Mazingatio

SIR CAPTAIN

Member
Joined
Aug 9, 2019
Posts
29
Reaction score
10
Kuna mwalimu mmoja aliingia darasani akaandika ubaoni kama ifuatavyo
(1) 9+1=70
(2) 9+2=11
(3) 9+3=12
(4) 9+4=13
(5) 9+5=14
(6) 9+6=15
(7) 9+7=16
(8) 9+8=17
(9) 9+9=18
(10) 9+10=19

Alipo maliza kuandika tu, akaona wanafunzi wote walikua wanacheka, kwasababu alikua amekosea swali la kwanza.

Akawatazama wanafunzi, kisha akawaambia yafuatayo:
```"Nimejikosesha lile swali la kwanza makusudi, kwasababu nilihitaji mjifunze kitu kimoja muhimu sana.Mnapaswa kujua namna ambavyo dunia inaweza kuwachukulia. Unaona hapo, nimeandika kwa usahihi maswali tisa (9), lakini hakuna kati yenu aliyenipongeza kwa hilo; wote mmecheka na kunilaumu kwasababu ya kosa moja tu nililofanya."```

#HIVYO, HILO NI SOMO KWENU:

Dunia haijali mazuri unayofanya hata ukiyafanya mara milioni, lakini fanya baya moja uone jinsi watakavyo kulaumu..`

Hata hivyo usikate tamaa, mara zote simama imara na ushinde vikwazo vyote .Huu Ndio Ujumbe wangu kwenu leo...

#Timiza malengo yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…