Mawazo ya ccm kuhusu idadi ya waliotoa maoni kuhusu serikali tatu ni ya kihuni

Mawazo ya ccm kuhusu idadi ya waliotoa maoni kuhusu serikali tatu ni ya kihuni

KYAMTUNDU

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2013
Posts
1,820
Reaction score
295
Ndugu zangu, nimekuwa niwasikiliza sana watanzania wenzetu hasa wale makada, wanachama, mashabiki na wapenzi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuhusu idadi ya watu waliotoa maoni kwenye Tume ya Kukusanya Maoni iliyoongozwa na Jaji Mstaafu Joseph Sinde Warioba. Watanzania wenzetu hawa wamekuwa wakielekeza utii wao kwenye “IDADI” ya watanzania waliotoa maoni kuhusu uhitaji wa serikali (siyo nchi) tatu. Na sababu kubwa za kupendekeza muundo huo zimeoneshwa kwenye Viambatanisho vya Tume uk.248-249 Hoja yao kubwa ni kwamba wananchi sawa na asilimia 15% ya watanzania 323, 001 waliotoa maoni HAWAWEZI kuwa wawakilishi wa MAONI ya wananchi-ni idadi ndogo! Sasa naomba makada hawa walioishiwa hoja wajibu maswali yafuatayo: 1. Je, ni halali wajumbe 630 (0.000014% ya watanzania wote ) wa Bunge la Katiba kufanya uamuzi kwa niaba ya watanzania 44, 928,923 (NBS:2013) na mawazo yao yakakubaliwa?!
2. Je, ni halali kwa Jakaya Mrisho Kikwete aliyepata kura 5, 276,827 (0.24% ya watu milioni 22 waliojiandikisha mwaka 2010) kuwa Rais halali aliyechaguliwa na wananchi?

Sasa CCM wameongeza “upuuzi” kwa kuyagawa maoni hayo kwa kigezo cha “mahali” maoni hayo yalikotolewa. Leo katika kipindi cha Tuongee Asubuhi cha Star TV, nimemsikia KADA maarufu (japo anaonekana anatumia sana nguvu badala ya hoja) Christopher Ole Sendeka akisema Maoni ya kutaka serikali tatu yalitolewa Kigoma, na Pemba! CCM wanaopinga kuigawa nchi katika serikali tatu, wanaona ni heshima kuyagawa maoni kwa kuangalia mahali yalikotoka! Huu ni upuuzi. Hata hivyo nimeona ni vyema kuelekeza maswali yafuatayo kwa wenzetu wa CCM:
1. Je, ni halali kwa Dk. Mohamed Shein kuwa Rais halali wa Zanzibar wakati asilimia kubwa ya kura zake 179,809 (ZEC 2010) zilitoka Unguja?
2. Dk. Shein ni Rais wa Zanzibar au Rais wa Unguja?!

CCM walete hoja, wasifiche vichwa na kuacha viwiliwili nje.
 
Nawewe kwa akili yako unaona sawa asilimia 15 ya watu laki tatu ndio yabadili muundo wa serikali kutoka 2 kwenda 3? Tatizo wenye akili mbovu mnataka kutengeneza katiba ya kuitoa ccm madarakani na syo katiba ya kuleta mabadiliko ya kiuchumi na ustawa wa watanzania kwa miaka mingine 50 na zaidi, hapo mmekwama lazima mtakumbana na visiki maana ccm nacho ni chama chenye wanachama na wapenzi wake
 
Kwa kutaja chama na muda uliokwishapita tangu uweke uzi huu na hizo inference basing on representative ya sample,area na cluster!!!!!

Ukimya huu unasema kitu!!!!
 
Nawewe kwa akili yako unaona sawa asilimia 15 ya watu laki tatu ndio yabadili muundo wa serikali kutoka 2 kwenda 3? Tatizo wenye akili mbovu mnataka kutengeneza katiba ya kuitoa ccm madarakani na syo katiba ya kuleta mabadiliko ya kiuchumi na ustawa wa watanzania kwa miaka mingine 50 na zaidi, hapo mmekwama lazima mtakumbana na visiki maana ccm nacho ni chama chenye wanachama na wapenzi wake

Na watu laki tatu unakubali maoni yao kuwakilisha the rest of population????!!!!
Hata kama ni qualitative sidhani kama saturation utaipata!!!!

