Mawakala wa mpira wa miguu wenye mkwanja mrefu duniani

BilioneaPATIGOO

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2012
Posts
12,320
Reaction score
11,327
Mpira wa miguu haujakamilika bila kuwepo mawakala. Wao ni watu pekee wanaodhibitishwa na FIFA kusimama kama "mtu kati" katika uhamisho wa mchezaji na makubaliano ya mikataba yao. Hata hivyo mchezaji bado anaendelea kua "boss" na anaweza kumtimua wakala wake kazi muda wowote.

Leo hii biashara ya kuwakilisha wachezaji imekua biashara nzuri sana, "super agents'" kama akina Mendes wameibuka na wanatengeneza pesa NYINGI SANA zaidi ya hata klabu za mpira zinaponunua ama kuuza wachezaji wake.

Hawa hapa ndio wako kwenye chati katika upande wa PESA kupitia commision walizopata tokea waanze kua mawakala wa wachezaji tofauti tofauti haswa wa barani ulaya.


6. Jose Otin- Bilioni 59 za kitanzania



Ame base sana La Liga na ni mtu muhimu huko ligi ya La Liga na amekua wakala wa wachezaji wengi ambao ni wahispania ambao ni Pedro, Vitolo, Torres Fernando, Jesus Navas, Raul Garcia na Nacho Monreal.

5. Volker Struth- Bilioni 77 za kitanzania.


Klabu yoyote inayotaka mchezaji yeyote kutoka Ligi ya Ujerumani maarufu kama Bundesliga lazima kwa.udi na uvumba umtafute huyu jamaa ili kukamilisha dili. Wateja wake ni Marco Reus, Mario Gotze, Toni Kroos, Benedikt Howedes, Sidney Sam, Omer Toprak, Gonzalo Castro, na Josip Drmic.

4. Mino Raiola- Bilioni 97 za Kitanzania



Mino Raiola ni super agent. Huyu alipiga hela sana uhamisho wa Paul Pogba kwenda Man Utd kutokea Juventus na Lukaku pia. Wateja wake ni kama Paul Pogba, Henrikh Mkhitaryan, Blaise Matuidi, Zlatan Ibrahimovic, Maxwell, Romelu Lukaku, Mario Balotelli

3. Jonathan Barnett- Bilioni 119 za Kitanzania



Linapokuja wachezaji mahiri na wakubwa wa Premier League basi huyu ndo mwenyewe...alipiga pesa nyingi usajili wa Bale kwenda Madrid. Wateja wake ni Gareth Bale, Joe Hart, Wojciech Szczesny, Scott Sinclair, Luke Shaw, Rafael, Glen Johnson, Phil Jagielka, Adam Lallana, Ashley Cole, Sylvain Distin, Patrick Roberts, Richard Wright.


2. Jorge Mendes- Bilioni 172 za Kitanzania


Jorge Mendes bila shaka ndie wakala maarufu duniani, inasemekana ana zaidi ya pesa hii anayotajwa ameingixa kupitia madili makubwa ya uhamisho wa wachezaji...yeye ni wakala kwa wachezaji na hata makocha wenye majina makubwa kama Cristiano Ronaldo, James Rodriguez, Eliaquim Mangala, Pepe, Ricardo Carvalho, Fabio Coentrao, Diego Costa, Thiago Silva, Tiago, Radamel Falcao, Angel di Maria, David de Gea, Jose Mourinho

1. Constantin Dumitrascu- Bilioni 242 za Kitanzania


Constantin Dumitrascu ndie tajiri zaidi kwa sasa, ana kampuni yake inaitwa Mondial Sports Management iliyoko Ujerumaniby , na ni juzi tu ameweka kibindoni pesa kibao za usajili wa Coutinho kwenda Barca akitokea Liverpool...! Ni wakala mkubwa wa wachezaji kama Edinson Cavani, Philippe Coutinho, Douglas Costa, Nemanja Matic, Dimitri Payet, N’Golo Kante, Raphael Varane, na Olivier Giroud.
 
Hivi Mkuu ,wakala ndio dalali?


Ndio hivyo hivyo mwanangu asikwambie mtu. Kwa mtazamo wangu wakala namchukulia kama pimp tu. Ni sawa na na madalali wa mnadani, wanachoangalia ni kupiga pesa tu. Ukiingia kichwa kichwa utajijua mwenyewe.
 
Ndio hivyo hivyo mwanangu asikwambie mtu. Kwa mtazamo wangu wakala namchukulia kama pimp tu. Ni sawa na na madalali wa mnadani, wanachoangalia ni kupiga pesa tu. Ukiingia kichwa kichwa utajijua mwenyewe.
Hata mm nadhani ,maana biashara yao kubwa ni hao wachezaji,bila wao hakuna wakala
 
Hata mm nadhani ,maana biashara yao kubwa ni hao wachezaji,bila wao hakuna wakala
Kila mtu anamtegemea mwenzake maana kila mtu anahitaji Huduma ya mwingine ni Sawa na madalali wa Bank Bila dalali bank haijauza mali ya mteja alieshindwa kulipa mkopo na bila bank dalali ajaingiza kipato ivyo wote wanategemeana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…