Mayele Vs Phiri

kwisha

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2021
Posts
1,779
Reaction score
4,982
Kuna ubishi siku hizi ambao unaendelea kwa watu wakilinganisha Mayele na Phiri. Kuna watu wanasema Phiri siyo stricker kama Mayele, bali ni kiungo mshambuliaji.

Kwahiyo goli zake nyingi anafunga kwa kujitafutia mpira au kwa mwenyewe, kitu ambacho siyo kweli.

Kama wewe ni mfatiliaji mzuri wa mechi za Simba utakubaliana na mimi jambo hili. Goli nyingi za Phiri ni mipira ya kutengewa na Chama au wachezaji wengine, ila anyway lengo langu siyo hilo.

Nataka tu ukweli kuhusu uchezaji wa Phiri na Mayele. Phiri ni faux number 9 ambaye anacheza kama namba 10 au 7 au 11 lakini namba yake halisi kabisa ni 9, mfano ni kwa Mbape na Ronaldo.

Mbape kipindi cha Cavani alikuwa anacheza kama namba 7 huku akitokea pembeni, lakini goli zake nyingi alikuwa anafunga akiwa kama namba 9 kwa kutoa pass kwa wenzake halafu anakimbilia kwenye box haraka sana kusubiri mpira. Na ndivyo Phiri naye anavyocheza. Kwahiyo ni vigumu kutambua kama ni namba 9 lakini hatulii kwenye namba yake.

Mayele naye siyo stardup scricker kama watu wanavyo dhani, Mayele akiwa ndani yq uwanja mara nyingi anacheza kama namba 10 siyo mtu wa kutulia sana kwenye eneo lake.

Ni mtu ambaye anaanzisha mashambulizi, akipata mpira anatoa pass halafu anakimbilia kwenye box, ndivyo naye anacheza. Mfano ni mechi ya Simba ile ngao ya jamii na zingine nyingi tu amekuwa akifanya hivo.
 
Kuna ubishi siku hizi ambao unaendelea kwa watu wakilinganisha Mayele na Phiri.

Kuna watu wana sema phiri sio stricker kama mayele bali ni kiongo mshambuliaji.
Sijakuelewa Unasema Phiri kafanyaje🤔🤔🤔
 
Faux 9 ndio nini? Na hiyo stardup scricker ndio nini?

Kwahiyo phiri ni faux namba 9 na mayele ni stardup scricker.

Tuachane na hivyo viwili huwenda ni makosa ya uandishi tu.
Soma tena uchambuzi wako.
Hii ndio aina ya wachambuzi tulionao kwenye soka letu, wanachoongea mwanzo mpaka mwisho wengi wao hawaeleweki eleweki.
Points zao hazina uzito, ni kama wabahatishaji.

Ukisikiliza kwenye radio au kuwatizama unabaki unatabasamu tu, hawa ni football pundits kweli au wachumia tumbo tu!!
 
Mayelle yuko special hata mimi nisiyejua mpira wala wachezaji ninamjua Mayelle
 
Wote hao ni wageni..baadae timu yenu ya taifa ikipakatwa mnaanza kusema hamna wachezaji....amkeni wenzenu kwenye timu kubwa wanajitahidi kuweka wazawa ili wapate uzoefu
 
Na hili ndilo linalothubitisha kauli ya manara kuwa pale yanga wenye akili timamu ni wawili tu.
 
Moses unamfananisha na fifimoto mtingisha manyonyo?!!!!!!khaaaaa utakuwa na shida kichwani
 
Mayele ameachieve nini kwani mpk mnampigia makelele hivi, si ni huyu msimu uliopita kapitwa na kijana G. Mpole ambaye alikuwa anacheza kwenye timu isiyo na wachezaji bora kama alipokuwa Mayele!!

Kwa maana nyingine Mpole angekuwa hapo jangwani angefunga mengi zaidi, msimu huu mpk sasa hivi wamefungana magoli sasa kelele za huo ubora zinatokea kwenye nn kuwafunga Zalan?
 
Samia ana kazi kubwa sana hasa kudeal nawatu wanaojiita mashabiki wa Simba. Hebu angalia uwasilishaji wao hasa post namba 17,18, 19.

Umbumbumbu ni kipaji asee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…