Sabi Sanda
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 409
- 31
Wakuu,
Wakati tukisubiri ripoti ya Tume ya Profesa Sifuni Mchome inayochunguza sababu ya wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2012 kufeli sana katika mitihani yao ya kumaliza kidato cha nne, naomba nipendekeze yafuatayo:-
1. Wanafunzi watakaokuwa wakifaulu mitihani ya kumaliza darasa la saba ambao watapata angalau alama 160 kati ya 250, Serikali iwasamehe kulipa ada na michango ya kidato cha kwanza pindi wajiungapo na elimu ya Sekondari katika shule za Serikali.
2. Kila mwanafunzi wa Sekondari ambaye ataamua kuchukua masomo ya Sayansi angiapo kidato cha tatu, asamehewe kulipa ada kwa sharti kuwa wastani katika masomo yake ya kidato cha tatu na nne usiwe chini ya maksi 41. Iwapo atapata wastani chini ya 41 lakini zaidi ya maksi 30 alipe nusu ada. Na iwapo wastani wake utakuwa chini ya maksi 30 inashauriwa alipe ada kamili pamoja na kwamba atakuwa anachukua masomo ya Sayansi.
3. Kwa Wanafunzi ambao watakuwa hawachukui masomo ya Sayansi nao wasamehewe kulipa ada mwaka unaofuata iwapo wastani wao katika mwaka uliopita utakuwa si chini ya maksi 41 katika masomo yao.
4. Wanafunzi wote ambao wastani wao katika masomo yao ya kumaliza kidato cha tatu utakuwa si chini ya maksi 41, Serikali iwasamehe kulipa ada kwa ajili ya kufanya mitihani ya kumaliza kidato cha nne ambayo hulipwa NECTA.
Jioni njema kwenu wote.
Wakati tukisubiri ripoti ya Tume ya Profesa Sifuni Mchome inayochunguza sababu ya wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2012 kufeli sana katika mitihani yao ya kumaliza kidato cha nne, naomba nipendekeze yafuatayo:-
1. Wanafunzi watakaokuwa wakifaulu mitihani ya kumaliza darasa la saba ambao watapata angalau alama 160 kati ya 250, Serikali iwasamehe kulipa ada na michango ya kidato cha kwanza pindi wajiungapo na elimu ya Sekondari katika shule za Serikali.
2. Kila mwanafunzi wa Sekondari ambaye ataamua kuchukua masomo ya Sayansi angiapo kidato cha tatu, asamehewe kulipa ada kwa sharti kuwa wastani katika masomo yake ya kidato cha tatu na nne usiwe chini ya maksi 41. Iwapo atapata wastani chini ya 41 lakini zaidi ya maksi 30 alipe nusu ada. Na iwapo wastani wake utakuwa chini ya maksi 30 inashauriwa alipe ada kamili pamoja na kwamba atakuwa anachukua masomo ya Sayansi.
3. Kwa Wanafunzi ambao watakuwa hawachukui masomo ya Sayansi nao wasamehewe kulipa ada mwaka unaofuata iwapo wastani wao katika mwaka uliopita utakuwa si chini ya maksi 41 katika masomo yao.
4. Wanafunzi wote ambao wastani wao katika masomo yao ya kumaliza kidato cha tatu utakuwa si chini ya maksi 41, Serikali iwasamehe kulipa ada kwa ajili ya kufanya mitihani ya kumaliza kidato cha nne ambayo hulipwa NECTA.
Jioni njema kwenu wote.