Tetesi: Maxcom Africa: Mkataba wa kukusanya faini za barabarani umekwisha?

Tetesi: Maxcom Africa: Mkataba wa kukusanya faini za barabarani umekwisha?

nyumbamungu

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2017
Posts
1,033
Reaction score
895
Habari za jioni wadau, kunatetesi kuwa Mkataba kati ya Maxcom Afrika (Maxmalipo) na Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama barabarani umekwisha na hawajaongezewa muda tena. Tetesi hizo zipo baada ya Jeshi la Polisi Usalama barabarani kukabidhiwa mashine za kutoza faini zinazomilikiwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, sio zile za Maxmalipo.
Tofauti na awali dereva anapopigwa faini ya barabarani alikuwa analipa kwa wakala wa Maxmalipo, lakini kwasasa haziwezi kulipia faini hizo tena. Pia mfumo wa awali uliokuwa unaendeshwa na Maxcom Africa ulikuwa unamsaidia dereva kufahamu kiwango cha malipo anachotakiwa kulipia kwa kupiga (Shot Code) mfumo saidizi, kutumia simu *152*75#
Kwasasa ukitumia mfumo saidizi kuangalia deni *152*75# inarudisha majibu gari halidaiwi, wakati deni lipo. Lakini ukisoma karatasi ya faini ina maelezo lipia tawi lolote la NMB au kwa mitandao ya simu tumia namba ya kampuni 888999.
Tunaomba Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani kutoa elimu kwa umma kutokana na mabadiliko hayo, Kwani ukipiga simu Maxcom Africa kutaka ufafanuzi wa majibu wanayotoa hayana msaada kwa dereva, watakwambia uwatajie namba ya gari waangalie kiwango unachotakiwa ulipie wakitazama mfumo wao unaonesha hakuna deni. Ukweli wangekuwa wazi kwa kuwaambia wanaouliza kuwa kuna mtoza faini mwingine.
 
Ningekuwa naweza kupiga picha muone tofauti ya hizo karatasi zilizokuwa zinatolewa na Maxcom Africa na hizi za sasa zilivyotofauti... Au kwamsaada nifanyeje ilinitume hizo picha??
 
Serikali ime train wataalamu wa kila idara na wenye uwezo wa kutengeneza mifumo ya kukusanya mapato na kuisimamia kwa ujira wa mishahara yao. Haipendezi fedha za serekali kukusanywa au kupitia mikononi mwa mtu binafsi halafu ndipo aziwakilishe serikalini. Anaweza kufanya chochote hapo katikati
 
Miaka ya nyuma kila kitu kilifanyika serikalini na wizi ulikuwa mwingi sana. Tunataka kurudi huko?
Maxmalipo ana create employment.
Huyu mkulu ataua sekta binafsi
 
nyumbayamungu, hili ni tatizo na hamna directives.

Ukipigwa fine ya barabarani kwa sasa, na ukapewa notification ukalipie, huwezi kulipia kwa njia za mtandao kwa kutumia kumbukumbu uliyopewa. Na kibaya zaidi wameandika unaweza pia kulipia NMB bank lakini hawajaweka account no. na wala hamna jina la account. Na hata ukienda NMB, mpaka umpate customer care sahihi ambaye anaufahamu, wengine hawajui.

Aliyeandaaa hiyo notification hakuwa na maono, na wala sidhani kama walifanya majaribio kabla ya kuanza kutumia mfumo rasmi ili wazijue changamoto. Kwa kweli ni usumbufu kwa wengi.

Kibaya zaidi ile karatasi haina maelezo ya notification, kwamba grace period ni siku saba, na usipolipa kwa siku saba gharama zitazidi kuongezeka.

Mfumo wao ni mzuri ila umegubikwa na sitofahamu na maelezo yasiyojitosheleza. Na hata ile number kwenye notification, ukipiga inaita lakini haipokelewi.
 
Miaka ya nyuma kila kitu kilifanyika serikalini na wizi ulikuwa mwingi sana. Tunataka kurudi huko?
Maxmalipo ana create employment.
Huyu mkulu ataua sekta binafsi
Kwahiyo waliomba leseni ili wakusanye fine za traffic?
 
nyumbayamungu, hili ni tatizo na hamna directives.

Ukipigwa fine ya barabarani kwa sasa, na ukapewa notification ukalipie, huwezi kulipia kwa njia za mtandao kwa kutumia kumbukumbu uliyopewa. Na kibaya zaidi wameandika unaweza pia kulipia NMB bank lakini hawajaweka account no. na wala hamna jina la account. Na hata ukienda NMB, mpaka umpate customer care sahihi ambaye anaufahamu, wengine hawajui.

Aliyeandaaa hiyo notification hakuwa na maono, na wala sidhani kama walifanya majaribio kabla ya kuanza kutumia mfumo rasmi ili wazijue changamoto. Kwa kweli ni usumbufu kwa wengi.

Kibaya zaidi ile karatasi haina maelezo ya notification, kwamba grace period ni siku saba, na usipolipa kwa siku saba gharama zitazidi kuongezeka.

Mfumo wao ni mzuri ila umegubikwa na sitofahamu na maelezo yasiyojitosheleza. Na hata ile number kwenye notification, ukipiga inaita lakini haipokelewi.
Kwa hiyo wanatarajia dereva akipigwa fine akapange foleni nmb?????

Kazi kweli kweli
 
Lazima tukiri Maxcom alileta teknolojia ambayo si ngeni duniani ila Tanzania ilisaidia sana. Amemkimbiza Selcom kwenye sekta.

Na fedha alipiga kweli sababu aliaminiwa yeye kama yeye, hakukuwa na connected platform ya kuona anachokusanya.
 
Lazima tukiri Maxcom alileta teknolojia ambayo si ngeni duniani ila Tanzania ilisaidia sana. Amemkimbiza Selcom kwenye sekta.

Na fedha alipiga kweli sababu aliaminiwa yeye kama yeye, hakukuwa na connected platform ya kuona anachokusanya.
Kuiba ilikuwa ngumu kwa sababu nakumbuka kamanda Mpinga aliwahi sema, Police wana server zao ambazo ndipo Maxcom alikuwa ana connect kwa hiyo data zilizopo Maxcom zipo pia Police. Utaibaje?
 
Ni hatua nzuri kwasababu serikali itapata mapato mengi zaidi.

Maana ile commision ya maxmalipo kuwa kama wakala wa ukusanyaji haipo tena hivyo pesa zote zinarudi serikalini.

Sema serikali wakati huu kiboko hata 7saba mwaka jana Maxcom ndo walikua wakala wa ukusanyaji mapato ila mwaka huu naona wamepewa chuo cha UDSM chini ya college yao ya UCC so mapato yatarudi kwenye taasisi ya serikali vile vile
 
Sioni mazingira ya kuistawisha sekta binafsi yakijengwa. Mtindo wa serikali kumiliki njia zote za uchumi ni katika nchi za kijamaa.

Kama tungekua tunajitegemea kwa kila kitu isingekua na tatizo kabisa.
Tusubiri na kuona.
 
Kaondolewa Saba Saba pia kapewa UCC/UDSM
TRA nao watamtosa soon,
DART nao wanatengeneza mfumo wao ili mtu wa kati asiwepo
Afu ubaya wamekopi mfumo wake

Maximalipo atabakia kuuza vocha........ Naona sote twaisoma namba
 
Back
Top Bottom