Hoja ya wajumbe wa bunge la katiba unaikalia???!!!
Ukiweka suala la sampling hapa kwa uwazi i doubt kama bunge litaendelea
 
Nilikuwa nikimtazama Sendeka kwa umakini sana.Kwa kweli inahuzunisha sana.Kama kweli hayo ndiyo yatakuwa mawazo ya wale wanaotuongoza na makada makini wa CCM basi no matter why we are poor. Hauwezi tegemea mind ya aina ya Sendeka iwe mbunge utegemee miracles.
 
Nawewe kwa akili yako unaona sawa asilimia 15 ya watu laki tatu ndio yabadili muundo wa serikali kutoka 2 kwenda 3? Tatizo wenye akili mbovu mnataka kutengeneza katiba ya kuitoa ccm madarakani na syo katiba ya kuleta mabadiliko ya kiuchumi na ustawa wa watanzania kwa miaka mingine 50 na zaidi, hapo mmekwama lazima mtakumbana na visiki maana ccm nacho ni chama chenye wanachama na wapenzi wake
Mbona huoji Kikwete alipigiwa kura ngapi kati ya watanzania 46 milioni mpaka awe rais?jibu hilo ndiyi nitakuona una akili siyo boga
 
Nilikuwa nikimtazama Sendeka kwa umakini sana.Kwa kweli inahuzunisha sana.Kama kweli hayo ndiyo yatakuwa mawazo ya wale wanaotuongoza na makada makini wa CCM basi no matter why we are poor. Hauwezi tegemea mind ya aina ya Sendeka iwe mbunge utegemee miracles.

Enlightenment is underway viongozi wasio fikiria uwezo wa akili wa hadhira wataumbuka sana!!!
 
Sidhani kama umeelewa hoja ya msingi ya mleta mada...

Nawewe kwa akili yako unaona sawa asilimia 15 ya watu laki tatu ndio yabadili muundo wa serikali kutoka 2 kwenda 3? Tatizo wenye akili mbovu mnataka kutengeneza katiba ya kuitoa ccm madarakani na syo katiba ya kuleta mabadiliko ya kiuchumi na ustawa wa watanzania kwa miaka mingine 50 na zaidi, hapo mmekwama lazima mtakumbana na visiki maana ccm nacho ni chama chenye wanachama na wapenzi wake
 
-Sendeka

-Serukamba

-Ummy mwalimu

-Simba chawene

-Pindi chana

-makonda

hawa viumbe ni wapuuzi kupita kiasi wakisimamiwa na kuongozwa na

1. Endrew Chenge-mzee wa vijisenti

2. Willium lukuvi

Nikama maroboti, wakidhani na kuamini kwamba nje/bila ya ccm hakuna maisha.

wanatetea kwa nguvu kubwa wasichokijuwa wala kukitambuwa, madhali ni hoja ya ccm hatakam ni upumbav.u wao wapo teyari kuufia huo msimamao.

kikundi hiki wanapotetea serikali mbili hawaelezi kabisa wala kugusia ni vipi matatizo na kero hizi vitashughulikiwa

i. serikali ya watu wa zanziba wana rais wao hili likoje

ii. zanziba wana bendera yao hili lipo vipi

iii. zanziba wanawimbo wao wa taifa

iv. zanziba wanakatiba yao

v. zanziba kwasasa ni nchi inamipaka na kila kitu kinachostahili kuitwa inchi

vi. Wazanzibar huku bara ni kwao kule zanzibar pia kwao, lakini watanganyika kule hawapewi vitambulisho vya wakazi

viiwazanzibali wanauwakilishi kwenye serikali huku tanganyika, kule visiwani hatuna wawakilishi

viii wazanzibal wanatutawala huku bara tena wengi tu kama vile ghalib bilali, huseni mwinyi, nk sisi mbona hatuwatawali kule kwao

ix. wazanzibar wanauhuru wa kumiliki ardhi huku Tanganyike, kule kwao watanganyika hawana uhuru huo

achilia mbali, mapato, raslimali nk

hawa akinasendeka wanatoa povu huku kero wakizipiga chenga, huo sio ujanja sanasana ni ushenzi tu
.
 
Back
Top Bottom