoja na fulana kubwa kupita mwili ndo ubitoz
 
Suruali za timbaland, zikiwa na mifuko mifuko mpaka magotini tu inaitwa timbaland.
-pensi nyanya
-ribbon ya kichwa kama kina nelly, lil bow wow na fabulous, pamoja na fulana kubwa kupita mwili ndo ubitoz
Hahahahaa na bega moja chini na kakitambaa nyuma ya mfuko wa suruali...kweli tumetoka mbali
 
We hizi jeans za Savco na Tokyo ni za juzi juzi hapa miaka ya 1992 hadi 1996 hivi.

Enzi zetu Christmas tulikuwa tunapiga suruali za Michael Jackson.
michael jackoni ni ya miaka ya hiyo kweli, ila nyuma kidoogo ya hapo kulikuwa na mashati yanaitwa juliana
 
Winger,bio act,wacko jacko miaka hiyo ilikuwa balaa chini ni clipper au Kawasaki lakuchumpa lakuparama.
 
Hata sijui nilikuwa Monduli nachunga ngombe ya msee
Habari noo!!basi hapo ulikua umevaa rubega sidaiii na moka chinii napigia ngishu tu muluzii[emoji2] [emoji2] [emoji2]
 
Back
Top Bottom